Hillary Clinton akumbwa na Ugonjwa Ghafla

Hillary Clinton akumbwa na Ugonjwa Ghafla

Ethos

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2015
Posts
2,294
Reaction score
2,111
Mgombea wa kiti cha urais nchini Marekani kupitia chama cha Democratic Hillary Clinton amelazimika kuahirisha ziara yake ya kuchangisha fedha katika jimbo la California baada ya vipimo kuonyesha ana ugonjwa wa homa ya mapafu, baada ya kujisikia vibaya wakati alipohudhuria shughuli ya kumbukumbu ya mashambulizi ya septemba 11 na kuibua upya uvumi kuhusu afya yake wiki sita tu kabla ya uchaguzi mkuu.

Je, Hillary Clinton ataweza kuwa na nguvu ya kuendelea na kampeni za uchaguzi?

Source. DW swahili
 
Khaaa! eti Killery Clinton!
Vote For [HASHTAG]#DonaldJokerTrump[/HASHTAG] to [HASHTAG]#MakeAmericaGreatAgain[/HASHTAG]
 
Yale Yale ya EL vs JPM
 
Nimeiona hii incidence live kwenye BBC, mmmh tatizo la afya ya huyu mama inaweza kuwa zaidi ya pneumonia, maana wakati wa wanamwingiza kwenye gari alikuwa anatetemeka na akaanguka! Walinzi walijitahidi kuziba ili incidence isionekane vizuri lakini wapiga picha walipata part ya kilichotokea.
 
Nimeiona hii incidence live kwenye BBC, mmmh tatizo la afya ya huyu mama inaweza kuwa zaidi ya pneumonia, maana wakati wa wanamwingiza kwenye gari alikuwa anatetemeka na akaanguka! Walinzi walijitahidi kuziba ili incidence isionekane vizuri lakini wapiga picha walipata part ya kilichotokea.
sure pia anaonekana kama kukakamaa hivi hadi kiatu kikavulika
 
Clinton hana lolote ni kick tu za kisiasa, et! aonekane kuwa ameguswa na msiba wa 9/11 ili ajenge ushawishi kwa wapiga kura, unacheza na siasa wewe, siasa unaweza kujifanya hata umekufa ili wakupigie kura. Kwanza mama lenyewe jasusi kucheza ile muvi pale mbele ya majasusi wenzake na kujifanya kama ka paralysis na walinzi kumdaka. Sio mageni hayo katika siasa.

THINK BIG.
 
Clinton hana lolote ni kick tu za kisiasa, et! aonekane kuwa ameguswa na msiba wa 9/11 ili ajenge ushawishi kwa wapiga kura, unacheza na siasa wewe, siasa unaweza kujifanya hata umekufa ili wakupigie kura. Kwanza mama lenyewe jasusi kucheza ile muvi pale mbele ya majasusi wenzake na kujifanya kama ka paralysis na walinzi kumdaka. Sio mageni hayo katika siasa.

THINK BIG.
Kwani yeye siyo binadamu kuwa asiumwe?

Hata machofu yanaweza kumfanya akatakaka kuanguka, kampeni siyo mchezo katika umri wake (68)
 
Back
Top Bottom