Historia ipo kututukumbusha mengi, kiburi hakisaidii

Historia ipo kututukumbusha mengi, kiburi hakisaidii

Usisahau...
Bajeti ya nchi yetu wanaijazia wao...
Sisi tukikusanya 100% basi 60% yote inakwenda kwenye matumizi ya Serikali Kuu, Idara zake zote, Mahakama na Bunge

Inayobakia 40% inakwenda kwenye mipango ya maendeleo, lakini ki uhalisia hii 40% huwa hata haifiki ama inafika kwa % ndogo mno, hizo figure wanazozisoma Bungeni huwa ni justification tu ya kisheria,

Kwa mfano hawa mabeberu wakigoma kutoa Misaada hasa kwenye Secta ya Afya tu na hii Corona aisee - sitaki kufikiria.
 
Huyu Mahiga inaonekana ana historia kubwa na nchi yetu tusiyoifahamu. Hebu siku moja mtu mwenye dondoo alizoifanyia nchi yetu kwenye matukio muhimu aziweke tupate kumfahamu maana inaonekana kuna watu wanataka asijulikane kiasi cha kuziba pengo lake hata kabla kaburi lake halikafukiwa wakati inaonekana kuna mengi sana kaifanyia nchi hii

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijui huwa taratibu zikoje za kuweka hadharani matukio yaliyokwisha pita muda mrefu, ila Mheshimiwa Mabere Nyaucho Marando anaweza tusaidia kwa hili, inasemekana kuwa yeye aliongoza kikosi cha kumkakata Captain Tamimu (komandoo), hawakufanikiwa kumkata hai, kwani aliuwawa kwa kupigwa risasi mchana kweupe huko Kinondoni.
 
Kwahiyo wewe na akili zako unaona Mabeberu ni watu wema?

Kweli ujinga ni mzigo
Kama ni wabaya wanapotuletea Pesa tusiwaite kwa jina la wahisani,au hao mabeberu wanapokutana na viongozi wetu wawaambie kuwa ninyi ni mabeberu na hela zenu hatutaki.Mbona tunapokea misaada toka kwao? Tuache unafiki?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tusidanganyane, kwa wanahistoria wanafahamu kuwa Neo Colonialism ni mfumo halisi ulioratibiwa kimkakati ili nchi za Africa ziendelee kutawaliwa. Uhuru wa bendera uliotolewa ulikuwa ni wa makusudi kabisa, lakini uchumi na masuala mengine uhuru huo HATUNA! Na hakuna mnanja wa kujitoa kwenye mfumo huo isipokuwa labda Africa yote iungane, tutengeneze uchumi wetu wenyewe, tuwe na viwanda vyetu wenyewe, tuuziane sisi wenyewe, kama hilo litawezekana hapo tutashinda vita dhidi ya mabeberu. Kinyume cha hapo ni mbwembwe tu! Tutaendelea kula vya mabeberu na tutaendelea kuwapigia magoti. Mwl. Nyerere alijaribu kwa kupitia mfumo wa ujamaa na kujitegemea, alijitahidi sana kuishawishi Africa iungane maana alijua ndio njia pekee ya kujitegemea kama Africa lakini haikuwezekana. Mtoa mada umeona mbali, kwa wanaokubeza ni wale wasiojua chochote juu ya mifumo ya dunia inavyofanya kazi.
 
Mleta mada una takwimu zozote za corona.
Ambazo ni tofauti na za wizara ya afya?.

Kama Who wamekubali kusubiri taarifa Za serikali wasubiri haraka za nini.
Vinginevyo watupe takwimu zao kuhusu corona hapa Tanzania na ziwe sahihi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
JERUSALEMU,

yani wewe hata mabeberu wakikwambia huwe shoga utakubali.
nikukatishe kwanza na historia yako usiyo jua. uchumi wa tanzania ulikuwa mzuri hata kufanya thamani ya pesa kuwa nzuri kuliko hile ya marekani.

Kwa kuwa marekani thamani yake ya pesa kipindi kile kwa nchi za afrika na sehemu zingine ilikuwa aina thamani.kama unavo jua waswahili wanavo sema ukitaka ufanikiwe waharibie wanzako wanao kuzunguka ili wewe huwe bora.
kasome kitabu cha ujasusi cha eriko nyerere


Sent from my iPhone using JamiiForums
Unatakiwa kutumia akili kuchambua mambo! Kwanini wamarekani wote ni mashoga? Je,Hakuna watanzania mashoga? Wamefundishwa na mabeberu? Wewe wazazi wako walikufundisha kufanya mapenzi? Msiharibu uwezo wenu wa kufikiri tu kwasababu unalipwa book 7!

Mimi nimeshuhudia transformation ya uchumi wa Tanzania toka enzi za TANU! Wakati huo wajinga kama wewe wasinge pewa kuchangia chochote.
 
Kwahiyo wewe na akili zako unaona Mabeberu ni watu wema?

Kweli ujinga ni mzigo
Mkuu wala usipoteze muda,hawa vijana wa leo wanaunga ujinga hawajui madhara tuliopata hadi Mwl.Nyerere akajingatua kwa aibu.

Mtoto akitaka kuchezea wembe mpe.
 
Hata hiyo chupi uliyovaa wametengeneza wao, pedi uliyovaa wametengeneza wao. Hivi wewe dada unajielewa?

Hivyo vidonge vya kuzuia mimba unavyotumia tukikutana wametengeneza hao mabeberu. Kuwa na adabu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakika umemaliza kila kitu! Huo ndio ukweli. Kila kitu unacho tumia kinatoka kwao halafu mnajitia ujeuri ili mharibu maisha ya watanzania. Kuwa na adabu.
 
Mimi namtoa BWM kwa kuwa tuko hapa kwa matokeo ya wana Mtandao wale wa u-Rais wa 2005. Halafu JAKAYA alipofika madarakani yeye na mshirika wake LOWASA walianza kwa kumchafua BWM. Wakamtengenezea kashfa ya Mgodi wa Kiwira through TANPOWER. wakasema mpaka akadharaulika mbele ya jamii.

Isitoshe, Jakaya Mrisho Kikwete ameshindwa kabisa kuacha LEGACY kwa kuwa
1.Ni yeye peke yake aliyelazimisha kubadili Katiba ya CCM kwa kuwatoa Viongozi na Marais Wastaafu kwenye Central Committtee ili apate nguvu nyingi binafsi
2 Alishindwa kutuachia Katiba mpya pamoja na kutumia Mabilioni ya fedha za walipa Kodi
3.Jakaya ndiye alikuwa Mwenyekiti wa Kamati Kuu iliyomingiza Magufuli kuwamo kwenye 5 Bora
4. UDHAIFU wake ndiyo uliopelekea CCM kutaka mtu mbabe!
5. Aliendekeza BIFU lake binafsi na LOWASSA

My take: We are here BECAUSE of JK and dont include BWM
Sikubariani na wewe! Aliyeanza kuharibu nchi zaidi ni Mkapa. Nakubali kuwa Kikwete hakututendea mema kwa katiba ya CCM na ya nchi! Lakini mengine yote muasisi ni Mkapa, tangu ufisadi, makundi, na kuminya demokrasia,! Hata kuingia Kikwete unayemlalamikia Mkapa ndio alisababisha vinginevyo raid angekuwa Salim! Mkapa ndio amefanya taifa letu kukosa muelekeo hata huyu tuliyenaye ni kazi yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah! Nimezaliwa 1975, std 1 1985 baada ya mkono kufeli kushika sikio la pili. Tuliokuwa na REDIO nikawa msikilizaji mzuri. Nakumbuka hicho kipindi kigumu. Baba,alishona viraka, ukiwa na Rafiki TPC, POLICE MAISHA YENU YANSKUWA NAFUU SANA. Sukari ilikuwa kama Dawa ya mgonjwa, Mzazi anaitunza sana, akiwa mgonjwa jirani wanakuja omba sukari, kulikuwa na wagambo wababe sana. Sitasahau. Mungu atusaidie tusirejee kule. Hawa watoto waliozoea chai daily sijui itakuwaje.
Kwa kweli kuna kizazi hiki cha kuanzia miaka ya 90 ambao ndio wengi kwenye mitandao,hawawezi kujua hali ilivyokuwa ngumu miaka ya 80 - 86

Kulikuwa na kipindi kigumu sitaki hata kukikumbuka.Nilikuwa mdogo sana ila hali tuliyokuwa tunapitia haijatoka akilini.

Kukosa sabuni za kufulia,kukosa mafuta ya kula,kula unga ulioharibika kutoka NMC,kutembea bila Viatu,viraka na wakati mwingine makalio yanabaki wazi,sukari guru au miwa kutumika kwenye chai(vikiwepo),Uji wa chumvi,kukosekana kwa dawa muhimu(Nakumbuka dawa ya sikio ilikuwa mafuta ya Kuku),kutokupatikana kwa magodoro,(watu wakilalia magodoro ya makapi ya mbegu za pamba,au gunia zilizotiwa nyasi),kutokuwepo kwa dawa za mbu za kutosha kiasi kwamba watu walichoma magunia ili mbu wakimbie kwa ule moshi,kuwepo kwa kunguni sugu wengi,chawa kwa wingi ilikuwa kawaida sana,vifo vya wajawazito ilikuwa tishio mno...na mengine mengi.

Kusema kweli sitaki kuzikumbuka Siku hizo na nilikuwa naomba Mungu zisotokee tena katika uhai wangu.Ninatamani kizazi changu kipite,ili kama kuna watu wanakiburi cha kupambana na hao mnaowaita mabeberu,mpambane nao.

Vijana wengi wanaishi kwa ndoto tu.Wanaona maisha ya kwenye muvi wanadhani ndiyo uhalisia.Na sisi watu wazima,tukiwapotosha,tutajikuta tunawaangamiza sana.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mleta mada una takwimu zozote za corona.
Ambazo ni tofauti na za wizara ya afya?.
Kama Who wamekubali kusubiri taarifa Za serikali wasubiri haraka za nini.
Vinginevyo watupe takwimu zao kuhusu corona hapa Tanzania na ziwe sahihi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi wewe unafikiri unaweza kuwadanganya? Chombo chochote kama Simu, TV, computer na hata hiyo machine inayo tumika kupima Covid-19 na kutoa data haina siri! Jiulize China walipo taka kudanganya walifanikiwa? Kwanini?
Na mimi nasema,kwa kizazi hiki,yakiwakuta yale ya miaka ya 80,nakuhakikishia kuwa hali itakuwa mbaya mno.Hawana uvumilivu kabisa hawa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unajua hawa watoto wanafikiri hivi tulivyo hatuwezi kufilisika na kuwa masikini Kabisa. Kumbe tukitengwa mwaka mmoja tu yaani tutakuwa hoi bini taabani. Huna mafuta, huna mazao ya kuuza nje unategemea nini?
 
Kwahiyo wewe na akili zako unaona Mabeberu ni watu wema?

Kweli ujinga ni mzigo
Sio wema ila ndio tegemeo letu kwa %80, hatuna uwezo wa kuwavimbia wakati sisi ni tegemezi
 
Usitutishe, IMF, WHO, zipo kwa sababu Tanzania ipo, propaganda za vitisho hazisaidii na hakuna nchi ambayo hajapitia kwenye changamoto za kiuchumi, Kama tulipita uko unakotuonyesha unafikiri tutashindwa kupita hapa. Hata Kama tukiachwa nakuhakikishia tutavuka na kujiamini ndio kutaongezeka Mara Mia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom