Miaka 20 Baada ya Kufika Pwani ya Kipumbwi: Historia ya Kipumbwi Katika Mapinduzi ya Zanzibar

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,266
MIAKA 20 BAADA YA KUFIKA PWANI YA KIPUMBWI: HISTORIA YA KAMBI YA KIPUMBWI KATIKA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Miaka 20 iliyopita tarehe kama ya leo 9 December, 2003 ndiyo siku Mohamed Omari Mkwawa alipotufikisha mimi na Dr. Harith Ghassany Kipumbwi.

Siku hii iliangukia kuwa siku Tanganyika ilipopata uhuru wake.
Kipumbwi ni kijiji kidogo cha wavuvi kilomita chache kutoka Tanga.

Hapa Kipumbwi ndipo ilipowekwa kambi ya askari mamluki wengi wao Wamakonde waliokuwa wanapewa mafunzo ili washiriki katika mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964.

Historia hii si ngeni kwa sasa kwani Dr. Ghassany kaieleza kwa kirefu katika kitabu chake, "Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru," (2010).

Lakini kabla ya yeye kufika Kipumbwi na kushuhudia kwa macho yake yale aliyoelezwa na Mzee Mkwawa Tanga mjini kuwa alihusika katika kuwavusha Wamakonde kwa siri kuingia Zanzibar kushiriki katika mapinduzi hii ilikuwa siri kubwa sana.

Sikupata siku kumuona Dr. Ghassany kafurahi kama siku ile.

Kwa hakika kabisa alikuwa na haki ya kufurahi kwani alikuwa amekitegua kitendawili kikubwa; kwanza kuwa kuwa kulikuwa na kambi ya mamluki katika ardhi ya Tanganyika waliovushwa na kuingia Zanzibar kusaidia mapinduzi.

Kafika Kipumbwi na Mzee Mkwawa akatupitisha sehemu zote kuanzia pango la chini walikukuwa wanaficha majahazi yao hadi kutuonyesha mgahawa mdogo walipokuwa wakila usiku kabla ya kuingia katika vyombo na kuanza safari.

Pili Kipumbwi ilisaidia kueleza mauaji yaliyotokea mashamba ambako Waarabu wengi waliuliwa.

Leo naikumbuka siku hii miaka 20 iliyopita na naweka picha tulizopiga Kipumbwi.

PICHA: Picha ya mwisho ni Mzee Mohamed Omari Mkwawa na mkewe.

1702160040508.jpeg

1702160073277.jpeg
1702160107821.jpeg

1702160166653.jpeg
 
Wabondei wapo ,wadigo wapo,wazigua wapo,wamakonde bado wapo pale hakuna mgosi tu😂
Asilimia chache sana wabondei mkuu, Wazigua wapo wa kutosha kuanzia Sakura mpaka Mkwaja huko Na mkalamo ndo wako kibao usiseme.....

Wamakonde Wapo wengi sana Wilaya ya Pngani nafikiri kuliko sehemu yyte Tanga nzima 😅😅😅
Mgosi hawezi ishi huko wako wachache sana
 
Huo ndo ukweli mchungu mkuu...
Wazanzibar walikuwa wameridhia na Utawala wao kwani waliishi kwa Raha..
Story kama hizi ukitaka kuzipata nenda zanzibar na Tanga...
Ilikuaje kina mzeee karume walishiriki yale mapinduzi matukufu? Ina maaana walikua kinyume na wazanzibar wenzao?
 
Kuna wazanzibar walishiriki?
Amenitajia Jina ni John Okelo..
Mapinduzi yale yalikuwa Chinja chinja alot of Genocide sitaki hata kuyazungumzia mkuu!

Nimejaribu kulitafuta Jina ni kweli yeye ndo kiongozi wa Mapinduzi ya zanzibar baada ya kukamilisha wakamkabidhi Karume atabgaze Radioni
 
Mapinduzi yale yalikuwa Chinja chinja alot of Genocide sitaki hata kuyazungumzia mkuu!
Ilikuaje wazanzibar walidai uhuru kwa Mwingereza wakaupata then wakatawaliwa na mwarabu? Au ni mwarabu alipambana kudai uhuru baada ya kupata wazanzibar wakampindua?
 
Amenitajia Jina ni John Okelo..
Mapinduzi yale yalikuwa Chinja chinja alot of Genocide sitaki hata kuyazungumzia mkuu!

Nimejaribu kulitafuta Jina ni kweli yeye ndo kiongozi wa Mapinduzi ya zanzibar baada ya kukamilisha wakamkabidhi Karume atabgaze Radioni
Huyu Ndo mwamba Mwenyewe wa Mapinduzi japo alitishiwa kinoma Mpaka kutishiwa kuuliwa aondoke Nchini..

ElhdAvzW0BEp-nz.jpg_large.jpg

ElhdAvzW0BEp-nz.jpg_large.jpg


276619_original.jpg

images.jpeg
images.jpeg

images (1).jpeg


Hii picha akiwa alna karume akimtangaza..
okelo.jpg



haya ndo magazeti ya kipindi hiyo...

download (1).jpeg



E9w2TjCXoAEhNXi.png

images.jpeg
images (1).jpeg
images (1).jpeg

E9w3U3UXEAY07PE.jpg

E9w-9o0WYAAIZJv.jpg
 
Amenitajia Jina ni John Okelo..
Mapinduzi yale yalikuwa Chinja chinja alot of Genocide sitaki hata kuyazungumzia mkuu!

Nimejaribu kulitafuta Jina ni kweli yeye ndo kiongozi wa Mapinduzi ya zanzibar baada ya kukamilisha wakamkabidhi Karume atabgaze Radioni
Okelo hakuwahi kuwa mwanajeshi,bwana yule alienda kule kisiwani "kubangaiza" tu maisha.

Baadhi ya maandiko yalidai kwamba Okelo alitumika tu sababu alikua na lafudhi ya kutisha sana na sura yenye matisho hivyo kuogofya wapinzani lakini hakuna .

Kumbukumbu rasmi inayoonyesha hakuwahi kupata training yoyote ya kijeshi.
 
Back
Top Bottom