Nimeyasoma maandishi ya ndugu yangu,nimejiridhisha kwamba mwandishi ni sawa na fungu la kukosa,amewasilisha kilio cha malalamiko kupata huruma asiyostahili,akijazilisha hoja zake kwa maneno mengi yasiyokuwa na chembe ya ukweli,mimi ntamjibu hoja kwa hoja,nikitumia uzoefu wangu katika uhudumu wa mifuko mbalimbali ya jamii nchini na nje ya nchi yetu,KWANZA-ni kweli kwamba,wafanyakazi wa mashirika ya umma wanapaswa kuwa chini ya masharti ya kudumu na pensionable,na katika hoja hii,ni vema nikamfahamisha mwandishi na wadau wa fikra pevu kwamba,dai la mwandishi lilishatekelezwa mda kitambo yapata mwaka wa pili sasa,na hii ni baada ya sheria inayounda mashirika ya umma kwa mfuko wa ppf kubadilishwa na kurudi kwenye utaratibu wake wa awali kama ilivyokuwa mpaka mwaka 2003,kuileta hapa kama hoja mpya,ni kuvia fikra na kutaka kuaminisha umma wa wanafikra vitu vya uongo na uzushi kwenye jambo linalohitaji majibu ya fact badala ya maoni binafsi ya mwandishi au mlalamikaji.-kwa sasa nadiliki kuliita dai hili la mwandishi mlalamikaji kama dai lisilo na mashiko.
PENYE RED
1.Erio usiwe mwongo kiasi hicho. Mwezi March mwaka huu wakurugenzi wako walimaliza mikataba leo unasema miaka miwili iliyopita mlibadili (UKIWA MUONGO JITAHIDI USIWE MSAHAULUFU)
2. Ukawalipa gratuity na Group Endowment, ukawaongezea mkataba wa miaka mitatu, baada ya mwezi mmoja tu, ukawabadilishia ajira kuwa za kudumu. Ukawalipa gratuity ya mwezi mmoja. Je huu ni uongo wa mwandishi?
Mbili:-hoja au dai la pili la mwandishi ni dai mufilisi,mwandishi anashindwa kujua kwamba,hoja au nia ya malipo ya gratuity,sii hoja ya mtu binafsi kuja nayo mfukoni,maamuzi yote ya malipo katika ajira za ppf kama tunavyotaraji kuwa katika mifuko mingine ya jamii huamuliwa na bodi ya mfuko wa ppf,sii busara wala hekima,kutoa zigo la tuhuma kwa mtu,katika maamuzi ambayo yeye ni mjumbe tu,ikumbukwe kwamba bodi ya ppf,inaundwa na watu wengi na wenye uwezo na uzoefu katika nyanja mbalimbali,tena wakitoka maeneo mbalimbali ya kikazi,ikiwemo uwakilishi wa muhimili wa bunge,wizara ya fedha na taasisi nyingine za kiserikali,dg wa ppf,anakuwa sehemu tu ya wajumbe,na inapolazimu mambo mengine huamliwa atoke nje ya kikao husika ili wajumbe wa bodi wawe huru zaidi katika kujadili afya ya mfuko wa ppf,ikiwemo malipo ya wafanyakazi wanaomaliza mikataba yao ya mda mfupi na mrefu,ushahidi upo wazi,ppf imekuwa mstari wa mbele kuwalipa mafao wafanyakazi wake pindi wanapofikia tamati ya mikataba yao ya utumishi kwa wakati muafaka,na ndio maana hakuna mahala ppf imewahi kulalamikiwa na wafanyaklazi wanaomaliza mikataba yao kuwa eti hawajalipwa inavyostahili,haya ni maneno na maono binafsi ya mwandishi au mlalamikaji huyu,nadiriki kuyaita majungu ya ofisini,ambayo kwa tanzania ni sehemu ya maish-itoshe tu kusema mwandishi au mlalamikaji ana hoja dhaifu,anajaribu kupaza sauti isikike.
PENYE RED: Alhaji Kilima, ulimlipa ipasavyo? Engineer Mwageni na F. Mbala uliwalipa group endowment japo walitumikia mfuko zaidi ya miaka sita? Walileta madai yao kuwa hawajalipwa endowment mkawajibu kuwa wao walikuwa wa mikataba, ninyi mlikuwa wa nini? Jibu hii tuhuma vizuri. Ukiijibu, nazimwaga hapa JF communication zenu zote ili umma uamue nani mwongo.
HOJ YA TATU-nianze tu kwa kusema hasidi hakosi sababu kama msemo wa kiswahili unavyotufunza,ni kejeli na uwongo wa mchana kweupe kusema eti hazina imelala,na kufumbia macho kupuuzwa kwa waraka wa utumishi-kwa taarifa tu,ppf-kama nilivyosema awali inaundwa na bodi,dg ni mjumbe,hazina ni mdau wa bodi,bunge lina uwakilishi katika bodi hii,wizara ya fedha ina uwakilishi,kwa pamoja wajumbe wa bodi walijiridhisha na kuidhinisha malipo ambayo ndugu yangu anayalalamikia,katika maamuzi yanayomgusa dg,bodi humuondoa nje kikao mkurugenzi ili kuwa huru kujadili jambo linalohusu maslahi yake kwa uhuru,wanabodi walijiridhisha wakaidhinisha malipo,nimwombe mwandishi awe muungwana kukubaliana na maazimio ya bodi ya mfuko badala ya kumalizia kinyongo chake kwa ndugu dg,bodi ilipitisha malipo ya watumishi,haiojalishi watakuja wa majina gani,leo ni erio,kesho atakuja saiboki,au atakuja manka,ni vema wanafikra pevu,tufunzane kujadili mifumo kuliko kujadili watu.maana kwa maazimio ya bodi ya ppf,hata mwandishi wa malalamiko haya akipata nafasi ya erio kuwa dg,atalipwa kwa maelekezo haya ya bodi,narudia kumshauri,aandike hoja mantiki na sii hoja nyongo.
PENYE RED
Hivi PPF kweli mna BODI au kivuli? Bodi ya PPF hufuata yale unayoyataka wewe, FEDHA FEDHEHA, Mwenyekiti wako mshahara wake aliko hauzidi sitting allowance ya kikao kimoja, kwa nini asikutii? Wanakujua kuwa una nguvu sana kwenye kuteua wajumbe wa Bodi maana Waziri wa Fedha umeshika vilivyo kifedha na pia umemrushia KIBURUDISHO.
Hapa hakuna kinyongo chochote.
HOJA YA NNE,-Hapa nimsaidie mwandishi,kumchangia mtumishi asilimia au gawio kat ika pension yake ,ni haki ya msingi kwa mwajiriwa,naamini iwe ppf au katika eneo lingine la ajira,haijalishi ni kiwango gani cha mshahara mtumishi analipwa,katika hili,mwandishi ameonyesha kinyongo cha kupitiliza kwa anaowatuhumu,narudia kumpa ushauri wa bure,mwandishi,malipo ya ppf-yanamlenga mtumishi katika ngazi fulani,ama dg,au mkurugenzi au mkuu wa kitengo,hayalengi jina la mtu,hata kama ni yeye ataajiliwa ppf,stahili hizi anazozilalamikia kwa dg,atalipwa yeye,maana anamjadili dg kama mtu binafsi,badala ya kumjadili dg kama mtumishi wa umma,
PENYE RED: Ndugu yangu, usidhani JF ni watu waliokosa akili za kufikili. Waonee hao wafanyakazi wako tu.
Ni kweli kumchangia mtumishi wa ni haki lakini sio mtumishi wa UMMA aliye amua kuwa kwenye ajira ya Mkataba. Wa ajira ya mkataba hupata gratuity sio kuchangiwa pension. Mbona waraka wa Utumishi uko wazi? Unataka niweke humu jinsi ulivyomdanganya Katibu Mkuu Luhanjo kwa kuhusu Pension za wakurugenzi wako? Unataka niweke humu jinsi mlivyoomba mrudishiwe michango yenu ya 2003-2008 na majibu ya Hazina pamoja na ya Luhanjo baada ya kukustukia?
Sipendi kumchafua Luhanjo kwa kuwa aliwajibu kutokana na kutokumpa taarifa sahihi (KUMPA UONGO)
HOJA YA TANO;-Mwandishi anajichanganya,dg hakujilipa kama anavyotaka umma wa wanafikra uamini,bali sentesi sahihi ni bodi ya ppf,ilikubali kuidhinisha malipo ya mkurugenzi na wakurugenzi wa idara,na sii kweli kwamba watu wa hazina walikataa kusaini,huu ni ulaghai kwa watu maana hazina ni sehemu ya uwakilishi katika bodi ya ppf,na kwa taarifa tu ni kwamba,hakuna jambo linalofanyika ndani ya ppf bila kuwa na idhini au baraka za bodi na wizara ya fedha kama mdau wa serikali,unless kama mwandishi anatafuta wapi apake tope lake,lakini kiuhalisia hoja yake ni hoja maslahi yake binafsi yenye lengo la kupotosha na kuharibu utendaji wa mtu,kama wanafikra tabia hii ni vema tukaiepuka kwa faida ya tanzania tunayoitaka.
PENYE RED: usitake nijaze nafasi za wengine maana nina mengi sana.
1. Mkataba wa Hali Bora toka 2008 hadi leo umesainiwa na kupata baraka za Hazina? Kama Bodi ilipitisha ikiwa na uwakilishi wa Hazina vipi tena ulipofika huko ukwame? Hazina wanakujua ulivyo mtaaluma wa kutoa pesa ili upete kwa ulaini. Ukijibu hoja hizi nitakuletea ushahidi wa maandishi.
2. Ulipokodi ndege kwenda Kagera kuwabeba waheshimiwa, ulikuwa na baraka za BODI? Je za Waziri wa Fedha? Mbona uliomba usamehewe! Leo unasema hufanyi kitu mpaka Bodi ikupe baraka.
HOJA YA SITA,-Kamati ya bunge inashauri,haiagizi,na ushauri au maagizo yake sharti yajadiliwe katika bodi ya ppf,mwandishi anatafuta huruma kuchomeka jina la mwenyekiti wa kamati ya bunge mh.Zitto Kabwe,bodi haikupuuza ushauri wa kamati ya bunge,na pia kamati haikupuuza mapendekezo au maamuzi ya bodi ya ppf,pamoja na mwandishi kujaribu kuumba maneno yenye lengo la kujenga chuki baina ya kamati ya mh.Zito na ppf,bado namuhakikishia kamati hii ya bunge inayoimani kubwa sana na utendaji wa menejiment ya ppf na bodi yake.
PENYE RED: Hata ya JAIRO ilikuwa hivi hivi, ngoja tusubiri warudi mjengoni. Kama hakupuuza kwa nini mlipe wakati mmeagizwa na chombo cha UMMA?
HOJA YA SABA;-napata shida na dhamira ya mwandishi,kwake hana jema wala zuri,hoja yake ya kwanza na ya pili kalilia ajira za kudumu na pensionable kwa watumishi wa mfuko ppf,hata pale ambapo mfuko wa ppf umefanya mabadiliko katika sheria zake za ajira kuwa za kudumu,bado mwandishi anaonekana kukerwa,kuwa kwenye mkataba tabu,kurudi kwenye ajira za kudumu tabu,ee Mungu tuepushe na roho hizi zisizopendezwa na wanadamu wenzao kwa kila jambo,labda tu hapa niseme jambo moja,maamuzi ya malipo yaliyofanyika kabla ya sheria ya ajira za kudumu kufanyika hayatafanyika tena,kwa sasa malipo ni kwa mujibu wa sheria mpya ambayo inawatambua wafanyakazi wa ppf kuwa wa kudumu na pensionable.
PENYE RED: Hapa bwana Erio umejitambulisha vema kuwa hayatafanyika tena. Maamuzi yalifanyika 2009 na Utumishi kutoa waraka, malipo yamefanyika 2011, hivi uko serious kweli kwa haya maelezo bwana DG? Unataka niweke vielelezo?
MWANDISHI HAISHI VISA-eti anauliza kama ni sahihi mfanyakazi kuchangiwa 87% kwa mshahara mkubwa!!!! mifano ipo wazi na ni mingi,wapo wafanyakazi migodini,na kwenye makampuni mengi hapa nchini,ambao wanachangiwa asilimia kubwa ya gawiwo la mishahara yao na waajiri,na wapo wakurugenzi katika makampuni mengi hapa nchini wanaolipwa mishahara mikubwa zaidi ya huo wa ppf,dunia leo ni kama kijiji,mwandishi afanye tafiti ya mishahara ya wakurugenzi wa mashirika ya umma hapa nchini ili ajiridhishe kama kiwango hicho ambacho pia hana uhakika nacho kwa dg wa ppf ni kiwango cha kumtisha mtu,nimkumbuhe tu kwamba,mshahara wa dg wa ppf na wafanyakazi,huamriwa na bodi ya ppf kwa kuzingatia sheria ya mfuko ambayo hutamka pia ni kiwango gani cha asilimia kitatumika kwa mishahara na malipo ya wafanyakazi,sii mshahara wa mtu kuamka asubuhi na kujipangia.
PENYE RED: Nimekubali PPF ni shamba la bibi, kuna mgodi umegunduliwa shambani humo humo? Ndugu zangu pesa zilichangwa na wanachama ambao wengi wao ni walalahoi leo unazifananisha na mgodi? Mungu akufungue ufahamu na utubu.
MWISHO KABISA-Mwandishi ametuelezea historia binafsi ya dg wa ppf,nimwombe sasa nje ya kuwa mpwa wa mkapa benjamin,atueleze sifa mbadala,je,huyo erio alipataje hiyo nafasi? alishindanishwa,au alipachikwa?? je,ana sifa za kuwa dg,kitaaluma na kiuwezo,au hana?kasoma wapi,au elimu yake inatiliwa shaka vipi?katokea wapi,nani aliwafanyisha usaili,alishindanishwa na nani ambaye mwandishi aliona labda alistahili kuliko erio??na kama ni mwandishi mwenyewe alipigwa mweleka kwenye usaili pia adekree intrest,maana asimwage tu sumu kumbe ni fungu la kukosa,maana wanadamu hawana dogo,na je,mwandishi alihitaji mpwa wa mkapa awe ombaomba hata kama anauwezo na sifa za kufanya kazi??je ni sahihi mtoto wa dada yangu asiajiliwe mahala eti kwa kuwa mie mjombaye ni rais wa nchi?? tusifikishane kwenye ulemavu huu wa fikra na mawazo tengefu,tumpe mtu kile astahilico na kumpongeza hata kama roho ya kukosa inakuuma,sii vema ukikosa jambo,au kama uliachishwa kazi mahala,ukakusanya uwongo wako na kuja hapa jukwaa la fikra huru kuja kumalizia stress zako,jamvi hili ni la fikra pevu,tujihadhari na wanaotaka kufanya liwe jamvi la kitchen pat;
PENYE RED:
Erio aliingia madarakani kwa hila ambazo zilifanikishwa na mjomba wake Mkapa.
1.Elimu: Masters ya sheria, sina tatizo,
2.Uzoefu: Desk officer TLS up to May 2000, june 2000 PPF Legal Officer na Katibu wa Bodi (hana assistant), 2003-2005 PPF Head of Legal Unit supervising one staff and a secretary, 2005 Sept, Director General PPF, supervising 200 staff and more than 100,000 members. Hapa ndio tatizo hana leadership skills na uzoefu
3. Katibu wa Hazina by the Mgonja, aliandaa dokezo kwenda kwa Waziri kuwa Mr. Nsemwa anapendekezwa kuendelea kuwa DG PPF kwa kipindi cha pili. Dokezo likiwa mezani kwa Waziri, Erio akajua maana alikuwa aifuatilia sana hiyo nafasi. Akamtumia mama mmoja pale Hazina mwenye cheo kikubwa, akachukua faili na kurudi nalo kwa Mgonja na kumshawishi kuwa nafasi itangazwe ili kumpata DG. Kama mjuavyo, hata Adam wa kale alishawishiwa na Hawa. Tangazo likatolewa.
4. Interview ilikuwa ifanywe na PWC, badala yake shabiki mkuu wa Erio, Marehemu Elvis Musiba akasimamia ili kuhakikisha aliyekuwa DG wa wakati huo hapiti maana angekuwa threat kwenye hila zao. PWC wanajua vema na hawakufurahishwa na hili ndio maana baada ya kupewa maelekezo kuwa lazima Nsemwa ashindwe kwenye mchujo walikataa kusimamia na kupewa Musiba.
5. Interview ya pili aliongoza mtu mmoja wa TRA (DF) akafuatiwa na DF wa PPF, erio alikwa wa TATU.
6. Mapendekezo ya Waziri wa Fedha Mramba (yalikuwa ya shinikizo la .....) yakampendekeza Erio ambaye ni wa tatu kuwa apewe na Mjomba mtu hakutia ajizi akampa.