Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,483
- 40,008
Jmushi1..Slaa alirudi CCM lini?Wanajamvi,
Balozi Dr Slaa, ambaye yumo humu lakini sijamsikia zaidi ya kuona akitoa likes kwa wana ccm wenzake, alisema kuwa kitendo cha Lowassa kuhamia chadema ni sawa na “choo kuhamishiwa sebuleni”
Lakini Sasa Lowassa amerudi ccm, Slaa yumo humo, hivyo yuko chooni na hapo hapo sebuleni. Hii ni kwa mujibu wake yeye mwenyewe.
Kuna wanaodhani kuwa sasa atarudi chadema. Na hii imefikia hadi kwa mwana jamvi maarufu na madai mkubwa wa chadema humu, Salary Slip kuanzisha mada inayosema kuwa “ije mvua lije jua, Slaa asiruhusiwe kurudi chadema”. Lakini pia kuna wanajamvi wanaodhani kuwa si rahisi kwa Slaa kuachia “Keki” kwasababu ya ubalozi aliopewa na Maghufuli mara baada ya kum sapoti kwenye mbio za urais na kukupigia chama alichoshiriki kwa kiasi kikubwa sana kukijenga!
Ni wazi kuwa kurudi kwa Lowassa ccm kuna consequences zake. Mojawapo ni issue ya Slaa. Sana sana ni kwasababu ya legacy yake. Kama ni kweli hakuwa na tamaa ya urais, na alihama chama kwasababu tu ya Lowassa kuhamia, basi shurti atoke ccm. Great thinker anyeitwa barafu , alisema “asiyempenda kaja”. Hivyo kuonyesha msimamo hapa ni muhimu.
Lakini kama alihama kwasababu alipoteza ile nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya chadema, basi ni wazi itabidi awaombe msamaha wanajamvi wenzetu humu ambao na walijitoa kindakindaki kumsapoti na hata kuwa na mawazo hasi kabisa kwa baadhi yao. Mfano Mzee Mwanakijiji pamoja na MTAZAMO . Lakini mkuu idawa yeye kidogo alikuwa bado ana “balance”! Pamoja na great thinker mwingine Nguruvi3 . Lakini msimamo wa JokaKuu haukubadilika. Ningependa kusikia maoni yao kuhusu hilo. Pamoja na ushauri wowote kwa Dr Slaa kama wanao!
Nisiseme mengi kwa sasa.