Hivi Hatumuoni Huyu......! au yuko sawa?

Hivi Hatumuoni Huyu......! au yuko sawa?

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,198
Reaction score
7,536
  • Huyu mtu ana mpango wa kugombea urais 2015,


  • Huyu mtu huyu hutangazia nia yake maeneo ya ibada,


  • Huyu mtu huyu hutanguliza vibahasha katika maeneo hayo ya ibada kabla ya kutangaza nia (na vibahasha vyake vya ukweliii).


  • Huyu mtu huyu wengine humlaumu eti ni fisadi.

Sasa mimi wasi wasi wangu ni pale ninapoona hakuna mtu anayemkemea.Najiuliza je! ina maana huyu mtu yuko sahihi? Kama tunadhani yuko sahihi; ni kwa nini? Hatuoni kuwa kama akiendelea hivi, wenzake ambao nao wana nia ya kugombea urais 2015, wataanza kuingia na vibahasha kwenye maeneo ya ibada na hiyo sio tu kwamba itakuwa ni aina fulani ya rushwa bali pia itachochea migawanyiko ya kidini?

Kama hayuko sahihi; kwa nini vyombo mbali mbali vya kitaifa kama vile Chama chake, Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa, Rais, TISS, n.k wasimshauri? Je! inamaana watakuwa hawaoni, au wanamuogopa, au wana maslahi na kinachofanyika?

Kwa maoni yangu jambo hili linachukuliwa kama mzaha ila mwisho wa siku linaweza kuleta migawanyiko mibaya.Wenzake watakuwa wanasoma upepo, wakiona hili la kutoa na kusaidia kuchangisha fedha kwenye maeneo ya ibada linasaidia nao watawekeza huko huko.Mwisho wake watu wataanza kuhoji fulani kachangia msikiti au kanisa? kama kachangia kanisa kachangia bei gani na msikiti kachangia kiasi gani? kisha kwa nini kule kachangia zaidi ya kule ? kwa nini kwetu hajachangia? kwa nini kapendelea dini ile au hii? fulani na yeye na aje kwenye dini hii au ile n.k. Hii ni hatari aisee.

Nashauri katika kuchangia msitaje majina ya watu.Changieni tu hoja kwa ujumla wake kwa sababu mkitaja taja majina ya watu, upo uwezekano wa uzi huu kupoteza muelekeo na kisha kufungiwa
 
ni hatari kwa afya ya nchi hii ila sijui kwa nini hata chama chake hakichukui hatua ya kuepusha madhara tunayo yaona sisi great thinkers wa jf.
 
Na akishapata urais atakachofanya ni kuwafunga midomo viongozi wa dini ambako ndiko alikoingilia akiwa MCHAFU na akaibuka akiwa MSAFI.
 
Nashangaa mwenyekiti wake jana anakemea viongozi wa dini badala ya kumkemea huyu jamaa yake
kuendekeza siasa za kijinga kwa mgongo wa kuchangia makanisa na misiskiti,na la kujiuliza watanzania
huyu mtu hii pesa kaipata wapi na lengo lake ni nini ktk hili,je kama alijilimbikizia pesa nyingi kiasi hiki akiwa
waziri akipata huo urais tutegemee nini'!!!!

cc.Pasco
 
Ukiijua siku atakayogawa vibahasha tustue na sisi tukajizolee. Kura na siri yetu.
 
Watu wa chama chake na wao wanalalamika pembeni bila ya kumfesi mhusika tena hawathubutu hata kumtaja jina kama mwanzisha mada alivyoogopa kumtaja jina.
Kuna kitu si cha kawaida kwa Lowasa, kwa nini anaogopwa na kila mtu hapa nchini?
Hadi mwenyekiti wa chama chake anamwogopa.
 
Watu wa chama chake na wao wanalalamika pembeni bila ya kumfesi mhusika tena hawathubutu hata kumtaja jina kama mwanzisha mada alivyoogopa kumtaja jina.
Kuna kitu si cha kawaida kwa Lowasa, kwa nini anaogopwa na kila mtu hapa nchini?
Hadi mwenyekiti wa chama chake anamwogopa.
Tehe! tehe! tehe! sasa mkuu Ndibalema ; kama Mwenyekiti mwenyewe anaogopa, sembuse mimi Betlehem? Wewe unanitakia mema kweli?
 
Last edited by a moderator:
Watu wa chama chake na wao wanalalamika pembeni bila ya kumfesi mhusika tena hawathubutu hata kumtaja jina kama mwanzisha mada alivyoogopa kumtaja jina.
Kuna kitu si cha kawaida kwa Lowasa, kwa nini anaogopwa na kila mtu hapa nchini?
Hadi mwenyekiti wa chama chake anamwogopa.
Tutamuonesha hatumuogopi kwenye sanduku la kura.
 
hivi mnakumbuka ule ujasiri uliosemwa na kamati ya bunge uliitwa ujasiri wa nini vile!??
 
Ooops! yani unataka kuniambia kuna uwezekano chama chake kikamuamini na kumsimamisha yeye katika nafasi ya urais?
Yeye kwenye chama chake kashika mpini. Na ikumbukwe kua kwenye chama lao mwenye kisu kikali ndie anae kula steki.
 
Tutamuonesha hatumuogopi kwenye sanduku la kura.

Nimekuja kugundua kupiga kura ni jambo linalohitaji kujitoa kwa moyo wote, kama kila mtu angekuwa napiga kura hasa wale wanaokuwa msatari wa mbele kuwapigia debe wanasiasa mbona tungekuwa mbali.

Nimefuatilia kwa karibu sana story ya Kethi Kilonzo binti wa aliyekuwa waziri wa elimu Kenya marehemu Mutula Kilonzo, huyu dada ni mwanasheria machachari sana na alionyesha umahiri wake katika masuala ya sheria wakati wa kesi ya kupinga uchaguzi wa uraisi nchini Kenya nilimuona mtu wa maana sana lakini nimekuja kugundua hata kura yenyewe hakupiga. Nimejiuliza maswali mengi sana hivi unawezaje kuongelea na kutetea jambo with such passion wakati you are not part of it. Habari imekuwa mbaya upande wake imeonekana hayupo kwenye register ya wa piga kura na kama itagundulika amejipatia stakabadhi ya mpiga kura kwa njia za mkato hata proffession yake itakwisha.

To cut the long story short, kama msomi kama huyu haoni sababu ya kupiga kura je mwananchi wa kawaida si itakuwaje???
Kethi Kilonzo - Wikipedia, the free encyclopedia
 
Huyu mtu anamtumia Mwigulu kukivuruga Chama Cha Mapinduzi kwa kufanya mambo yanayoshusha heshima ya chama!
 
nina uhakika watu timamu ndani ya ccm watakimbia chama chao kama huyu mtu atapewa ridhaa.
 
Ooops! yani unataka kuniambia kuna uwezekano chama chake kikamuamini na kumsimamisha yeye katika nafasi ya urais?
Kama ameweza kuwaghiribu maaskofu na masheikh, ni nani CCM mwenye usafi wa kumzuia Lowasa? kama ni swala la pesa ndio usiseme kabisa.

Ni wazi kabisa tujiandae na mpambano wa kufa mtu Dr Slaa vs Lowasa.
 
Kama serikali pia imeshindwa kumsema wakati akitafuta hiyo nafasi, je akiisha ipata si atawapandia migongoni.
Tanzania imekuwa rikizo ya kiuongozi kwa miaka kumi, ndiyo maana mpaka viraza kama mwigulu nchemba nao waka pata pakusemea
 
nina uhakika watu timamu ndani ya ccm watakimbia chama chao kama huyu mtu atapewa ridhaa.
Ukituliza akili yako na ukafikiri vizuri na kwa maono ya kiungu, na siyo uchambuzi wa kihuni kama wa Mwanakijiji utagunduwa kitu kimoja cha ajabu sana.

Lowasa ni karata muhimu sana kwa Chadema ambayo inasubili muda muhafaka mjuwe Lowasa atatumiwa vipi na Mungu kuiondoa CCM madarakani.

Wakimteuwa kugombea wanang'oka na wasipomteuwa ndio watang'oka kwa aibu kubwa, Lowasa hatokuwa na Cha kupoteza wasipomteuwa kamwe hawezi kubaki CCM huu ndio ukweli.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom