Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,703
- 218,248
Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Njombe anayemaliza muda wake , Kamanda kabisa Rose Mayemba , ambaye ametajwa kuinyoosha ccm katika uongozi wake Mkoani humo , huku akiisambaza Chadema hadi kwenye maeneo ambayo awali yaliamini kwamba CCM ni dini , ameomba tena nafasi ya uenyekiti wa Chadema Mkoani humo
Huyu mama ndio aliyewaambia watu wa Nyasa waliodanganywa kwamba CCM ni dini kwamba , Dini haiwezi kuwasababishia umasikini wa kutupwa walionao , hapo ndipo watu wa ludewa wakaanza kufunguka na kujiunga na CHDEMA. Hebu jaribu kutafakari hili , Binadamu kwa vile wako gizani basi wanadanganywa kwamba ccm ni dini na kwamba wakihama, kule mbinguni watakutana na moto kama ule wataoukuta Watenda dhambi wengine!
Hata hivyo Mayemba alifutilia mbali uongo huu na kwa mafanikio huku akijaza ofisi za Chadema Ludewa bila huruma yoyote ile
Wamejaribu hata kumtisha na hata kumloga (Kumbuka hiyo mikoa) lakini wamechemsha na hakuwahi kutetereka, Hebu angalieni, Chama cha siasa kinapanga njama za kumloga kiongozi wa upinzania yaani .
Binafsi namtakia kila la heri.