Mimi nilisimamia uchaguzi, kituo changu matokeo yalikuwa hivi, Tundu Antipas Lissu kura 79 Magufuli kura 31 lakini matokeo yalibandikwa Tundu Antipas Lissu kura 6 Magufuli kura 370 . hapakuwa na uchaguzi ilikuwa ni ujinga tu.
Binafsi sina shaka kabisa na ulichokisema hapa. Hivi ndivyo ilivyokuwa. Huu haukuwa uchaguzi bali yalikuwa maigizo tu ya uchaguzi...
Mathalani, Mimi katika kata niliyosimamia wizi na uigizaji huu ulikuwa dhahiri shayiri kabisa...
Nitaeleza;
Kwamba amini usiamini, Mtendaji kata wala hakujisumbua kufanya compilation ya matokeo ya vituo vyote katika kata yake ili ampate mshindi wa udiwani na kumtangaza...
Kikawaida baada ya wasimamizi wa vituo vya kupigia kura kukamilisha kazi ya kuhesabu na ku - compile matokeo ya kituo, unayatangaza na kuyabandika nje ya kituo cha kupigia kura ukutani ili wananchi waone..
Baada ya hapo unabeba masanduku ya kura na fomu za matokeo zote udiwani, ubunge na urais hadi kwa msimamizi msaidizi uchaguzi wa kata. Naye atapokea matokeo ya kila kituo katika kata yake na kuyajumuisha na kisha kumtangaza diwani mshindi wa kata husika...
Sasa soma kwa makini hapa chini kilichotokea makao makuu ya kata niliyosimamia;
Kwamba, mpaka kufikia saa 5 usiku, karibu wasimamizi wote wa vituo vyote vya kata ile walishafika na kukabidhi fomu za matokeo ya udiwani..
Jambo lililotushangaza ni kuwa mpaka saa 7 ya usiku siku hiyo jamaa tulimuona akiwa yupo yupo tu. Tunamuuliza mbona huyajumuishi matokeo na kuwatangazia watu mshindi wa udiwani kisha waondoke zao?
Jamaa alikuwa anaguna guna tu. Kumbe alikuwa anasubiria matokeo ya kutumwa toka "somewhere" na baadaye akayabandika kuonesha mCCM ameshinda wakati huohuo sisi wasimamizi wa vituo tukiwa na picha kamili kabisa na uhakika wa 100% kuwa CHADEMA walishinda mafiga yote (udiwani, ubunge na Urais) katika kata X ile niliyosimamia mimi na wenzangu...
We were very shocked and surprised as well...!!
Later on wasimamizi wakuu wote wa vituo tukabebwa usiku uleule kwenda makao makuu ya Halmashauri ya wilaya kupeleka masanduku ya kura na fomu za matokeo ya kura za Ubunge na Urais...
Surprisingly, huko nako matokeo tuliyoyakuta na kutangazwa ni tofauti kabisa na uhalisia wa matokeo ya kwenye vituo vya kupigia kura tuliyokuwa nayo sisi...
That was too bad and disgusting in deed...
Ni KWELI na HAKIKA kuwa CCM walichakazwa vibaya sana ktk sanduku la kura kwenye uchaguzi mkuu wa tarehe 28/10/2020....
å CHADEMA na Tundu Lissu kwenye Urais alishinda kwa zaidi 70% ya kura zote...!
å CHADEMA kwenye ubunge, walishinda zaidi ya 60% ya majimbo yote...!!
å CHADEMA, walishinda udiwani kwa zaidi ya 60% ya kata zote Tanzania nzima...!!
### Hili halina shaka wala ubishi kuwa, Magufuli na CCM KAMWE hawakushinda uchaguzi huu...
### Hili halitapita hivi hivi. Karma lazima itaadhibu watu tu. Huwezi iba haki za watu ukaachwa na ukabaki kama ulivyo...!!