Luca Paguro
JF-Expert Member
- Mar 26, 2023
- 476
- 1,060
Nauliza tu kazi ya wabunge Tanzania ni nini?
Sisi kwenye Civics tuliambiwa kazi kuu ya Mbunge ni kuwawakilisha wananchi, sasa mbona kero za wananchi hatuoni zikijadiliwa kwa wingi bungeni?
Wananchi wanadai Katiba Mpya, Uchaguzi Huru na wa Haki, wanataka waweze kukosoa serikali kwa uhuru bila kuhofia kutekwa, wanataka mazingira mazuri ya kuajiriwa na kujiajiri, nk. Haya yote yanahitaji watu smart wa kuyajadili na kuyafanyia ufumbuzi.
Ukisema maisha ni magumu kwa mamilioni ya Watanzania, watu wanasema serikali haiwezi kukuletea hela nyumbani kwako, ukikosoa serikali wanakuita mhaini, ukiongea kuhusu miundombinu mibovu serikali inafumba macho, kama jinsi mikoani tunavyoteseka na shida ya maji.
Maana yake matatizo ya wananchi hakuna anayeyasikiliza, na mengi wanasema sio kazi ya serikali au wanayapuuzia, ukiyataja wanasema wewe sio mzalendo!
Sasa kama wananchi wenyewe ndio sisi, na hakuna wa kutetea kero zetu bungeni, kazi ya wabunge huwa ni nini? Kwamba ubunge imekuwa tu kazi ya kukimbiliwa ili kupata posho, mishahara mikubwa, magari ya kifahari na mafuta full tank?
Wabunge wanalipwa hela kubwa, tena nchi masikini kama Tanzania inawanunulia magari ya kifahari, inawajazia na mafuta, wanapewa posho nyingi na mishahara mikubwa na sijui kama wanalipa kodi hawa. Wamekuwa wakilipwa hivi kwa miaka na miaka ila kero za wananchi kila siku zinaongezeka badala ya kupungua!
So, kazi ya wabunge ni nini?
Sisi kwenye Civics tuliambiwa kazi kuu ya Mbunge ni kuwawakilisha wananchi, sasa mbona kero za wananchi hatuoni zikijadiliwa kwa wingi bungeni?
Wananchi wanadai Katiba Mpya, Uchaguzi Huru na wa Haki, wanataka waweze kukosoa serikali kwa uhuru bila kuhofia kutekwa, wanataka mazingira mazuri ya kuajiriwa na kujiajiri, nk. Haya yote yanahitaji watu smart wa kuyajadili na kuyafanyia ufumbuzi.
Ukisema maisha ni magumu kwa mamilioni ya Watanzania, watu wanasema serikali haiwezi kukuletea hela nyumbani kwako, ukikosoa serikali wanakuita mhaini, ukiongea kuhusu miundombinu mibovu serikali inafumba macho, kama jinsi mikoani tunavyoteseka na shida ya maji.
Maana yake matatizo ya wananchi hakuna anayeyasikiliza, na mengi wanasema sio kazi ya serikali au wanayapuuzia, ukiyataja wanasema wewe sio mzalendo!
Sasa kama wananchi wenyewe ndio sisi, na hakuna wa kutetea kero zetu bungeni, kazi ya wabunge huwa ni nini? Kwamba ubunge imekuwa tu kazi ya kukimbiliwa ili kupata posho, mishahara mikubwa, magari ya kifahari na mafuta full tank?
Wabunge wanalipwa hela kubwa, tena nchi masikini kama Tanzania inawanunulia magari ya kifahari, inawajazia na mafuta, wanapewa posho nyingi na mishahara mikubwa na sijui kama wanalipa kodi hawa. Wamekuwa wakilipwa hivi kwa miaka na miaka ila kero za wananchi kila siku zinaongezeka badala ya kupungua!
So, kazi ya wabunge ni nini?