Historia ya NEEMA (Safari yako inaendelea)

Historia ya NEEMA (Safari yako inaendelea)

Amba Samedi

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2024
Posts
205
Reaction score
336
Kuna historia ndani yako inayoshuhudia kuwa hata katika giza zito, nuru iliwahi kuchomoza. Pengine sasa umechoka, Mwili umelemewa, moyo umevunjika, na ndoto zako zinaonekana kwa mbali kwenye upeo wa macho yako.

Lakini historia yako haijaisha bado. Historia yako inajua kusimama tena, kusamehe tena, kuamini tena, na kupigana tena.

Usikate tamaa. Kumbuka ulipotoka. Kumbuka jinsi Mungu alivyokuinua pale ambapo wote walidhani umeanguka. Kumbuka yale machozi yaliyogeuka kuwa ushuhuda. Historia yako ina nguvu. Historia yako ni ushahidi wa rehema ya Mungu isiyoisha.

Leo, vuta pumzi. Simama tena. Tembea kwa imani, hata kama huoni mwisho wa njia. Kwa sababu historia yako bado inaendelea, na mwandishi wake ni Mungu ambaye hajawahi kushindwa.

Historia yako ni ushahidi kwamba bado kuna zaidi huko mbele na yajayo yanafurahisha.

Pr. Makore hapa
Wimbo Ulio Bora Media
 
Kweli nimekumbuka nyakati nilizopitia...ni ngumu, chungu zilizojaa giza kukata tamaa kukosa tumaini na kila mtu alinikimbia mpaka ndugu jamaa na marafiki.....

Kukosa chakula,nguo kuchakaa, viatu kuisha kabisa kabisa...mpaka sehemu nilizokuwa nakwenda kuomba vibarua nilikataliwa au nilidhulumiwa

Njaa ilikuwa ni sehemu ya maisha yangu...na ndio nikaja kugundua kulala njaa mwili asubuhi unaamka ukiwa na nguvu sana, sasa hii sijui ni muujiza kwangu tu au inatokea kwa wote?

Na wakati napitia magumu yote haya nyumbani nilikuwa nina mtoto mchanga na mke wangu kajifungua kwa operation.

Tulianza kuuza vitu kimoja kimoja mpaka nyumba ikabaki inatushangaa....

Mungu saidia hiyo nyumba nilikuwa nimeanza kuijenga haina sakafu..haina plasta tuepauwa vyumba viwili tu...nyoka nnge na wadudu mbalimbali walikuwa ndio maskani yao

Pesa ya mkaa tulikosa nikaanza kuokota chupa nachanganya na kuni kidogo ndio zinakuwa za kupikia..sufuria zote ziligeuka nyeusi kwa ajili ya kupikia kuni.

Watu hasa ndugu walianza maneno kwamba kuna laana za mababu,baadhi ya majirani walitushauri kwenda kwa waganga.

Katika yote hayo kwa ndani kabisa ya moyo wangu kulikuwa na sauti inasema waziwazi kwamba iko siku...na mimi mwenyewe nilikuwa ninajitamkia kwamba iko siku mateso haya yote yatakwisha.

Na kweli acheni Mungu aitwe MUNGU.
 
Kweli nimekumbuka nyakati nilizopitia...ni ngumu, chungu zilizojaa giza kukata tamaa kukosa tumaini na kila mtu alinikimbia mpaka ndugu jamaa na marafiki.....

Kukosa chakula,nguo kuchakaa, viatu kuisha kabisa kabisa...mpaka sehemu nilizokuwa nakwenda kuomba vibarua nilikataliwa au nilidhulumiwa

Njaa ilikuwa ni sehemu ya maisha yangu...na ndio nikaja kugundua kulala njaa mwili asubuhi unaamka ukiwa na nguvu sana, sasa hii sijui ni muujiza kwangu tu au inatokea kwa wote?

Na wakati napitia magumu yote haya nyumbani nilikuwa nina mtoto mchanga na mke wangu kajifungua kwa operation.

Tulianza kuuza vitu kimoja kimoja mpaka nyumba ikabaki inatushangaa....

Mungu saidia hiyo nyumba nilikuwa nimeanza kuijenga haina sakafu..haina plasta tuepauwa vyumba viwili tu...nyoka nnge na wadudu mbalimbali walikuwa ndio maskani yao

Pesa ya mkaa tulikosa nikaanza kuokota chupa nachanganya na kuni kidogo ndio zinakuwa za kupikia..sufuria zote ziligeuka nyeusi kwa ajili ya kupikia kuni.

Watu hasa ndugu walianza maneno kwamba kuna laana za mababu,baadhi ya majirani walitushauri kwenda kwa waganga.

Katika yote hayo kwa ndani kabisa ya moyo wangu kulikuwa na sauti inasema waziwazi kwamba iko siku...na mimi mwenyewe nilikuwa ninajitamkia kwamba iko siku mateso haya yote yatakwisha.

Na kweli acheni Mungu aitwe MUNGU.
Hongera sana mkuu kwa kuvuka hatua hii. Mungu sio athumani, na hutoa njia pasipo na njia
 
Back
Top Bottom