Kamanda mkuu wa jeshi la CHADEMA mkoa mpya wa Njombe akishirikiana na kamanda Nyagawa(Lutondwe).Amedhamiria kuhakikisha ifikapo 2014 jina la CCM linabaki historia katika mkoa mpya wa Njombe.Kamanda huyo ambaye anafanya kazi ya kueneza chama usiku na mchana katika mkoa mpya wa Njombe tayari amefungua zaidi ya matawi 180 ndani ya mwaka mmoja na anatarajia kuendelea kufungua matawa katika kata zote za mkoa huo.Jumamosi na jumapili ya tarehe 14.4.2012 na 15.4.2012 ataongoza kikosi cha maangamizi katika tarafa ya Lupembe,eneo ambalo linaongozwa na mbunge aliyeandika historia ya kuingia bungeni kwa elimu ya K.K.K.
Mikutano ya mwishoni mwa wiki itaanza katika kijiji cha Madeke mpakani na Morogoro,Mfiriga na Igombola.Siku ya jumapili ya tarehe 15 atakuwa Lupembe barazani na Matembwe.
Kwa kuwa ni wakati mwafaka wa kuleta mabadiliko katika nchi yetu,mheshimiwa Nyimbo anawaomba wazalendo wote duniani kute kujitokeza ili kuleta ukombozi wa kweli na uhuru wa kweli.
Mikutano ya mwishoni mwa wiki itaanza katika kijiji cha Madeke mpakani na Morogoro,Mfiriga na Igombola.Siku ya jumapili ya tarehe 15 atakuwa Lupembe barazani na Matembwe.
Kwa kuwa ni wakati mwafaka wa kuleta mabadiliko katika nchi yetu,mheshimiwa Nyimbo anawaomba wazalendo wote duniani kute kujitokeza ili kuleta ukombozi wa kweli na uhuru wa kweli.