Hivi kwanini jamii ya kitanzania hatuwezi kufanya biashara ya kifamilia

Hivi kwanini jamii ya kitanzania hatuwezi kufanya biashara ya kifamilia

Kazanazo

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2023
Posts
5,557
Reaction score
8,195
Watanzania tulio wengi tumeshindwa kabisa kufanya biashara ya pamoja kama wanafamilia au watu wa ukoo mmoja kwanini?

Tofauti na jamii za kiarabu, kihindi na hata familia nyingi za kizungu hudumisha tamaduni hii ya biashara za kifamilia. Yani kutoka kwa muasisi (hasa alieleta mageuzi ya kiuchumi) familia huendeleza biashara hizo na kurithishana kizazi hadi kizazi bila kuuza wala kugawanywa kwa warithi. Hii husaidia familia hizi kutoanza kutoka mavumbini kama tulivyo wengi wetu hapa tz,

Familia nyingi za kitanzania baada ya kufa muasisi awe Baba au mama wa familia watoto huanza kugombania Mali na kugawana assets au kuziuza kabisa na kugawana hela. Yani hawawezi kuthubutu kutunza na kuendeleza alipoishia muasisi na kufanya biashara hizo au uwekezaji kuwa mkubwa kwa ajili ya kunufaisha kizazi kilichopo na kuandaa warithi kwa ajili ya vizazi vingine

Wengi wa walioacha uwekezaji mkubwa mali zao huishia kuuzwa au kugawanywa au tena kama kaacha wosia mali zisiuzwe basi watoto hawawezi kuendeleza kutoka moja kwenda mbili na tatu bali watabweteka na macho yote yatakuwa kwenye mirathi hiyo iwafanyie kila kitu wala hawatashughulika kuitunza wala kuiendeleza na kuwekeza zaidi mwisho wa siku wanaishia kugombana na kesi zisizoisha mahakamani

Je, elimu ndio tatizo?

Je wewe kama mwanafamilia unaona nini kikwazo?

Je ni kweli biashara za kifamilia hazina tija kwa familia za kitanzania?

Kama ipo tija nini kifanyike?

Umeweka mikakati gani kuhakikisha kizazi chako kinaendeleza unachokifanya?

Karibu tujadili.
 
Kutokuandaliwa toka utotoni ili kuja kuendeleza biashara za wazazi wao,wazazi kua wasiri kwenye biashara zao na kutowashirikisha watoto wao,

Waarabu,wahindi na hao wengineo,huwaandaa watoto wao kuja kuendeleza biashara zao,
Wazazi wengi wa kibongo hawana tabia hiyo,watoto hawaandaliwi kuja kushika biashara za wazazi wao,

So,kwavile hawana maandalizi wala experience,hiyo biashara huishia kufilisika tu na kufa,
Pia biashara inahitaji nidhamu ya hali ya juu sana,na hayo yote hupatikana kuanzia kwenye malezi ya mtoto mpaka makuzi yake.
 
Kutokuandaliwa toka utotoni ili kuja kuendeleza biashara za wazazi wao,wazazi kua wasiri kwenye biashara zao na kutowashirikisha watoto wao,

Waarabu,wahindi na hao wengineo,huwaandaa watoto wao kuja kuendeleza biashara zao,
Wazazi wengi wa kibongo hawana tabia hiyo,watoto hawaandaliwi kuja kushika biashara za wazazi wao,

So,kwavile hawana maandalizi wala experience,hiyo biashara huishia kufilisika tu na kufa,
Pia biashara inahitaji nidhamu ya hali ya juu sana,na hayo yote hupatikana kuanzia kwenye malezi ya mtoto mpaka makuzi yake.
Ni kweli lakini si unaweza ukazisajili mali zako na kuzikabidhi kwa wataalamu wa biashara kama unaona watoto wako hawana uwezo wa kuziendeleza
 
Unawajua mashangazi kweli na baba wadogo na wakubwa wasio na haya wala utu,,

Kila mtu apambane na mzgo wake
Wana gubu kama baba wa kambo 😃

Sasa tutaanza kila siku hadi lini? Inawezekanaje mzee kaacha hekalu ambapo kila mwanafamilia anaweza akaishi humo lakini niteseke kuanza kutafuta hela ya kiwanja, nijenge nitafute na pesa za biashara kwa vibarua wakati mzee aliacha biashara nzuri ni kuendeleza tu. Na sasa mkigawana hata pesa ya boda haitoshi
 
Wana gubu kama baba wa kambo 😃

Sasa tutaanza kila siku hadi lini? Inawezekanaje mzee kaacha hekalu ambapo kila mwanafamilia anaweza akaishi humo lakini niteseke kuanza kutafuta hela ya kiwanja, nijenge nitafute na pesa za biashara kwa vibarua wakati mzee aliacha biashara nzuri ni kuendeleza tu. Na sasa mkigawana hata pesa ya boda haitoshi
Hahahaha hatare sana,,
 
Kwanza inabidi tujenge uwezo wa kuendesha biashara kwa miaka zaidi ya 20. Hakafu ndio tuangalie uwezekano wa kurithisha. Sasa biashara haitoboi miaka 10 itaendelezwa vipi na kizazi kijacho?
 
Kwa sababu mna roho mbaya, husda, wizi, utapeli na mnaamini sana ushirikina.

Hamuamiani kabisa, hata mwanao anakuibia na mke ndio usiseme kabisa

Tofauti na jamii zingine ambazo zinaamini kuacha kitu kwa vizazi vyao
 
Kwanza inabidi tujenge uwezo wa kuendesha biashara kwa miaka zaidi ya 20. Hakafu ndio tuangalie uwezekano wa kurithisha. Sasa biashara haitoboi miaka 10 itaendelezwa vipi na kizazi kijacho?
Sio zote zingine zimefanikiwa na hadi kupita hicho kiwango

Wilaya ninayoishi kuna mbunge alikuwa na kampuni ya magari ya abiria na biashara kadhaa lakini alivyokata moto watoto wamegawana mabasi na kuuza zingine hadi sasa hiyo kampuni haipo tena
 
Nini kifanyike kiongozi ni kweli tuendelee kuwa masikini na kuanza upya kila siku ilhali wazazi wetu waliteseka kwa ajili yetu?

Je wewe watoto wako unawaandaaje?
(Je wewe watoto wako unawaandaaje?)_usirudie tena kuniuliza mambo haya tutapigana .

Sasa nitoe ushauri baada ya biti kali kwa rafiki yangu .

Naona iwe ni jukumu mama kwa wazazi kukiandaa kizazi chao kurithi mali na kuziendeleza lakini hapo pia nikukumbushe kwa uchache japo sio kwa umuhimu kuwa shida ya hayo yote mbali na habari za ndugu pande za wazazi kuingilia watoto lakini suala kubwa la wazazi kuamini kwenye elimu kuwa mpe mtoto elimu ili akimaliza aajiriwe ndiyo sababu kuu ya uzorotaji wa maendelezo wa mali za urithi

Kivipi hii inakuwa ,ni pale mtoto unamtupa shuleni hakuna habari ya hata siku moja ushinde naye dykani walau aone vipi unabembeleza wateja au unajinyenyekeza ili watu wanunue bidhaa sasa mtoto wa hivyo hata kesho ukifa haelewi aanzie wapi


Watoto wapate elimu ila wafundishwe pia kuwa mbali na ajira kuna ajira binafsi pia kama wanazofanya wazazi .

Nafurahi kuona jamii kwasasa imeanza kuamka kwa kuamini kuwa kwenda shule hakumfanyi mtoto kuwa tajiri ila juhudi ,ujuzi na bidii ndiyo msingi wa mafanikio .

Ahsante kaka ,karibu tena kaka Kazanazo
 
Mimi Nadhani inachangiwa pamoja na mfumo wa makazi. Jamii ulizozitaja zina desturi ya kuishi pamoja kama familia hata kijana anapooa. Wanaishi kiukoo. Hii inarahisisha upangaji wa mipango ya kifamilia na pia inarahisisha kudhibiti tabia chonganishi/tawanyishaji toka kwa walioingia ukoo wenu kupitia ndoa. Sisi wabantu wengi tunaishi tofauti. Ukikomaa tuu huyoooo kaishi kuleeee na mkeo. Inakuwa vigumu kufanya vitu kama biashara ya familia pamoja.
 
(Je wewe watoto wako unawaandaaje?)_usirudie tena kuniuliza mambo haya tutapigana .

Sasa nitoe ushauri baada ya biti kali kwa rafiki yangu .

Naona iwe ni jukumu mama kwa wazazi kukiandaa kizazi chao kurithi mali na kuziendeleza lakini hapo pia nikukumbushe kwa uchache japo sio kwa umuhimu kuwa shida ya hayo yote mbali na habari za ndugu pande za wazazi kuingilia watoto lakini suala kubwa la wazazi kuamini kwenye elimu kuwa mpe mtoto elimu ili akimaliza aajiriwe ndiyo sababu kuu ya uzorotaji wa maendelezo wa mali za urithi

Kivipi hii inakuwa ,ni pale mtoto unamtupa shuleni hakuna habari ya hata siku moja ushinde naye dykani walau aone vipi unabembeleza wateja au unajinyenyekeza ili watu wanunue bidhaa sasa mtoto wa hivyo hata kesho ukifa haelewi aanzie wapi


Watoto wapate elimu ila wafundishwe pia kuwa mbali na ajira kuna ajira binafsi pia kama wanazofanya wazazi .

Nafurahi kuona jamii kwasasa imeanza kuamka kwa kuamini kuwa kwenda shule hakumfanyi mtoto kuwa tajiri ila juhudi ,ujuzi na bidii ndiyo msingi wa mafanikio .

Ahsante kaka ,karibu tena kaka Kazanazo
😃😃 nimecheka kwa sauti sio kwa biti hilo, niseme sitarudia kiongozi ila pia shukran kwa ushauri mzuri maana elimu ya kuajiriwa nayo ni kikwazo kwa watoto ni bora wafanye vyote kama ulivyoshauri hapo
 
Kwanza inabidi tujenge uwezo wa kuendesha biashara kwa miaka zaidi ya 20. Hakafu ndio tuangalie uwezekano wa kurithisha. Sasa biashara haitoboi miaka 10 itaendelezwa vipi na kizazi kijacho?
Sisi tunachojua tu ni kukata mauno tajiri anapofilisika ama kugongewa mke.

giphy.gif
 
Kwanza inabidi tujenge uwezo wa kuendesha biashara kwa miaka zaidi ya 20. Hakafu ndio tuangalie uwezekano wa kurithisha. Sasa biashara haitoboi miaka 10 itaendelezwa vipi na kizazi kijacho?
Hili nalo neno.
 
Mimi Nadhani inachangiwa pamoja na mfumo wa makazi. Jamii ulizozitaja zina desturi ya kuishi pamoja kama familia hata kijana anapooa. Wanaishi kiukoo. Hii inarahisisha upangaji wa mipango ya kifamilia na pia inarahisisha kudhibiti tabia chonganishi/tawanyishaji toka kwa walioingia ukoo wenu kupitia ndoa. Sisi wabantu wengi tunaishi tofauti. Ukikomaa tuu huyoooo kaishi kuleeee na mkeo. Inakuwa vigumu kufanya vitu kama biashara ya familia pamoja.
Hili nalo ni tatizo tunaishi kibepari zaidi na sio kijamaa

Lakini tuchukue mfano wa familia za kizungu kama vile Gates, Rockefeller na Ford ambazo zinaishi kibepari kama sisi lakini zimeweza kudumisha tamaduni ya biashara za kifamilia toka kwa muasisi hadi sasa, wao wanafanyaje?

Kuna kitabu nimesoma kuwa huwa wanasajili Mali zao na kuziweka under trust au Foundation ambapo wataalamu wa uchumi huajiriwa kwa ajili ya kusimamia mali na biashara za warithi huku warithi wenyewe wakiwa kama wasimamizi wakuu na wenye maamuzi

Kwa njia hii hata kama huyo mtoto atakuwa anaishi kivyake haizuii uendelezwaji wa mirathi na haki zake pia hazipotei
 
Back
Top Bottom