Historia ya mkoa wa Tanga

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,112
Mkoa wa Tanga una eneo la 27,348 km² na uko Kaskazini Mashariki mwa Tanzania ukipakana na Kenya upande wa Kaskazini, Bahari Hindi upande wa mashariki na mikoa ya Morogoro, Manyara na Kilimanjaro. Mpaka upande wa kusini unafuata mto wa Mligaji. Mkoa wa Tanga unaunganisha sehemu za pwani pamoja na milima ya ndani kama Usambara.

Kuna wilaya 10 ambazo ni Handeni Vijijini, Handeni Mjini, Kilindi, Korogwe Vijijini, Korogwe Mjini, Lushoto, Mkinga, Muheza, Pangani na Tanga Mjini. Eneo linalofaa kwa kilimo ni 17,000 km². Tanga ni kati ya mikoa midogo ya Tanzania ikiwa na msongamano mkubwa wa wakazi ndani ya eneo lake.

Jina hili la mji wa Tanga lilitokana neno la Kiajemi lenye maana nne tofauti ambazo ni: Iliyo nyooka; Bonde lenye rutuba; Barabara upande wa mto na Shamba juu ya mlima, neno hilohilo la Tanga kwa kabila la Kibondei ambalo ni wenyeji wa mkoa huo linamaana ya shamba, wao hulitamka N'tanga.

Tanga inasamekana imeanzishwa na wafanyabiashara Waajemi katika karne ya 14 BK. Mji wa Tanga haikupata umuhimu kama mji wa jirani ya Mombasa. Tarihi ya Pate inasema ya kwamba kabla ya kuja kwa Wareno Pate iliwahi kutawala Lindi kwa muda fulani. Katika karne ya 19 BK Tanga ilikuwa chini ya utawala wa Omani na Zanzibar. Misafara ya biashara imeanzishwa hapa kwenda bara.

Kutokana na bandari yake nzuri ya kiasili Tanga ilikua sana wakati wa ukoloni wa Wajerumani waliojenga bandari wa kisasa pamoja reli kwanda Moshi. Reli iliwezesha kilimo kwa ajili ya soko la dunia Tanga ikawa bandari kuu kwa jili ya katani na kahawa. Baada ya Uingereza kuchukua utawala wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani reli ya Tanga-Moshi iliunganishwa na ile ya kati hivyo ikawa na njia kwenda Daressalaam pia.

Wakati wa Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Tanga iliona mapigano makali tar. 3 - 5 Novemba 1914. Jaribio la Uingereza kuvamia Tanga kwa kikosi cha maaskari 8000 Waingereza na Wahindi kutoka meli kwenye Bahari Hindi ilishindwa vibaya na Jeshi la Ulinzi wa Kijerumani chini ya uongozi wa Paul von Lettow-Vorbeck.

Mwaka 1922 "Tanganyika Territory African Civil Services Association" (TAA) iliundwa Tanga ambayo ilikuwa shirika ya kwanza ya Kiafrika yenye shabaha za kisiasa.

Hali ya hewa
Kwa jumla hali ya hewa ni joto lenye unyevu. Handeni kuna joto ikiwa pakavu zaidi. Milima ya Usambara hapana joto sana. Miezi ya Desemba - Machi halijoto huko Tanga inafikia sentigredi 30-32 mchana na 26-29 usiku. Wakati wa Mei hadi Oktoba halijota inapoa ni sentigredi 23-28 mchana na 20-24 usiku. Unyevu iko juu kati ya asilimia 100 na asilimia 65.

Maeneo mengi ya mkoa hupokea angalau milimita 750 za mvua kwa mwaka au zaidi. Pwani ni zaidi takriban milimita 1,100 hadi 1,400 mm ikipungua sehemu za ndani isipokuwa milima ya Usambara ambako mvua inaweza kuzidi milimita 2000 kwa mwaka.

Makabila na wakazi
Makabila makubwa mkoani Tanga ni Wasambaa, Wazigua, Wabondei na Wadigo. Wasambaa ndio kabila kubwa lililoko katika milimani ya Usambara, Muheza, Korogwe na Lushoto. Kwa jumla ndio asilimia 40 ya wakazi wote wa mkoa.

Wazigua ni kabila kubwa huko Handeni na sehemu za Korogwe na Pangani. Wabondei wako hasa Muheza na sehemu za Pangani. Wadigo ndio wengi Tanga penyewe na sehemu za Muheza.

Msongamano wa wakazi ni mkubwa hasa wilaya ya Lushoto penye ardhi yenye rutuba nzuri. Wiyala ya handeni kuna machimbo ya madini.ila kuhusu elimu ipo nyuma sana.kwani mpaka sasa hakuna shule ya sekondari inayotoa huduma ya kidato cha tano na sita.kama haitoshi shule za watu binafsi hakuna ata moja

Elimu
Katika mkoa huu elimu inahitajika zaidi kuboreshwa hasa naeneo ya vijijini maana watu wengi wa mkoa huu hufanya shughuli zao za kimila hali hiyo huwafanya kushindwa kuendelea elimu pamoja na shughuli za kimaendeleo katika ujenzi wa taifa la tanzania

Uchumi
Wakazi wengi hutegemea kilimo cha riziki pamoja na ufugaji na uvuvi. Mazao ya chakula hasa ni mahindi, muhogo, ndizi, maharagwe na mpunga. Mazao ya biashara ni katani, pamba, kahawa, chai, nazi, tumbaku na korosho. Mifugo ni ngombe, mbuzi na kondoo pamoja na kuku.

Katani ilikuwa zao la biashara hasa kwa ajili ya Tanga tangu kuingizwa kutoka Mexico zamani za Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Hulimwa kote mkoani isipokuwa Lushoto, hasa Muheza na Korogwe kwenye mashamba makubwa. Mashamba haya yalikuwa ya walowezi, yalitaifishwa baada ya uhuru. Tangu kuanguka kwa sekta ya umma yamebinafsishwa tena siku hizi. Zao la katani inategemea sana soko la dunia, umuhimu wake ilirudi nyuma tangu miaka ya 1960.

Tanga ilikuwa na viwanda vingi kiasi katika miaka ya 1960 na 1970 lakini karibu vyote vimekwama kutokana na siasa ya Ujamaa na uchumi wake ulioiga mfumo wa nchi za kisoshalisti. Viwanda vichache vilivyobaki havizalishi mali kulingana na uwezo wao. kilichobaki hasa ni kiwanda cha saruji Tanga.
Utalii umeanza kupanuka kidogo hasa katika eneo la Pangani,Mapango ya Amboni na kituo cha Makumbusho URITHI Tanga.

1579586785980.png

Mkoa wa Tanga unapopatikana katika ramani Tanzania

1579587056342.png

Ramani ya mkoa wa Tanga

1579586887911.png

Picha ikionesha hali ya hewa mkoa wa Tanga

1579587309869.png

Mapango ya Amboni ni moja ya vivutio vya kitalii vilivyopo mkoani Tanga
 
Mapango ya Amboni, kijiji cha kigombe umekisahau, kulikua na mzee hamisi, (rejea kiswahili darasa la nn) cha zamani
 
Unaposema Tanga hakuna shule za kidato cha tano na sita, sijui unaelezea Tanga ipi.Lakini kama Tanga,Tanzania,ina shule zifuatazo za serekali na watu binafsi zenye vidato vya tano na sita,kwa Tanga mjini,Wacha huko wilayani:
Tanga Tech
Galanos
Usagara
Masechu
Popatlal
Coastal
Arafa
Istiqama
Al kheir
Hizo ni za Tanga mjini,bado za nje ya mji wa Tanga na wilaya zake.
Na kuhusu shule za binafsi ni nyingi,kuanzia msingi mpaka secondary,na vyuo pia vipo vingi.
 
Hata Wilaya ya Handeni ina Shule ya kidato cha sita, Shule inaitwa Handeni Sekondari mwanzo ilikuwa O-level tu lakin sasa hivi imeongezewa na A-level kwa boys ina zaidi ya miaka 3
 
Umesema Tanga ina wilaya 10. Wilaya ziko 8. Kuna wakuu wa wilaya wanane katika mkoa. Wilaya ni Tanga mjini, Muheza, Mkinga, Pangani, na Korogwe.

Wilaya zingine ni Lushoto, Handeni na Kilindi.

Tofaufisha wilaya na halmashauri. Korogwe kuna halmashauri mbili ktk wilaya moja. Handeni kuna majimbo mawili wilaya moja.
 
Kwa Lushoto zipo shule kama Shambalai naJonas hubiri za serikali advanced level na Lwandai private


Pia kule Lushoto kuna kabila la waambugu naona hujaliongolea mkuu
 
KWENYE POINTI YA KUSEMA MKOA WA TANGA NI KATI YA MIKOA MIDOGO SIKUBALIANI NA WEWE TANGA NI MKOA MKUBWA SANA NDIO MAANA UNA WILAYA NYINGI 10 KULIKO MKOA WOWOTE TZ.ULIPASWA KUGAWANYWA KATIKA MIKOA MIWILI KAMA SIO MITATU.SIJUI VIONGOZI WETU HAWALIONI HILI.TANGU UHURU NI MKOA WA TANGA AMBAO MPAKA LEO HAUJAGAWANYWA.UKIACHANA NA PROPAGANDA HAKUNA MKOA MZURI NA WENYE MAENDELEO KAMA TANGA KILA BINADAMU ANATAMANI KUISHI MKOA WA TANGA.TATIZO LETU NI SIASA TUNACHAGUA VIONGOZI HASA WABUNGE KWA AJILI YA KUJUANA SIO MAENDELEO.HATA ULAYA WANAJUA TANZANIA NI TANGA.WAJERUMANI WALIJIKITA SANA TANGA NA MJI WAO MKUU ULIKUWA LUSHOTO.SHIME SHIME WANA TANGA TUCHAGUE VIONGOZI WENYE VISION ILI KURUDISHA HADHI YA MKOA WETU.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom