Hili suala la kipimo pekee cha COVID-19 kuwepo Dar peke yake ni changamoto kubwa sana. Inawezekana maambukizi yakawa mengi zaidi!

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,989
22,521
Wanajamvi, hili suala la vipimo vya Corona, hata Marekani wanapambana kuhakikisha vinapatikana nchi nzima kadri ya mahitaji. Trump yeye alilalamikiwa kwa kuzikataa zile walizotoa W.H.O hapo awali.

Lakini leo nimemsikia Waziri Mkuu (na juzi Ummy), akisema sample za wanaohisiwa kuwa na Virusi vya Corona zinachukuliwa hospital zilizoko maeneo ya karibu na airports kutoka kwa washukiwa, na kusafirishwa kwenda Dar kufanyiwa vipimo vya Corona. Mfano yule mama wa Arusha ilichukuwa siku tatu! Hatua zinazochukuliwa sasa hivi ni kama patapotea tu. Mara sijui guest house inafungwa na Dereva taxi na familia yake wanatafutwa, as if wako na bidhaa za wizi!

Sasa najiuliza upatikanaji wa vifaa vya kufanya vipimo hivyo ndo umeleta hii shida au ni sisi tulijiamulia kuwa kifaa kimoja tu kinatosha? Kwanini hatukuanza na kuhakikisha kila hospital aliyoitaja waziri mkuu inakuwa na uwezo huo?

Kwasababu nimeona kama vile serikali inakuwa reactive badala ya kuwa proactive. Yaani mpaka malalamiko yazidi ndo hatua inachukuliwa. Na sasa ile tabia ya kudharau ushauri unaotolewa pengine kutokana na itikadi zetu inatakiwa iachwe mara moja. Mfano kuhusu hoja nzuri tu ya Msigwa kule bungeni ya kutaka bunge lijadili suala la Corona ilipozimwa huku ile ya kutaka Zitto auawe ikipigiwa meza, makofi na vigelegele.

Kwa sasa hivi Europe wanataka kupiga kura ili kufunga mipaka yao. Mataifa haya makubwa lazima chumi zao zitayumba na wamejiandaa kwa hilo. Sisi hatuna ujanja zaidi ya kuchukua tahadhari ili tusipoteze maisha ya wananchi kizembe. Halafu tujiandae kwa changamoto ya kiuchumi.

Kitu kinachosababisha panic ni kuchelewa kuchukua hatua. Marekani panic imekuwa kubwa kiasi kwamba kuna wanaoamini ni mwisho wa dunia nk. Lakini cha msingi hapa, ni kwamba bidhaa nyingi muhimu hazipatikani tena kwenye supermarkets. Hata vyakula watu wamerundika nyumbani. Lakini wale tuliowacheka, bahati yetu itakuwa pale tu hili janga litakapoanza kupungua makali. Yaani kuwepo na sufuri kwenye ripoti ya wagonjwa na wale wanaopoteza maisha. Kwasababu ni wazi uzalishaji na upatikanaji wa baadhi ya bidhaa utapungua, na uwezekano wa serikali kulazimisha rationing. Hilo lilishawahi kutokea kwenye sukari.

Serikali itambuwe kwamba kuchukua hatua mapema kutasaidia siyo tu kuokoa maisha, bali pia na uchumi wetu. Nchi ya Italia ambao pia tunawategemea kwa utalii, wamefunga mipaka yao. Na wao pia wanajilaumu kwa kuchelewa kuchukua hatua. Sisi tulitakiwa tujifunze na siyo kuhisi kwamba tuko immune kwasababu ya hizo habari kwamba virusi hivyo haviishi kwa muda mrefu kwenye miale ya jua na joto kali. Hata kama ikiwa hilo ni kweli, bado kutakuwepo na uambukizaji, hapo kwa rate ya chini.

Nashauri serikali iongeze vifaa vya kupima Corona, na kila anayeingia kuzuiwa kwa siku 14 ndipo waruhusiwe hata kama wamepima na kukutwa hawana. Nilimsikia Mkuu wa Mkoa wa Arusha akiongelea kuwazuia walioko guest bila kutaja muda watakaowazuia. Ni vyema viongozi hao wakawa busy kujifunza kuhusu janga hili la dunia badala ya kuhangaika na upinzani.

Pia ni wakati wa kuwa activate vile vikosi vyetu vinavyoshughulika na majanga. Ni wakati wa kulinda Taifa na siyo chama fulani peke yake. Marekani wao wameanza kuwa deploy wale national guards. Hata mapolisi tunao wengi sana na wanatafuna kodi zetu tu wapewe kazi kwenye hili janga la Corona, mfano traffic police. Na pia JKT kutengeneza vitanda vya wagonjwa na pengine kambi nk.
 
Kama vifaa vya kupima vikiongezwa, tunaweza kukuta tuna idadi kubwa ya waathirika kuliko tunavyodhani. Ni bora viongezwe sasa kabla serikali haijazidiwa na wagonjwa. Na kwasasa hata huko ulaya na marekani wanapambana na hali zao. Hivyo ni muhimu kuongeza vifaa vya kupima na mikusanyiko yote piga marufuku kwa muda huku tathmini ya kirusi hiki ikiendelea nk. Inawezekana serikali ina wasiwasi kuhusu uchumi wetu, lakini kwa upande mwingine kuna wananchi ambao ni binadamu wanaotegemewa kwenye ujenzi wa uchumi wetu.
 
Nimeona uzio la kufunga shule, ligi kuu kusimama ila bado serikali haikutoa ufananuzi juu ya usafiri, night clubs, bars, hotels na nyumba za wageni.

Maana watu huenda kwenye hayo maeneo pia na hata huko mahoteli usafi wa malazi uzingatiwe na ikibidi mashuka yafuliwe na maji ya moto kisha kunyooshwa kabla ya mteja mwingine kutumia.

Kwenye daladala tamko la level seat liwekwe na lisimamiwe na vyombo vya usalama barabarani, night clubs zitiwe kufuli hii ikiambatana na matamasha ya wasanii.

Mikutano ya taasisi za kiserikali ama taasisi binafsi ipigwe marufuku. Ningependekeza vijana wa JKT wapewe mafunzo ya Corona na wawe tayari kwa usaidizi pale inapobidi.


Makanisa na misikiti vyote vifungwe na watu wafanye ibada wakiwa nyumbani tusije tukaleta mzaha.

Mwisho.
 
Ni mtu mpuuzi na mjinga Tu anayeweza kuogopa Corona , Kwa mda wa miez miwili Corona imeua watu 7000+ , at the same tyme malaria killed 84000 for February alone , huku ikiua watoto 3000 Kwa sku , bendera fata upepo taabu Sana ,
 
Ni mtu mpuuzi na mjinga Tu anayeweza kuogopa Corona , Kwa mda wa miez miwili Corona imeua watu 7000+ , at the same tyme malaria killed 84000 for February alone , huku ikiua watoto 3000 Kwa sku , bendera fata upepo taabu Sana ,
It’s a novel virus.
 
Nimeona uzio la kufunga shule, ligi kuu kusimama ila bado serikali haikutoa ufananuzi juu ya usafiri, night clubs, bars, hotels na nyumba za wageni.

Maana watu huenda kwenye hayo maeneo pia na hata huko mahoteli usafi wa malazi uzingatiwe na ikibidi mashuka yafuliwe na maji ya moto kisha kunyooshwa kabla ya mteja mwingine kutumia.

Kwenye daladala tamko la level seat liwekwe na lisimamiwe na vyombo vya usalama barabarani, night clubs zitiwe kufuli hii ikiambatana na matamasha ya wasanii.

Mikutano ya taasisi za kiserikali ama taasisi binafsi ipigwe marufuku. Ningependekeza vijana wa JKT wapewe mafunzo ya Corona na wawe tayari kwa usaidizi pale inapobidi.


Makanisa na misikiti vyote vifungwe na watu wafanye ibada wakiwa nyumbani tusije tukaleta mzaha.

Mwisho.
Nadhani wanasikilizia kwanza.
 
Wewe
Wanajamvi, hili suala la vipimo vya Corona, hata Marekani wanapambana kuhakikisha vinapatikana nchi nzima kadri ya mahitaji. Trump yeye alilalamikiwa kwa kuzikataa zile walizotoa W.H.O hapo awali.

Lakini leo nimemsikia Waziri Mkuu (na juzi Ummy), akisema sample za wanaohisiwa kuwa na Virusi vya Corona zinachukuliwa hospital zilizoko maeneo ya karibu na airports kutoka kwa washukiwa, na kusafirishwa kwenda Dar kufanyiwa vipimo vya Corona. Mfano yule mama wa Arusha ilichukuwa siku tatu! Hatua zinazochukuliwa sasa hivi ni kama patapotea tu. Mara sijui guest house inafungwa na Dereva taxi na familia yake wanatafutwa, as if wako na bidhaa za wizi!

Sasa najiuliza upatikanaji wa vifaa vya kufanya vipimo hivyo ndo umeleta hii shida au ni sisi tulijiamulia kuwa kifaa kimoja tu kinatosha? Kwanini hatukuanza na kuhakikisha kila hospital aliyoitaja waziri mkuu inakuwa na uwezo huo?

Kwasababu nimeona kama vile serikali inakuwa reactive badala ya kuwa proactive. Yaani mpaka malalamiko yazidi ndo hatua inachukuliwa. Na sasa ile tabia ya kudharau ushauri unaotolewa pengine kutokana na itikadi zetu inatakiwa iachwe mara moja. Mfano kuhusu hoja nzuri tu ya Msigwa kule bungeni ya kutaka wana siko suala la Corona ilipozimwa huku ile ya kutaka Zitto auawe ikipigiwa meza, makofi na vigelegele.

Kwa sasa hivi Europe wanataka kupiga kura ili kufunga mipaka yao. Mataifa haya makubwa lazima chumi zao zitayumba na wamejiandaa kwa hilo. Sisi hatuna ujanja zaidi ya kuchukua tahadhari ili tusipoteze maisha ya wananchi kizembe. Halafu tujiandae kwa changamoto ya kiuchumi.

Kitu kinachosababisha panic ni kuchelewa kuchukua hatua. Marekani panic imekuwa kubwa kiasi kwamba kuna wanaoamini ni mwisho wa dunia nk. Lakini cha msingi hapa, ni kwamba bidhaa nyingi muhimu hazipatikani tena kwenye supermarkets. Hata vyakula watu wamerundika nyumbani. Lakini wale tuliowacheka, bahati yetu itakuwa pale tu hili janga litakapoanza kupungua makali. Yaani kuwepo na sufuri kwenye ripoti ya wagonjwa na wale wanaopoteza maisha. Kwasababu ni wazi uzalishaji na upatikanaji wa baadhi ya bidhaa utapungua, na uwezekano wa serikali kulazimisha rationing. Hilo lilishawahi kutokea kwenye sukari.

Serikali itambuwe kwamba kuchukua hatua mapema kutasaidia siyo tu kuokoa maisha, bali pia na uchumi wetu. Nchi ya Italia ambao pia tunawategemea kwa utalii, wamefunga mipaka yao. Na wao pia wanajilaumu kwa kuchelewa kuchukua hatua. Sisi tulitakiwa tujifunze na siyo kuhisi kwamba tuko immune kwasababu ya hizo habari kwamba virusi hivyo haviishi kwa muda mrefu kwenye miale ya jua na joto kali. Hata kama ikiwa hilo ni kweli, bado kutakuwepo na uambukizaji, hapo kwa rate ya chini.

Nashauri serikali iongeze vifaa vya kupima Corona, na kila anayeingia kuzuiwa kwa siku 14 ndipo waruhusiwe hata kama wamepima na kukutwa hawana. Nilimsikia Mkuu wa Mkoa wa Arusha akiongelea kuwazuia walioko guest bila kutaja muda watakaowazuia. Ni vyema viongozi hao wakawa busy kujifunza kuhusu janga hili la dunia badala ya kuhangaika na upinzani.

Pia ni wakati wa kuwa activate vile vikosi vyetu vinavyoshughulika na majanga. Ni wakati wa kulinda Taifa na siyo chama fulani peke yake. Marekani wao wameanza kuwa deploy wale national guards. Hata mapolisi tunao wengi sana na wanatafuna kodi zetu tu wapewe kazi kwenye hili janga la Corona.
Wewe kipimo unakitaka cha nini, kwani huwezi kujigundua kwa dalili? Na ukaenda hospitali kupata dawa za kutibu hizo dalili
 
Mkuu Slowly wengi waliopimwa na kukutwa na pneumonie, na wengine kupoteza maisha yao, wengi wao wanawezekana wakawa na hivyo virusi. Sisi tumezoea magonjwa ndo maana. Kwani kuna takwimu gani? Kifaa cha kupimia chenyewe kiko sijui kwa mkemia mkuu. Na vipimo vinasafirishwa. Mr Slowly halafu bado unawasema wenzio kuwa ni bendera fuata upepo.
 
Wewe
Wewe kipimo unakitaka cha nini, kwani huwezi kujigundua kwa dalili? Na ukaenda hospitali kupata dawa za kutibu hizo dalili
Huwezi tu kwenda hospital kwasababu una dalili, labda uwekwe quarantined kwanza kwa siku 14 na vipimo vyako kuwa negative, ndipo uruhusiwe kuondoka.

Ukiwa na dalili siyo unarandaranda tu, kuna kitu kinaitwa “self quarantined”, ambapo sasa ndo unajifungia kwa siku 14 huko ndani kwako ukipambana na hizo dalili. Ndiyo maana mikusanyiko haitakiwi.
 
Hata chin
Mkuu Slowly wengi waliopimwa na kukutwa na pneumonie, na wengine kupoteza maisha yao, wengi wao wanawezekana wakawa na hivyo virusi. Sisi tumezoea magonjwa ndo maana. Kwani kuna takwimu gani? Kifaa cha kupimia chenyewe kiko sijui kwa mkemia mkuu. Na vipimo vinasafirishwa. Mr Slowly halafu bado unawasema wenzio kuwa ni bendera fuata upepo.
Hata China kwenyewe sio kila hospitali zina hicho kipimo acha uoga, jambo la msingi ukisha zungumzia dalili kimbia hospitali kupata dawa, acha uoga, ugonjwa unatibiwa kwa kutibu dalili.
 
Huwezi tu kwenda hospital kwasababu una dalili, labda uwekwe quarantined kwanza kwa siku 14 na vipimo vyako kuwa negative, ndipo uruhusiwe kuondoka.

Ukiwa na dalili siyo unarandaranda tu, kuna kitu kinaitwa “self quarantined”, ambapo sasa ndo unajifungia kwa siku 14 huko ndani kwako ukipambana na hizo dalili. Ndiyo maana mikusanyiko haitakiwi.
Sio kweli unacho kisema, unaongea kwa kutumia akili tu bila uzoefu, ndio maana wakaleta maski unavaa mask yako unakimbia hospital au pharmacy unachukua dawa zako unaendelea kujitibu.
 
Hata chin
Hata China kwenyewe sio kila hospitali zina hicho kipimo acha uoga, jambo la msingi ukisha zungumzia dalili kimbia hospitali kupata dawa, acha uoga, ugonjwa unatibiwa kwa kutibu dalili.
China waliwahi kwa isolation through self and authorized quarantines.

Watu wakiruhusiwa kurandaranda kama unavyotaka kutatokea shida kubwa zaidi.
 
It’s a novel virus.
Mimi wazo linaloniijia kichwani ni hili:

Unapoangalia picha ya vrus kama huyu, na hata wale wengine; kama wewe ni mwana sayansi, au binaadam mwenye akili ya kudadisi, ni kipi unachodhani unaweza kukibuni/kukivumbua kinachokaribiana na umbo la picha hiyo kikawa chenye manufaa makubwa kwa binaadam?

Ujue, hizo pembe (protrutions) zina kazi yake mhimu, na huko ndani ya duara lile kuna vitu mhimu pia.

Ningekuwa mwalimu sehemu fulani, ningetoa changamoto hii kwa vijana wenye akili zinazochemka, lakini wanaachwa tu waoze na akili zao vijiweni.
COSTECH - sijui huwa wanashughulikia vitu gani wao!

Hakuna kitu chochote kigumu dunia. Vumbuzi nyingi zimetokana na kugeza 'nature'

Najua nakutoa kwenye mstari wa mada yako, lakini nimeona bora nidandie hapo mkuu JMushi1
 

Attachments

  • corona.jpg
    corona.jpg
    89.3 KB · Views: 1
Wewe endelea kuwa mwoga tu, hakuna ugonjwa mbaya kama pressure, pata uzoefu kwa vijana wetu waliopo China maana wao mpaka leo wana survive
 
Wanajamvi, hili suala la vipimo vya Corona, hata Marekani wanapambana kuhakikisha vinapatikana nchi nzima kadri ya mahitaji. Trump yeye alilalamikiwa kwa kuzikataa zile walizotoa W.H.O hapo awali.

Lakini leo nimemsikia Waziri Mkuu (na juzi Ummy), akisema sample za wanaohisiwa kuwa na Virusi vya Corona zinachukuliwa hospital zilizoko maeneo ya karibu na airports kutoka kwa washukiwa, na kusafirishwa kwenda Dar kufanyiwa vipimo vya Corona. Mfano yule mama wa Arusha ilichukuwa siku tatu! Hatua zinazochukuliwa sasa hivi ni kama patapotea tu. Mara sijui guest house inafungwa na Dereva taxi na familia yake wanatafutwa, as if wako na bidhaa za wizi!

Sasa najiuliza upatikanaji wa vifaa vya kufanya vipimo hivyo ndo umeleta hii shida au ni sisi tulijiamulia kuwa kifaa kimoja tu kinatosha? Kwanini hatukuanza na kuhakikisha kila hospital aliyoitaja waziri mkuu inakuwa na uwezo huo?

Kwasababu nimeona kama vile serikali inakuwa reactive badala ya kuwa proactive. Yaani mpaka malalamiko yazidi ndo hatua inachukuliwa. Na sasa ile tabia ya kudharau ushauri unaotolewa pengine kutokana na itikadi zetu inatakiwa iachwe mara moja. Mfano kuhusu hoja nzuri tu ya Msigwa kule bungeni ya kutaka wana siko suala la Corona ilipozimwa huku ile ya kutaka Zitto auawe ikipigiwa meza, makofi na vigelegele.

Kwa sasa hivi Europe wanataka kupiga kura ili kufunga mipaka yao. Mataifa haya makubwa lazima chumi zao zitayumba na wamejiandaa kwa hilo. Sisi hatuna ujanja zaidi ya kuchukua tahadhari ili tusipoteze maisha ya wananchi kizembe. Halafu tujiandae kwa changamoto ya kiuchumi.

Kitu kinachosababisha panic ni kuchelewa kuchukua hatua. Marekani panic imekuwa kubwa kiasi kwamba kuna wanaoamini ni mwisho wa dunia nk. Lakini cha msingi hapa, ni kwamba bidhaa nyingi muhimu hazipatikani tena kwenye supermarkets. Hata vyakula watu wamerundika nyumbani. Lakini wale tuliowacheka, bahati yetu itakuwa pale tu hili janga litakapoanza kupungua makali. Yaani kuwepo na sufuri kwenye ripoti ya wagonjwa na wale wanaopoteza maisha. Kwasababu ni wazi uzalishaji na upatikanaji wa baadhi ya bidhaa utapungua, na uwezekano wa serikali kulazimisha rationing. Hilo lilishawahi kutokea kwenye sukari.

Serikali itambuwe kwamba kuchukua hatua mapema kutasaidia siyo tu kuokoa maisha, bali pia na uchumi wetu. Nchi ya Italia ambao pia tunawategemea kwa utalii, wamefunga mipaka yao. Na wao pia wanajilaumu kwa kuchelewa kuchukua hatua. Sisi tulitakiwa tujifunze na siyo kuhisi kwamba tuko immune kwasababu ya hizo habari kwamba virusi hivyo haviishi kwa muda mrefu kwenye miale ya jua na joto kali. Hata kama ikiwa hilo ni kweli, bado kutakuwepo na uambukizaji, hapo kwa rate ya chini.

Nashauri serikali iongeze vifaa vya kupima Corona, na kila anayeingia kuzuiwa kwa siku 14 ndipo waruhusiwe hata kama wamepima na kukutwa hawana. Nilimsikia Mkuu wa Mkoa wa Arusha akiongelea kuwazuia walioko guest bila kutaja muda watakaowazuia. Ni vyema viongozi hao wakawa busy kujifunza kuhusu janga hili la dunia badala ya kuhangaika na upinzani.

Pia ni wakati wa kuwa activate vile vikosi vyetu vinavyoshughulika na majanga. Ni wakati wa kulinda Taifa na siyo chama fulani peke yake. Marekani wao wameanza kuwa deploy wale national guards. Hata mapolisi tunao wengi sana na wanatafuna kodi zetu tu wapewe kazi kwenye hili janga la Corona.
Hivyo vifaa vya kupimia waombe msaada toka China sababu kule wenzutu wamesha fikia stage ya groupimmunity wagonjwa wanapungua kwa hiyo hawana uhitaji sana na wafanye haraka kabla wengine hawaja wa wahi.
 
Ni mtu mpuuzi na mjinga Tu anayeweza kuogopa Corona , Kwa mda wa miez miwili Corona imeua watu 7000+ , at the same tyme malaria killed 84000 for February alone , huku ikiua watoto 3000 Kwa sku , bendera fata upepo taabu Sana ,
Ngoja tusubiri mkuu bado ni ugonjwa mpya hapa Tz.
 
Sio kweli unacho kisema, unaongea kwa kutumia akili tu bila uzoefu, ndio maana wakaleta maski unavaa mask yako unakimbia hospital au pharmacy unachukua dawa zako unaendelea kujitibu.
Najaribu kuelewa ulichomjibu hapa mkuu jmushi1, nashindwa kukielewa.
Ni dawa gani unayopewa hospitali ya kujitibu?

China wamejenga hospitali nzima kwa wiki kadhaa kwa ajili ya wagonjwa wa aina hii, wewe unasema sio kweli na wala kweli yenyewe huiweki!

Maajabu ndio haya ya kujifanya ujuaji juu ya jambo ambalo hunalo ujuzi.

Analopendekeza mleta mada, lingekuwa jambo jema zaidi, lingerahisisha kazi na kupunguza mda kufanya vipimo hivyo kwenye hospitali maalum zilizo na wagonjwa hao.
Lakini inaeleweka uwezo wetu hauruhusu. Hii ingekuwa sababu tosha kabisa kujibu hoja yake.
 
Back
Top Bottom