Historia ya Zanzibar Kama Inavyoelezwa na Joseph Mihangwa

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,266
Gazeti la Jamhuri la Jumanne 21 - 27 November, 2023 lina makala: ''Zanzibar Ndani ya Muungano Haishikiki - (14).

Baada ya kusoma niliingia Maktaba na nikakuta hayo yafuatayo niliyoandika miaka mingi nyuma (2016):

''Katika mambo yaliyosaidia sana kuiweka vyema historia ya Zanzibar ni vitabu vilivyoandikwa na Wazanzibari wenyewe ambao walipigania u huru wa Zanzibar.

Historia iliyokuwa ikipewa nafasi ni historia ya mapinduzi peke yake ilhali Wazanzibari walipigania uhuru wao kutoka kwa Muingereza wakaupata na baada ya hapo kiasi cha mwezi mmoja tu yakatokea mapinduzi yaliyosababisha umwagaji mkubwa wa damu na madhila mengi.

Baada ya Ali Muhsin Barwani kuandika kumbukumbu zake: ''Conflicts and Harmony in Zanzibar,'' ambayo kwa hakika ni historia ya kudai uhuru wa Zanzibar na historia ya vyama vilivyopigania uhuru wa Zanzibar - Zanzibar Nationalist Party (ZNP) au Hizbu, Afro Shirazi Party (ASP) ya Abeid Aman Karume na Zanzibar and Pemba Peoples Party (ZPPP) ya Mohamed Shamte picha mpya ikajitokeza. Lakini ilikuwa kalamu ya Aman Thani katika kitabu chake: ''Ukweli ni Huu,''
ndiyo iliyokuja na historia ya kutisha.

Hata hivyo kitabu cha Dr. Harith Ghassany: ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' utafiti huu ulishinda tafiti zote za kigeni na ndicho kilichokuja kuweka historia ya Zanzibar katika mawanda ya dunia.

Yale yaliyokuwa yamefichwa sasa yakawa yapo uwanjani peupe yanasomwa, na wengi wa wasomaji hao ni vijana waliozaliwa baada ya mapinduzi.

Matokeo ya mwamko huu mpya ndiyo haya tunayoshuhudia hivi sasa.

Bahati mbaya badala ya kusikitishwa na yaliyotokea na kujaribu kuleta umoja pamezuka watu wanakejeli waliouawa kwa dulma katika mapinduzi yale.

Waliouawa wameacha watoto na wajukuu wapo kwa sasa, wamesimama kupinga kila aliyekuwa anaonyesha kufurahishwa na historia ile iliyowapotezea wapendwa wao.''

Sasa tupitie pamoja hayo niliyosoma kutoka kalamu ya Mihangwa:

1700593060942.jpeg

Kitabu cha Sheikh Ali Muhsin Barwani kwa Kiingereza na Kiswahili (1997)
1700593167396.jpeg

Kitabu cha Aman Thani
Dr. Ghassany ndiye mwandishi wa kwanza kuieleza dunia kuwa katika ardhi ya Tanganyika, kijiji cha Kipumbwi kulikuwa na kambi iliyoweka mamluki kwa ajili ya kuvushwa kwenda Zanzibar kusaidia kuiangusha serikali ya Sheikh Mohamed Shamte.

Dr. Ghassany kaja Tanga na mimi ndiye mwenyeji wake nikampeleka nyumbani kwa Mohamed Omari Mkwawa akazungumzenae kuhusu hii kambi ya Kipumbwi.

Nilimfikisha nami nikaondoka nikawaacha wawe na faragha wazungumze yale yaliyotokea katika mapinduzi ya Zanzibar.

Niliporudi kumchukua Dr. Ghassany nilimkuta amekalia mgongo wake.
Kitu gani kilimnyong'onyeza?

Endela kusoma:

''Hivi ndiyo nilivyomkuta Dr. Ghassany alivyokuwa amekaa nyumbani kwa Mohamed Omari Mkwawa Kisosora Tanga akisikiliza yale yaliyotendeka Zanzibar baada ya Wamakonde kuingia kushiriki katika mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

Hakuwa na nguvu ya kukaa sawasawa.
Alikuwa amechoka sana.

Watengeneza filamu wa Hollywood ni mafundi wa kutengeneza kitu kinaitwa, "set."

Ingekuwa wanapiga movie ile hali ya nyumba ya Mzee Mkwawa au Tindo kama Mzee Karume alivyopenda kumwita ilijitosheleza.

Mzee Mkwawa alikuwa kapanga banda la uani vyumba viwili Kisosora na mkewe alikuwa anafanya biashara ya "Mama Ntilie," nyakati za usiku.

Juu ya hali zao za shida walikuwa nadhifu.

Mpiga picha wa Hollywood angeonyesha chumba kidogo nadhifu lakini hakina mwanga wa kutosha.

Camera ingemchuka Harith Ghassany akiwa kainama anamsikiliza Mzee Mkwawa.

Katika scene hii Harith kakaa vizuri kitini.
Sasa camera inatoka kwake inakwenda kwa Mzee Mkwawa.

Mzee Mkwawa yuko kizani ila kwa sura yake iliyopigwa na mashakili ya maisha iko katika mwanga na anaanza kuzungumza.

Maneno yake yanasindikizwa na "flashbacks," za mapigano na mauaji Zanzibar wakionyeshwa watu "ragtag," wameshika mapanga mengine yakivuja damu."

Muogozaji filamu anakata anairudisha camera kwa Dr. Harith Ghassany.

Scene hii ndiyo inamuonyesha Dr. Ghassany aliyeelemewa na yale anayosikia sasa hajiwezi tena anakalia mgongo wake.

Taratibu camera man anaingiza giza kwenye kile chumba na anawaonyesha wote wawili Mzee Mkwawa na Dr. Ghassany kama vivuli lakini sauti ya Tindo bado inasikika.

Lakini hapa Tindo yuko katika, "soliloquy," anaisemesha nafsi yake kwa sauti ya masikitiko.

Mzee Mkwawa aliniambia, ''Hivi kweli baada ya kazi yote ile niliyofanya ijaza yangu ni hii mimi leo kuishia kuishi kwenye banda la kuku?''

Mzee Mkwawa ndiye aliyekuwa akiwavusha hawa Wamkonde usiku kwa siri kuwapeleka Zanzibar.

1700593869851.jpeg

Mohamed Omar Mkwawa​

Joseph Mihangwa anaandika anasema: "EAMWS kiongozi wake alikuwa Mnajimu mashuhuri Afrika Mashariki, Sheikh Yahaya Hussein.

Ilifutwa mwaka wa 1968 kwa sababu ya kujijusisha na nambo ya siasa kwa ukinzani na serikali za Afrika Mashariki.

Ukweli ni kuwa Tewa Said Tewa ndiye alikuwa President wa EAMWS kwa upande wa Tanzania.

Sababu za serikali kuivunja EAMWS ilikuwa inajenga Chuo Kikuu Cha Waislam.

Hili halikutakiwa.
Serikali ikavunja EAMWS na kuunda BAKWATA.

1700594201918.jpeg

Tewa Said Tewa Rais wa EAMWS

JOSEPH MIHANGWA ANASEMA JULIUS NYERERE HAKUWA NA TAARIFA ZA MAPINDUZI YA ZANZIBAR​

Kulikuwa na kambi Kipumbwi ambayo waliwekwa Wamakonde wakata mkonge na hawa Wamakonde walivushwa kuingia Zanzibar kupigia kura ASP Uchaguzi wa 1961 na walishiriki katika kupindua serikali mwaka wa 1964.

Hawa Wamakonde waliua Waarabu wengi waliokuwa wakiishi mashamba.

Dr. Harith Ghassany kaeleza kwa urefu historia hii katika kitabu chake, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru," (2010).

1700594449912.jpeg


JOSEPH MIHANGWA ANAVYOMWELEZA ABOUD JUMBE​

1700594530941.jpeg


Huu ndiyo ufahamu wa Joseph Mihangwa kuhusu historia ya mapinduzi ya Zanzibar na yalifuatia baadae.



 
Gazeti la Jamhuri la Jumanne 21 - 27 November, 2023 lina makala: ''Zanzibar Ndani ya Muungano Haishikiki - (14).

Baada ya kusoma niliingia Maktaba na nikakuta hayo yafuatayo niliyoandika miaka mingi nyuma (2016):

''Katika mambo yaliyosaidia sana kuiweka vyema historia ya Zanzibar ni vitabu vilivyoandikwa na Wazanzibari wenyewe ambao walipigania u huru wa Zanzibar.

Historia iliyokuwa ikipewa nafasi ni historia ya mapinduzi peke yake ilhali Wazanzibari walipigania uhuru wao kutoka kwa Muingereza wakaupata na baada ya hapo kiasi cha mwezi mmoja tu yakatokea mapinduzi yaliyosababisha umwagaji mkubwa wa damu na madhila mengi.

Baada ya Ali Muhsin Barwani kuandika kumbukumbu zake: ''Conflicts and Harmony in Zanzibar,'' ambayo kwa hakika ni historia ya kudai uhuru wa Zanzibar na historia ya vyama vilivyopigania uhuru wa Zanzibar - Zanzibar Nationalist Party (ZNP) au Hizbu, Afro Shirazi Party (ASP) ya Abeid Aman Karume na Zanzibar and Pemba Peoples Party (ZPPP) ya Mohamed Shamte picha mpya ikajitokeza. Lakini ilikuwa kalamu ya Aman Thani katika kitabu chake: ''Ukweli ni Huu,''
ndiyo iliyokuja na historia ya kutisha.

Hata hivyo kitabu cha Dr. Harith Ghassany: ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,'' utafiti huu ulishinda tafiti zote za kigeni na ndicho kilichokuja kuweka historia ya Zanzibar katika mawanda ya dunia.

Yale yaliyokuwa yamefichwa sasa yakawa yapo uwanjani peupe yanasomwa, na wengi wa wasomaji hao ni vijana waliozaliwa baada ya mapinduzi.

Matokeo ya mwamko huu mpya ndiyo haya tunayoshuhudia hivi sasa.

Bahati mbaya badala ya kusikitishwa na yaliyotokea na kujaribu kuleta umoja pamezuka watu wanakejeli waliouawa kwa dulma katika mapinduzi yale.

Waliouawa wameacha watoto na wajukuu wapo kwa sasa, wamesimama kupinga kila aliyekuwa anaonyesha kufurahishwa na historia ile iliyowapotezea wapendwa wao.''

Sasa tupitie pamoja hayo niliyosoma kutoka kalamu ya Mihangwa:

View attachment 2821157
Kitabu cha Sheikh Ali Muhsin Barwani kwa Kiingereza na Kiswahili (1997)
View attachment 2821159
Kitabu cha Aman Thani
Dr. Ghassany ndiye mwandishi wa kwanza kuieleza dunia kuwa katika ardhi ya Tanganyika, kijiji cha Kipumbwi kulikuwa na kambi iliyoweka mamluki kwa ajili ya kuvushwa kwenda Zanzibar kusaidia kuiangusha serikali ya Sheikh Mohamed Shamte.

Dr. Ghassany kaja Tanga na mimi ndiye mwenyeji wake nikampeleka nyumbani kwa Mohamed Omari Mkwawa akazungumzenae kuhusu hii kambi ya Kipumbwi.

Nilimfikisha nami nikaondoka nikawaacha wawe na faragha wazungumze yale yaliyotokea katika mapinduzi ya Zanzibar.

Niliporudi kumchukua Dr. Ghassany nilimkuta amekalia mgongo wake.
Kitu gani kilimnyong'onyeza?

Endela kusoma:

''Hivi ndiyo nilivyomkuta Dr. Ghassany alivyokuwa amekaa nyumbani kwa Mohamed Omari Mkwawa Kisosora Tanga akisikiliza yale yaliyotendeka Zanzibar baada ya Wamakonde kuingia kushiriki katika mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

Hakuwa na nguvu ya kukaa sawasawa.
Alikuwa amechoka sana.

Watengeneza filamu wa Hollywood ni mafundi wa kutengeneza kitu kinaitwa, "set."

Ingekuwa wanapiga movie ile hali ya nyumba ya Mzee Mkwawa au Tindo kama Mzee Karume alivyopenda kumwita ilijitosheleza.

Mzee Mkwawa alikuwa kapanga banda la uani vyumba viwili Kisosora na mkewe alikuwa anafanya biashara ya "Mama Ntilie," nyakati za usiku.

Juu ya hali zao za shida walikuwa nadhifu.

Mpiga picha wa Hollywood angeonyesha chumba kidogo nadhifu lakini hakina mwanga wa kutosha.

Camera ingemchuka Harith Ghassany akiwa kainama anamsikiliza Mzee Mkwawa.

Katika scene hii Harith kakaa vizuri kitini.
Sasa camera inatoka kwake inakwenda kwa Mzee Mkwawa.

Mzee Mkwawa yuko kizani ila kwa sura yake iliyopigwa na mashakili ya maisha iko katika mwanga na anaanza kuzungumza.

Maneno yake yanasindikizwa na "flashbacks," za mapigano na mauaji Zanzibar wakionyeshwa watu "ragtag," wameshika mapanga mengine yakivuja damu."

Muogozaji filamu anakata anairudisha camera kwa Dr. Harith Ghassany.

Scene hii ndiyo inamuonyesha Dr. Ghassany aliyeelemewa na yale anayosikia sasa hajiwezi tena anakalia mgongo wake.

Taratibu camera man anaingiza giza kwenye kile chumba na anawaonyesha wote wawili Mzee Mkwawa na Dr. Ghassany kama vivuli lakini sauti ya Tindo bado inasikika.

Lakini hapa Tindo yuko katika, "soliloquy," anaisemesha nafsi yake kwa sauti ya masikitiko.

Mzee Mkwawa aliniambia, ''Hivi kweli baada ya kazi yote ile niliyofanya ijaza yangu ni hii mimi leo kuishia kuishi kwenye banda la kuku?''

Mzee Mkwawa ndiye aliyekuwa akiwavusha hawa Wamkonde usiku kwa siri kuwapeleka Zanzibar.

View attachment 2821161
Mohamed Omar Mkwawa​

Joseph Mihangwa anaandika anasema: "EAMWS kiongozi wake alikuwa Mnajimu mashuhuri Afrika Mashariki, Sheikh Yahaya Hussein.

Ilifutwa mwaka wa 1968 kwa sababu ya kujijusisha na nambo ya siasa kwa ukinzani na serikali za Afrika Mashariki.

Ukweli ni kuwa Tewa Said Tewa ndiye alikuwa President wa EAMWS kwa upande wa Tanzania.

Sababu za serikali kuivunja EAMWS ilikuwa inajenga Chuo Kikuu Cha Waislam.

Hili halikutakiwa.
Serikali ikavunja EAMWS na kuunda BAKWATA.

View attachment 2821164
Tewa Said Tewa Rais wa EAMWS

JOSEPH MIHANGWA ANASEMA JULIUS NYERERE HAKUWA NA TAARIFA ZA MAPINDUZI YA ZANZIBAR​

Kulikuwa na kambi Kipumbwi ambayo waliwekwa Wamakonde wakata mkonge na hawa Wamakonde walivushwa kuingia Zanzibar kupigia kura ASP Uchaguzi wa 1961 na walishiriki katika kupindua serikali mwaka wa 1964.

Hawa Wamakonde waliua Waarabu wengi waliokuwa wakiishi mashamba.

Dr. Harith Ghassany kaeleza kwa urefu historia hii katika kitabu chake, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru," (2010).

View attachment 2821165

JOSEPH MIHANGWA ANAVYOMWELEZA ABOUD JUMBE​

View attachment 2821166

Huu ndiyo ufahamu wa Joseph Mihangwa kuhusu historia ya mapinduzi ya Zanzibar na yalifuatia baadae.




Joseph Mihangwa kaeleza ukweli wa mambo,ila kwakuwa kafunua mipango ovu iliyotaka kuwekwa zanzibar na east afrika kuimplemet islamic fundamentalism lazima uje kujivesha nguo.
 
Joseph Mihangwa kaeleza ukweli wa mambo,ila kwakuwa kafunua mipango ovu iliyotaka kuwekwa zanzibar na east afrika kuimplemet islamic fundamentalism lazima uje kujivesha nguo.

Chuki zako za juu kwa waislamu na uislamu haziishi .

Islamic fundamentalism ndio dini gani tena ??

Hamwachi chuki ?????? Kazi ipo
 
Joseph Mihangwa kaeleza ukweli wa mambo,ila kwakuwa kafunua mipango ovu iliyotaka kuwekwa zanzibar na east afrika kuimplemet islamic fundamentalism lazima uje kujivesha nguo.
Kwani vibaya mtu kufata fundamentals (misingi) ya dini yake?

Wewe wewe hufati misingi "fundamentals" za dini yako kwanini utake wote wawe kama wewe?
 
Joseph Mihangwa kaeleza ukweli wa mambo,ila kwakuwa kafunua mipango ovu iliyotaka kuwekwa zanzibar na east afrika kuimplemet islamic fundamentalism lazima uje kujivesha nguo.
Kwani vibaya mtu kufata fundamentals (misingi) ya dini yake?

Wewe wewe hufati misingi "fundamentals" za dini yako kwanini utake wote wawe kama wewe?
 
Joseph Mihangwa kaeleza ukweli wa mambo,ila kwakuwa kafunua mipango ovu iliyotaka kuwekwa zanzibar na east afrika kuimplemet islamic fundamentalism lazima uje kujivesha nguo.
Kwani vibaya mtu kufata fundamentals (misingi) ya dini yake?

Wewe wewe hufati misingi "fundamentals" za dini yako kwanini ulazimishe wote tuwe kama wewe?
 
Joseph Mihangwa kaeleza ukweli wa mambo,ila kwakuwa kafunua mipango ovu iliyotaka kuwekwa zanzibar na east afrika kuimplemet islamic fundamentalism lazima uje kujivesha nguo.
Kwani vibaya mtu kufata fundamentals (misingi) ya dini yake?

Wewe wewe hufati misingi "fundamentals" za dini yako kwanini ulazimishe wote tuwe kama wewe?
 
Kwani vibaya mtu kufata fundamentals (misingi) ya dini yake?

Wewe wewe hufati misingi "fundamentals" za dini yako kwanini ulazimishe wote tuwe kama wewe?
Wengine dini zao zinaruhusu ushoga ndio maana akatoa kauli zile
 
Gazeti la Jamhuri la Jumanne 21 - 27 November, 2023 lina makala: ''Zanzibar Ndani ya Muungano Haishikiki - (14).

Huu ndiyo ufahamu wa Joseph Mihangwa kuhusu historia ya mapinduzi ya Zanzibar na yalifuatia baadae.
Napendekeza kufanyike a compilation ya stories zote kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, halafu tukaja na version moja iliyokuwa straight.

Wana bodi, japo tuko kwenye harakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, kuna swali linanitatiza kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, ambapo majibu yake sahihi, pia yanaweza kuwa ni kiashiria tosha cha mshindi wa urais wa Zanzibar, iwapo uchaguzi utakuwa huru na wa haki.

Swali hili lahusu ukweli haswa kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, 1964, baada ya kuibuka kwa kitabu kingine kiitwacho "Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru"
View attachment 2077603
kilichoandikwa na Mwanazouni wa Zanzibar, Dr. Harith Ghassany, kama kilivyofanyiwa mapitio na mwandishi Mohamed Said kwenye gazeti la Al-Nuur la leo.

Ghasanny anasema kumbe Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalitekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde (Wakata Mkonge) ambao waliongozwa na Mzee Mohamed Omar Mkwawa (Tindo) chini ya Amiri Jeshi wa jeshi la mamluki hao Victor Mkello (RIP). (kumbe amiri jeshi hakuwa Mganda John Okello pekee, bali pia Mkello yumo?!.

Mamluki hao walitumia zana zao za kukatia mkonge, zile sime za makali kuwili, walizisunda kwenye nguo zao za ndani na kusafirishwa kwa mitumbiwi usiku usiku kupitia Kipumbwi. Jee wale mashuhuda wa Mapinduzi yale Matukufu ya Zanzibar, wanayakubali haya?.

Pia mwandishi anamalizia kwa kusema hata mauaji ya Karume, hayakutekelezwa na wapinga Mapinduzi, bali ni miongoni mwa hao hao wanamapinduzi, baada ya kupishana kauli fulani fulani za uendeshaji wa Zanzibar baada ya Mapinduzi.

Nimesoma kitabu cha John Okello kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar,
View attachment 2077618
yeye anasema yake, vitabu kadhaa vya waandishi wazungu wanasema yao, historia tukuka ya Mapinduzi Matukufuya ya Zanzibar nayo nayo inasema kivyake, hivi hakuna any straight line yoyote kuhusu Mapinduzi hayo, ya Zanzibar?.
Jee yalipangwa na nani? Yalitekelezwaje?.
Nini haswa kilichotokea usiku ule wa Januari 11?.
Nani alifanya nini wapi?
Na mwisho tuzungumzie wafaidika wa Mapinduzi hayo Matukufu ya Zanzibar na bila kuwasahau wahanga wa Mapinduzi hayo ambao kwako yatakuwa sio Matukufu, ni kina nani haswa?, na kama kuleta amani na utangamano wa Zanzibar kuhusu Mapinduzi hayo kutahitajika kuundwa kwa Tume ya Ukweli na Upatanisho, "Truth and Reconciliation Commission" ili waliohasimiana kutokana na Mapinduzi hayo, wapatanishwe kwa maslahi mapana ya Zanzibar?.

Majibu ya maswali haya yatasaidia kujua mustakabali wa matokea ya uchaguzi wa Zanzibar kudhirihisha kuwa Wazanzibari ni wamoja, hakuna kundi la walishiriki Mapinduzi ndio wenye uhalali zaidi kuitawala Zanzibar kuliko wasioshiriki, after all kumbe Mapinduzi yenyewe, yametekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde, toka mashamba ya mkonge Tanga!.

Pasco
Rejea za Mwandishi huyu kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
  1. Miaka 50 Ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Bado Kuna Maswali Bila Majibu -1
  2. Neno "Matukufu" Katika Mapinduzi ya Zanzibar, Lilitoka Wapi, na Yana Utukufu Gani?!,
  3. Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa! Walikimbia Wenyewe - Mzee Sukari
Tarehe kama ya leo 11/01/1964 miaka 60 iliyopita, ndio Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalifanyika!. Alfajiri ya Tarehe 12 Januari, 1964 ilikuwa ni kutangazwa tuu!.

Nawatakia maadhimisho mema ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
 
Back
Top Bottom