Nakumbuka mwaka jana tuliitwa kwenye semina Morogoro kujadili mchakato wa kuhamisha vyuo vya Ualimu kusimamiwa na NACTE badala ya NECTA. Dr. Primus Nkwera Katibu Mtendaji wa NACTE alisimama kidete na kuwataka wakuu wa vyuo kuanza mchakato kabla ya mwezi Disemba mwaka jana. Nashangaa mwaka mwingine karibu unakwisha Dr. Nkwera sijamsikia tena akiongelea jambo hilo. Au ndiyo kusema mpango umekwama. Basi watoe tamko ili wadau waelewe kinachoendelea. Naomba kuwasilisha.