Historia ipo kututukumbusha mengi, kiburi hakisaidii

Historia ipo kututukumbusha mengi, kiburi hakisaidii

JERUSALEMU

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2012
Posts
3,156
Reaction score
3,627
Salamu wanajamvi!

Niende kwenye mada moja kwa moja. Miaka ile ya 1980, Mwalimu Nyerere alishauriwa na Mabeberu ashushe thamani ya shillingi ya Tanzania ili kuokoa uchumi ulio kuwa unaporomoka kwasababu mbalimbali, Mwalimu akagoma. Wakati ule dola moja ya Marekani ilikuwa sawa na shillingi 7 za Tanzania. Wachumi pia walijaribu kumpa ushauri, akagoma.

Benki ya Dunia na shirika la fedha ulimwenguni wakasema madhali Mwalimu amekataa ushauri wao basi hawata mpa ushirikiano wowote ! Gavana wa Benki kuu naye akaamua kujiuzulu ili kama fedheha imkute Nyerere peke yake. Mwingereza naye akasema kwakuwa Nyerere ametaifisha mashamba ya chai ya Waingereza basi hawataisaidia Tanzania kwa lolote.

Mwalimu alitoa hotuba Kali sana kule Kigoma. Kesho yake wakinga wanao jiita wazalendo wakaandaa maandamano Nchi nzima wakimsifia wakisema mabeberu hawatubabaishi.

Ilipo fika mwaka 1983 hali ulikuwa mbaya usipime! Kuna wakati Petrol na dizel iliadimika Nchi nzima kwa karibu wiki mbili. Maduka yote yakakosa bidhaa. Ghafla tukawa masikini wa kutupwa. Kisa ukaidi.

Leo Nchi yetu imeingia kwenye mivutano na Benki ya Dunia kwa sababu za hivyo

Tunavutana na IMF kwa mambo yasiyo na msingi Kabisa.

Tumeingia kugombana na Shirika la Afya Duniani kwa mambo yasiyo na maana Kabisa. Hutoi takwimu halafu unazika watu usiku unategemea Dunia isikukemee?

Tutatengwa! Na ikifika hapo tutajuta.

Fikiria unyimwe dawa za wagonjwa wanao ishi na virusi vya HIV kwa miezi miwili tu hali itakuwaje?

Fikiria mabeberu wasisaidie bajeti yetu Kabisa, unajua maana yake?

Mabeberu wasitusaidie katika kupambana na malaria na Covid-19 unajua madhara yake?

Kwa maoni yangu tuache uzalendo wa kijinga, hatuishi Dunia ya peke yetu! Tunategemeana.

Tukileta ujuaji tutaangamia tena vibaya mno. Covid-19 ipo na HIV ipo! Tushirikiane na Dunia kuokoa watu wetu.
 
JERUSALEMU,

yani wewe hata mabeberu wakikwambia huwe shoga utakubali.
nikukatishe kwanza na historia yako usiyo jua. uchumi wa tanzania ulikuwa mzuri hata kufanya thamani ya pesa kuwa nzuri kuliko hile ya marekani.

Kwa kuwa marekani thamani yake ya pesa kipindi kile kwa nchi za afrika na sehemu zingine ilikuwa aina thamani.kama unavo jua waswahili wanavo sema ukitaka ufanikiwe waharibie wanzako wanao kuzunguka ili wewe huwe bora.
kasome kitabu cha ujasusi cha eriko nyerere


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ilipo fika mwaka 1983 hali ulikuwa mbaya usipime! Kuna wakati Petrol na dizel iliadimika Nchi nzima kwa karibu wiki mbili. Maduka yote yakakosa bidhaa. Ghafla tukawa masikini wa kutupwa. Kisa ukaidi.
Ninakumbuka Muamar Ghadafi alitupa msaada wa mafuta kulipa fadhila za mateka wa Libya waliotekwa kwenye vita ya Uganda. Hali ya nchi kiuchum ilikuwa mbaya sana. Lugakingira na akina Mcgee, Mapunda, Kamando na wengineo wakaanza kupanga yao.

Tumshukuru sana marehemu Mahiga wakati huo akijulikana kama Mr. X kwa kuokoa jahazi, vinginevyo sijui Tanzania ingekuwa hii inayoonekana sasa au vp?
 
yani wewe hata mabeberu wakikwambia huwe shoga utakubali.
nikukatishe kwanza na historia yako usiyo jua. uchumi wa tanzania ulikuwa mzuri hata kufanya thamani ya pesa kuwa nzuri kuliko hile ya marekani.kwa kuwa marekani thamani yake ya pesa kipindi kile kwa nchi za afrika na sehemu zingine ilikuwa aina thamani.kama unavo jua waswahili wanavo sema ukitaka ufanikiwe waharibie wanzako wanao kuzunguka ili wewe huwe bora.
kasome kitabu cha ujasusi cha eriko nyerere


Sent from my iPhone using JamiiForums
Thamani ya pesa inakuwa mzuri kiaje wakati hata dawa za meno madukani hazikuwepo?!

Uchumi na thamani ya pesa inakuwa mzuri kiaje wakati wananchi walikuwa wanatumia mipapai kufulia kama mbadala wa sabuni?!

Uchumi na pesa vilikuwa vizuri kiaje wakati taifa lilikuwa halifanyi uzalishaji wa kutosha wa ndani na hivyo kuchochea export ambayo ndiyo ingesababisha shillingi kuwa na thamani yake halisi?!

Seems ama una uelewa mdogo sana wa masuala ya uchumi, fedha na international trade au hufahamu kabisa hayo mambo au unaamua tu kujitoa ufahamu!

In 1980's, hatukuwa na vigezo vya kiuchumi vya kuifanya shillingi yetu iwe na thamani kubwa!

Export ilishuka sana! Production ilishuka sana! Hata Foreign Reserve hatukuwa nayo ya kutosha!!

Sasa how come shillingi iwe na thamani?!

Jibu ni rahisi tu: Shillingi ilikuwa overvalued!

Just Google "What's Currency Overvaluation" na utapata jibu kwanini shillingi ilionekana kuwa na thamani kuliko thamani yake halisi!

Na ingawaje watu wengi wanadhani sarafu kuwa na "thamani" kubwa ni jambo jema lakini kiuchumi ni kinyume chake, na ndio maana Mabeberu walimshauri Mwalimu ASHUSHE thamani ya shilingi.
 
Ninakumbuka Muamar Ghadafi alitupa msaada wa mafuta kulipa fadhila za mateka wa Libya waliotekwa kwenye vita ya Uganda. Hali ya nchi kiuchum ilikuwa mbaya sana. Lugakingira na akina Mcgee, Mapunda, Kamando na wengineo wakaanza kupanga yao. Tumshukuru sana marehemu Mahiga wakati huo akijulikana kama Mr. X kwa kuokoa jahazi, vinginevyo sijui Tanzania ingekuwa hii inayoonekana sasa au vp?
Huyu Mahiga inaonekana ana historia kubwa na nchi yetu tusiyoifahamu. Hebu siku moja mtu mwenye dondoo alizoifanyia nchi yetu kwenye matukio muhimu aziweke tupate kumfahamu maana inaonekana kuna watu wanataka asijulikane kiasi cha kuziba pengo lake hata kabla kaburi lake halikafukiwa wakati inaonekana kuna mengi sana kaifanyia nchi hii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wajinga wanafikiri we can move on our own.
 
salamu wanajamvi!
Niende kwenye mada moja kwa moja. Miaka ile ya 1980, Mwalimu Nyerere alishauriwa na Mabeberu ashushe thamani ya shilling ya Tanzania ili kuokoa uchumi ulio kuwa unaporomoka kwasababu mbalimbali, Mwalimu akagoma. Wakati ule dola moja ya Marekani ilikuwa sawa na shilling 7 za Tanzania. Wachumi pia walijaribu kumpa ushauri, akagoma.

Bank ya Dunia na shirika la fedha ulimwenguni wakasema madhali Mwalimu amekataa ushauri wao basi hawata mpa ushirikiano wowote ! Govana wa Bank kuu naye akaamua kujiuzulu ili kama fedheha umkute Nyerere peke yake. Mwingereza naye akasema kwakuwa Nyerere ametaifisha mashamba ya chai ya Waingereza basi hawataisaidia Tanzania kwa lolote.

Mwalimu alitoa hotuba Kali sana kule Kigoma. Kesho yake wakinga wanao jiita wazalendo wakaandaa maandamano Nchi nzima wakimsifia wakisema mabeberu hawatubabaishi.

Ilipo fika mwaka 1983 hali ulikuwa mbaya usipime! Kuna wakati Petrol na dizel iliadimika Nchi nzima kwa karibu wiki mbili. Maduka yote yakakosa bidhaa. Ghafla tukawa masikini wa kutupwa. Kisa ukaidi.

Leo Nchi yetu imeingia kwenye mivutano na Bank ya Dunia kwa sababu za hivyo

Tunavutana na IMF kwa mambo yasiyo na msingi Kabisa.

Tumeingia kugombana na shirika la Afya Duniani kwa mambo yasiyo na maana Kabisa. Hutoi takwimu halafu unazika watu usiku unategemea Dunia isikukemee?

Tutatengwa! Na ikifika hapo tutajuta.

Fikiria unyimwe dawa za wagonjwa wanao ishi na virusi vya HIV kwa miezi miwili tu hali itakuwaje?

Fikiria mabeberu wasisaidie bajeti yetu Kabisa, unajua maana yake?

Mabeberu wasitusaidie katika kupambana na malaria na Covid-19 unajua madhara yake?

Kwa maoni yangu tuache uzalendo wa kijinga, hatuishi Dunia ya peke yetu! Tunategemeana.

Tukileta ujuaji tutaangamia tena vibaya mno. Covid-19 ipo na HIV ipo! Tushirikiane na Dunia kuokoa watu wetu.
Potelea mbali, liwalo na liwe. Hawa ndugu wawili lazima waombe toba kwa watanzania. Mmetukosea sana kwa mliyofanya 2015. Mmetupa JANGA KUBWA. naomba kuishia hapo ila kwa uhalisia tuna kiumbe ambacho haikikupaswa kuwa kilipo.
Mimi namtoa BWM kwa kuwa tuko hapa kwa matokeo ya wana Mtandao wale wa u-Rais wa 2005. Halafu JAKAYA alipofika madarakani yeye na mshirika wake LOWASA walianza kwa kumchafua BWM. Wakamtengenezea kashfa ya Mgodi wa Kiwira through TANPOWER. wakasema mpaka akadharaulika mbele ya jamii.

Isitoshe, Jakaya Mrisho Kikwete ameshindwa kabisa kuacha LEGACY kwa kuwa
1.Ni yeye peke yake aliyelazimisha kubadili Katiba ya CCM kwa kuwatoa Viongozi na Marais Wastaafu kwenye Central Committtee ili apate nguvu nyingi binafsi
2 Alishindwa kutuachia Katiba mpya pamoja na kutumia Mabilioni ya fedha za walipa Kodi
3.Jakaya ndiye alikuwa Mwenyekiti wa Kamati Kuu iliyomingiza Magufuli kuwamo kwenye 5 Bora
4. UDHAIFU wake ndiyo uliopelekea CCM kutaka mtu mbabe!
5. Aliendekeza BIFU lake binafsi na LOWASSA

My take: We are here BECAUSE of JK and dont include BWM
 
Kuna watu wanajiita maskini jeuri lakini hawajui kama hii falsafa ni ya mtu binafsi na haitakiwa kuhusisha familia achilia mbali kwa Taifa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Magufuli alichaguliwa na watu milioni 8, CCM ina wanachama takiribani 10 milioni.Tanzania Ina watu karibia milioni 60. Je hawa watu milioni 45+ tuko wapi? Hadi tutegemee maamuzi ya mtu mmoja kwenye kila kitu
 
Ndio mkome kuchagua kila mtu mkidhani anaweza kuwaongoza kuna wengine hata familia zao walishindwa nyie mnamkabidhi nchi
Kweli mkuu, shida ni ujinga wewe. Mama Jesca alijitahidi sana kutuonesha kwamba huyu mtu hafai but watu tuliangalia tu faida za muda mfupi
 
Kwa kweli kuna kizazi hiki cha kuanzia miaka ya 90 ambao ndio wengi kwenye mitandao,hawawezi kujua hali ilivyokuwa ngumu miaka ya 80 - 86

Kulikuwa na kipindi kigumu sitaki hata kukikumbuka.Nilikuwa mdogo sana ila hali tuliyokuwa tunapitia haijatoka akilini.

Kukosa sabuni za kufulia,kukosa mafuta ya kula,kula unga ulioharibika kutoka NMC,kutembea bila Viatu,viraka na wakati mwingine makalio yanabaki wazi,sukari guru au miwa kutumika kwenye chai(vikiwepo),Uji wa chumvi,kukosekana kwa dawa muhimu(Nakumbuka dawa ya sikio ilikuwa mafuta ya Kuku),kutokupatikana kwa magodoro,(watu wakilalia magodoro ya makapi ya mbegu za pamba,au gunia zilizotiwa nyasi),kutokuwepo kwa dawa za mbu za kutosha kiasi kwamba watu walichoma magunia ili mbu wakimbie kwa ule moshi,kuwepo kwa kunguni sugu wengi,chawa kwa wingi ilikuwa kawaida sana,vifo vya wajawazito ilikuwa tishio mno...na mengine mengi.

Kusema kweli sitaki kuzikumbuka Siku hizo na nilikuwa naomba Mungu zisotokee tena katika uhai wangu.Ninatamani kizazi changu kipite,ili kama kuna watu wanakiburi cha kupambana na hao mnaowaita mabeberu,mpambane nao.

Vijana wengi wanaishi kwa ndoto tu.Wanaona maisha ya kwenye muvi wanadhani ndiyo uhalisia.Na sisi watu wazima,tukiwapotosha,tutajikuta tunawaangamiza sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom