jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 24,990
- 22,523
Wanajamvi,
Balozi Dr Slaa, ambaye yumo humu lakini sijamsikia zaidi ya kuona akitoa likes kwa wana ccm wenzake, alisema kuwa kitendo cha Lowassa kuhamia chadema ni sawa na “choo kuhamishiwa sebuleni”, na hivyo akaondoka chadema na kujiuzulu siasa!
Lakini Sasa Lowassa amerudi ccm, Slaa yumo humo,(anaitumikia serikali ya ccm) hivyo yuko chooni na hapo hapo sebuleni.
Hii ni kwa mujibu wake yeye mwenyewe. Kwamba alipo Lowassa ni sawa na choo kikiwa sebuleni. Ni kwasababu aliamini ni fisadi kama sikosei.
Kuna wanaodhani kuwa sasa atarudi chadema. Na hii imefikia hadi kwa mwana jamvi maarufu na mdau mkubwa wa chadema humu, Salary Slip kuanzisha mada inayosema kuwa “ije mvua lije jua, Slaa asiruhusiwe kurudi chadema”. Lakini pia kuna wanajamvi wanaodhani kuwa si rahisi kwa Slaa kuachia “Keki” kwasababu ya ubalozi aliopewa na Maghufuli mara baada ya kum sapoti kwenye mbio za urais na kukipinga chama alichoshiriki kwa kiasi kikubwa sana kukijenga!
Ni wazi kuwa kurudi kwa Lowassa ccm kuna consequences zake. Mojawapo ni issue ya Dr Slaa. Sana sana ni kwasababu ya legacy yake, pamoja na jasho lake kwenye chama, na jitihada zake dhidi ya mioango ovu, na mbinu chafu za ccm. Kama ni kweli hakuwa na tamaa ya urais, na alihama chama kwasababu tu ya Lowassa kuhamia, basi shurti atoke ccm. Great thinker anayeitwa barafu , alisema kauli inayofanana na hii kuelekea kwa Dr Slaa akasema “Sasa Dr Slaa huko alipo, asiyempenda kaja”. Alimaanisha kuwa sasa wako timu moja! Na kwasababu alimkimbia kule chadema na sasa kaja ccm! Hivyo kuonyesha msimamo hapa ni muhimu sana kwa Dr Slaa na legacy yake hapa nchini!
Lakini kama alihama kwasababu alipoteza ile nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya chadema, basi ni wazi itabidi awaombe msamaha wanachadema, wanajamvi wenzetu humu ambao nao walijitoa kindakindaki kumsapoti na hata kuwa na mawazo hasi kabisa kwa baadhi yao dhidi ya chadema! Mfano Mzee Mwanakijiji ambaye kwasasa anao sapoti ccm moja kwa moja na upinzani anauogopa kama Ukoka! pamoja na MTAZAMO .
Lakini mkuu idawa yeye kidogo alikuwa bado ana “balance”! Pamoja na great thinker mwingine Nguruvi3 . Lakini msimamo wa JokaKuu pamoja na Mag3 ,hawakubadilika.
Ningependa kusikia maoni yao kuhusu hilo. Pamoja na ushauri wowote kwa Dr Slaa kama wanao!
Nisiseme mengi kwa sasa.
Balozi Dr Slaa, ambaye yumo humu lakini sijamsikia zaidi ya kuona akitoa likes kwa wana ccm wenzake, alisema kuwa kitendo cha Lowassa kuhamia chadema ni sawa na “choo kuhamishiwa sebuleni”, na hivyo akaondoka chadema na kujiuzulu siasa!
Lakini Sasa Lowassa amerudi ccm, Slaa yumo humo,(anaitumikia serikali ya ccm) hivyo yuko chooni na hapo hapo sebuleni.
Hii ni kwa mujibu wake yeye mwenyewe. Kwamba alipo Lowassa ni sawa na choo kikiwa sebuleni. Ni kwasababu aliamini ni fisadi kama sikosei.
Kuna wanaodhani kuwa sasa atarudi chadema. Na hii imefikia hadi kwa mwana jamvi maarufu na mdau mkubwa wa chadema humu, Salary Slip kuanzisha mada inayosema kuwa “ije mvua lije jua, Slaa asiruhusiwe kurudi chadema”. Lakini pia kuna wanajamvi wanaodhani kuwa si rahisi kwa Slaa kuachia “Keki” kwasababu ya ubalozi aliopewa na Maghufuli mara baada ya kum sapoti kwenye mbio za urais na kukipinga chama alichoshiriki kwa kiasi kikubwa sana kukijenga!
Ni wazi kuwa kurudi kwa Lowassa ccm kuna consequences zake. Mojawapo ni issue ya Dr Slaa. Sana sana ni kwasababu ya legacy yake, pamoja na jasho lake kwenye chama, na jitihada zake dhidi ya mioango ovu, na mbinu chafu za ccm. Kama ni kweli hakuwa na tamaa ya urais, na alihama chama kwasababu tu ya Lowassa kuhamia, basi shurti atoke ccm. Great thinker anayeitwa barafu , alisema kauli inayofanana na hii kuelekea kwa Dr Slaa akasema “Sasa Dr Slaa huko alipo, asiyempenda kaja”. Alimaanisha kuwa sasa wako timu moja! Na kwasababu alimkimbia kule chadema na sasa kaja ccm! Hivyo kuonyesha msimamo hapa ni muhimu sana kwa Dr Slaa na legacy yake hapa nchini!
Lakini kama alihama kwasababu alipoteza ile nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya chadema, basi ni wazi itabidi awaombe msamaha wanachadema, wanajamvi wenzetu humu ambao nao walijitoa kindakindaki kumsapoti na hata kuwa na mawazo hasi kabisa kwa baadhi yao dhidi ya chadema! Mfano Mzee Mwanakijiji ambaye kwasasa anao sapoti ccm moja kwa moja na upinzani anauogopa kama Ukoka! pamoja na MTAZAMO .
Lakini mkuu idawa yeye kidogo alikuwa bado ana “balance”! Pamoja na great thinker mwingine Nguruvi3 . Lakini msimamo wa JokaKuu pamoja na Mag3 ,hawakubadilika.
Ningependa kusikia maoni yao kuhusu hilo. Pamoja na ushauri wowote kwa Dr Slaa kama wanao!
Nisiseme mengi kwa sasa.