Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,243
- 44,520
TANGAZO MUHIMU
=========
Kuna Video Clips za Mzee zimefanyiwa Slow Motion Kidogo zinasambazwa ili kupotosha watu waone Mzee anaumwa. Zipo kama tatu hivi ambazo nimekutana nazo. Naamini wengi wengi mmekutana nazo pia, Moja ile ya jogging ya Albino kule Temeke, Moja anakaa kwenye kiti ofisini Na nyingine anatembea, inawezekana zipo zingine ama zitakuja zingine tena. Video hizo mkikutana nazo msishiriki kuzisambaza, pili mzitolee maelezo Haya niliyowapa kwamba zimefanyiwa slow motion kidogo ili kupotosha mana kuna watu wanaamini tena na wengine ni kati yetu pia. Watu wanatakiwa walifahamu hilo kuwa zimefanyiwa slow motion kwa kiwango fulani.
==============
By Jacob Malihoja
Mshauri wa Siasa
Team Lowassa Makao Makuu
"Mtu mwenye akili akikuambia jambo la kipumbavu wakati anajua una akili, ukikubaliana nae anakudharau"- Mwl. Nyerere
Haya ni moja ya matumizi mabaya ya Mb zako Mzee Mwanakijiji.
Labda wengine mmeshaliona hili:
My Take: Sasa kama ni kweli wanafikiria hili au wanaamini hili basi bila ya shaka wanatufikiria sisi sote akili zetu ziko kwenye chupa. Hivi kweli video zote hizi zimewekwa slow motion? Seriously? Inawezekana Lowassa hana matatizo makubwa ya kiafya kama inavyohisiwa na baadhi ya watu lakini kusema kuwa video zimefojiwa ili kumfanya aonekane dhaifu zaidi nadhani si kutendea haki watu wengine. Kuna njia moja ya uhakika pkuondoa wasiwasi huu.
Umebakiza hatua moja tu ya kusema 'kila mtanzania ni fisadi.....tofauti ni kiwango cha ufisidi..." I love BongoKila mtanzania anaumwa...tofauti ni kiwango cha uuguaji, Lowassa hata kama anaumwa maradhi yake hayamfanyi asiwe Rais, Mbona kuna kiongozi mkubwa tu ana kifafa? na tulimchagua sisi wenyewe? hizi team za Urais sasa zitatupeleka pabaya sana.
Tatizo kubwa kwa sasa hivi kuna "vita".....na katika vita kitu cha kwanza "kuangamia" au "kuangamizwa" ni UKWELI. Inaweza kuwa vigumu sana kujua ukweli wa suala hili.
Hivi kama nchi hatuna sheria ya kuwataka wagombea kupata clean bill ya afya kabla ya kukubaliwa kugombea. Hii ingeweza kuondoa utata....wote wapimwe afya zao na wale ambao hawatimizi vigezo vya kiafya tunaweka pembeni.
Nilimsikia EL mwenyewe akitaka hili lifanyike....inawezekana kuna vitu anajua kuhusu wapinzani wake ambavyo sisi wengine hatuvijui?
Kila mtanzania anaumwa...tofauti ni kiwango cha uuguaji, Lowassa hata kama anaumwa maradhi yake hayamfanyi asiwe Rais, Mbona kuna kiongozi mkubwa tu ana kifafa? na tulimchagua sisi wenyewe? hizi team za Urais sasa zitatupeleka pabaya sana.
Ndio maana nikauliza kama tunayo sheria ili tuache kuongozwa na hisia.Kwenye sheria za kazi huu ubaguzi unaruhusiwa? Ni waathirika wangapi wa ukimwi wako makazini na hawajabaguliwa sembuse ugonjwa wa kutetemeka?