Ndugu zangu, katika harakati za kutafuta mkate wa kila siku nimezunguka baadhi ya mikoa, ila ki ukweli hali inatisha na kusikitisha, juzi nilikua Arusha, mji umeharibika, maeneo karibu na soko kuu machinga wanapanga bidhaa mpaka barabarani, jana asubuhi nawahi stendi ili nisafiri kurudi kwenye makazi yangu, nimekuta mawe yamepangwa kando ya barabara kuonesha kuwa ni alama ya eneo la biashara la mhusika, narudia inasikitisha