Sheria ya Mafao ya kukosa ajira (Unemployment benefits) kwa sasa mwanachama anapata 33.3% ya msharaha wake. Ambayo yanalipwa kwa miezi sita tu. Baada ya hapo mfuko unakuchoka na kukuacha upambane na hali ngumu ya maisha.
Ukizingatia ugumu wa kupata ajira ilivyo, napendekeza yafuatayo:
1. Mifuko ya Taifa ya hifadhi iwe inalipa hiyo 33.3% kila mwezi hadi mwanachama atakapopata ajira. Pesa hiyo isikatwe kwenye michango ya mwanachama coz tunajua NSSF wanafanya biashara na kupata faida.
2. IKIWA Option ya kwanza inashindikana, basi mifuko iwape wanachama waliopoteza ajira au walioacha pesa yao yote wakapambane na maisha. Uzuri ni kwamba watanzania wengi ni wapambaji. Ukitaka kujua hilo angalia ni asilimia ngapi ya watanzania wameajiriwa na ngapi inajipambania tena bila msaada wa yeyote.
Hili ni ombi kwa rais kwani watunga sheria wao wamejipendelea tayari kwao maisha yanasonga
Ukizingatia ugumu wa kupata ajira ilivyo, napendekeza yafuatayo:
1. Mifuko ya Taifa ya hifadhi iwe inalipa hiyo 33.3% kila mwezi hadi mwanachama atakapopata ajira. Pesa hiyo isikatwe kwenye michango ya mwanachama coz tunajua NSSF wanafanya biashara na kupata faida.
2. IKIWA Option ya kwanza inashindikana, basi mifuko iwape wanachama waliopoteza ajira au walioacha pesa yao yote wakapambane na maisha. Uzuri ni kwamba watanzania wengi ni wapambaji. Ukitaka kujua hilo angalia ni asilimia ngapi ya watanzania wameajiriwa na ngapi inajipambania tena bila msaada wa yeyote.
Hili ni ombi kwa rais kwani watunga sheria wao wamejipendelea tayari kwao maisha yanasonga