Kazanazo
JF-Expert Member
- Aug 16, 2023
- 5,557
- 8,193
Maadili ni neno pana ila linaloeleweka kiasi kwamba ukizungumza kuhusu maadili kikawaida mtu atafikiria moja kwa moja matendo mema
Katika jamii ya sasa ya kitanzania sijui kama kuna watu wema wenye matendo mema, lugha za staha, malezi bora na mavazi ya heshima kama wapo ni asilimia chache sana. Kumejaa watu wazima wasio na utofauti na watoto au vijana wao, ni kawaida kumuona kijana mdogo akiongea matusi na mtu mzima wenyewe wakiona ni moja ya utani
Familia zimekuwa mbovu kiasi kwamba mkubwa na mdogo hawajulikani, hakuna heshima wala aibu katika maongezi yao. Maneno yaliyojaa matusi na lugha mbovu baina ya wakubwa na wadogo ndio lugha zao za kutaniana
Japo nimezaliwa miaka ya 90's lakini katika umri wangu wa utoto sijawahi kuyashuhudia ninayo yashuhudia sasa, kipindi napata akili kulikuwa na utofauti wa marika na kulikuwa na gap baina ya Marika haya ni ngumu kukuta kijana akitukanana na mtu mzima kama sehemu ya utani
Binafsi natamani nikaanzishe kanchi kangu mimi na familia yangu tukaishi huko huenda tukaishi kwa amani, maadili na tabia njema hii jamii ya sasa haiendani kabisa na malezi niliolelewa
Nawasilisha hili kwa jamii ahsanteni
Katika jamii ya sasa ya kitanzania sijui kama kuna watu wema wenye matendo mema, lugha za staha, malezi bora na mavazi ya heshima kama wapo ni asilimia chache sana. Kumejaa watu wazima wasio na utofauti na watoto au vijana wao, ni kawaida kumuona kijana mdogo akiongea matusi na mtu mzima wenyewe wakiona ni moja ya utani
Familia zimekuwa mbovu kiasi kwamba mkubwa na mdogo hawajulikani, hakuna heshima wala aibu katika maongezi yao. Maneno yaliyojaa matusi na lugha mbovu baina ya wakubwa na wadogo ndio lugha zao za kutaniana
Japo nimezaliwa miaka ya 90's lakini katika umri wangu wa utoto sijawahi kuyashuhudia ninayo yashuhudia sasa, kipindi napata akili kulikuwa na utofauti wa marika na kulikuwa na gap baina ya Marika haya ni ngumu kukuta kijana akitukanana na mtu mzima kama sehemu ya utani
Binafsi natamani nikaanzishe kanchi kangu mimi na familia yangu tukaishi huko huenda tukaishi kwa amani, maadili na tabia njema hii jamii ya sasa haiendani kabisa na malezi niliolelewa
Nawasilisha hili kwa jamii ahsanteni