OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,195
- 103,721
Bado tunawapa nafasi ya kutubu na kubadili mawazo kabla hatujaanza kuja na TAKWIMU ambazo hamtozipenda nina uhakika😀
Tunashuhudia sio tu Mchezaji bali Mchezaji bora kuwahi kutokea tangu Milenia ya 2000 kwenye ardhi hii, sio kwamba ni mimi na wewe tu bali kila Mtu anajua hilo ila ni ngumu kukubali.
Huyu ni moja kati ya Viungo wachache sana kwenye soka la nchi hii kuwahi kubeba Tuzo ya Kiungo bora na tuzo ya Mchezaji bora, huyu unayemuona hapo kwenye clip.
Wachezaji wote ambao Malegend mnawataja sisi hatukatai ila tukiwauliza yapi makubwa yalifanyika tunaambiwa mwingine alikuwa anapiga chenga kuanzia chini mpaka goli, sawa tumekubali.
Tukiwauliza yapi makubwa mnatuambia walikuwa hawatoi pass bila kupiga kidali au tobo, sisi tunakubali hayo kwakuwa ni suala la mchezo wa mpira wa miguu ni burudani.
Lakini Clatous Chama amekuja kwenye zama hizi za mpira wa hesabu, zama za mpira sayansi na maelekezo ila Clatous Chama yeye ndie anatoa maelekezo kwenye mchezo huu.
Clatous Chama kwa miguu yake kaipeleka Simba kwenye michuano ya klabu bingwa barani Afrika, wameingia robo fainali mara mbili kwa miguu yake na jumla wameingia makundi mara tatu.
Takwimu kama hizi tunazisaka kwa tochi kwa wachezaji wengi ambao tunasema ni bora, namba zinambeba Chama na kipaji chake pia kinambeba sana, pasi na shaka.
Mchezaji ambaye anafunga mabao ya kideo, anakupa mpira wa kideo na bado anakupa takwimu nzuri ambazo hupati tabu kuzitetea😀
Mchezaji bora ni yupi? Wa kanzu na tobo? Mchezaji wa kufanya vyote na bado timu ikapata matokeo?
Clatous Chama ametokea kwenye kizazi bora cha Simba, nitajieni kama kuna Simba bora zaidi ya 2016-2020 kama ipo mnitajie! Kama kuna Simba iliyokuwa na takwimu bora kuliko hii nitajieni! Chama ndie kiini cha Simba hii.
Mchezaji bora zaidi kuwahi kutokea, Clatous Chama NO DOUBT.
Credit: Farhan