Hili la Rais Magufuli kiprotokali limekaaje?

Hili la Rais Magufuli kiprotokali limekaaje?

Nimejaribi ku observe video za Mh. Rais Magufuli anapokutana na watu mbali mbali kama vile mabalozi huwa anatangulia yeye kunyoosha mkono na kusalimia.

Kwa ujuvi wangu mdogo naelewa kwamba kiprotokali mkuu wa nchi yeyote ile duniani anapotembelewa na viongozi wenzie hao wageni wake ndo huwa wanatoa mkono wa salamu kwanza na sio mwenyeji.

Wale wenye ujuvi kwenye masuala haya ya kidiplomasia na protokali mje mtusaidie hapa au huenda Mh. JPM ameathirika na adabu
a mafunzo ya heshima aliyoyapata kwenye makuzi yake ya utotoni usukumani?

Anyway nampa big up kwenye kutumbua majipu na kupanga serikali yake asisahau wakurugenzi wa halmashauri hawa ndo wanakula hela za miradi ya maendeleo ya wananchi bila shaka utumbuaji utawahusu tu.
umeuliza swali zuri sana na unaonyesha umesomea diplomasia. sasa analia majibu ya watu wasio na uelewa watakavyokuja. wataliweka kisiasa, matusi na mengin. protokali zinatakiwa kufuatwa wakati wote na zimewekwa kwa malengo maalum. hii ndio sababu huwa tunasema ni vyema viongozi wa siasi wakapitia vyuo vya diplomasia

nampongeza nape na wengine wengi waliosomea kozi za diplomasia. zinasaidia sana kuwatengeneza wanasiasa. unajua kuwa na ujuzi tu haitoshi, lazima ujifunze kutumia huo ujuazi au kipaji. mtu anaweza kuwa mwanasiasa mzuri lakini akipata maarifa ya diplomasia na akasoma kozi ya protokali inamfanya awe bora.

sijui njia sahihi ya kusalimiana kwa marais maana sijafikia kozi ya protokali ingawa najua kwenye kozi ya diplomasia, protokali ni sehemu yake
 
Hiyo ni power play. Magufuli anajiamini kwa hiyo haoni kwamba anakuwa intimidated.

Kwa anayekumbuka waziri mkuu wa Israel Rabin na Arafat walifanya press conference marekani. Wakati wanarudi ndani kukawa na kamchezo cha 'after you'. Mwisho wa siku Arafat alitangulia kuingia ikaonekana kama Rabin ana upper hand.
Na sio kujiamini yeye tuu kupeana mkono ni kumuamini pia unaempa mkono.
 
Nimejaribi ku observe video za Mh. Rais Magufuli anapokutana na watu mbali mbali kama vile mabalozi huwa anatangulia yeye kunyoosha mkono na kusalimia.
.

Ndio maana Magufuli kawapiga marufuku msisafiri nje bila kibali sababu mkisafiri mlikuwa mnaenda kujifunza mila za kizungu kama kusalimia kula na umma na vijiko,uvaaji masuti nk na jinsi ya protocol za kutongoza au kutongozwa na wazungu.Hicho ndicho mlichokuwa mkirudi nacho kwenye safari zenu.Kuvaa sio protocal wako viongozi waKIARABU HUJA NA makanzu na vilemba protocol hapo imeakaje? Wako viongozi wa Afrika magharibi huja na majoho ya vitenge na kofia za vitenge procol hapo imekaeje ya uvaaji? Wako AKINA mfalme Mswati wanakuja na ngozi zao shanga shingoni mabega nje na miguuni wamevaa makobasi hapo protocol ya uvaaji imekaaje? mAVAZI KWA kiongozi wa nchi ni hiari yake.

Lini ulimwona Nyerere kavaa suti kanyonga na tai?

Magufuli siku ingine akija Obama VAA YALE manguo ya kisukuma na makobasI AFRTER ALL UKO NCHINI KWAKO

Kuna matatizo na ulimbukeni hasa kwa baadhi ya watanzania.Wamelewa ukoloni mambo leo hadi basi.Ukimpeleka nje anakuwa kama mjinga fulani kila anachokiona nje ndio chenyewe.


Utamaduni halisi wa Mwafrika mtu mdogo huruhusiwi hata siku mmoja kumnyooshea mkono kwanza wewe kumsalimia mtu mzima.Mtu mkubwa ndiye akunyooshee kwanza mkono kukupa ndipo na wewe umpe mkono umsalimie.Mimi kitoto kikinisalimia halafu kikaninyooshea kunipa mkono kwanza naweza kukizabua makofi.

Hivi wewe unaweza kwenda kwa chifu kumsalimia wewe ndio ukaanza kumpa mkono au umekutana na raisi wewe unaweza kuthubutu kumpa mkono kwanza?

Raisi ni mtu mkubwa asiponyoosha mkono wake huwezi mnyooshea hilo ulijue.Hata bosi wako kazini kwako usije kujitia unanyoosha kikono chako kwanza kumsalimia.

Tatizo hivyo visafari vyenu koko mmeenda kujifunza ujinga zaidi mkasahau ya kwenu ya kiafrika
 
Nimejaribi ku observe video za Mh. Rais Magufuli anapokutana na watu mbali mbali kama vile mabalozi huwa anatangulia yeye kunyoosha mkono na kusalimia.

Kwa ujuvi wangu mdogo naelewa kwamba kiprotokali mkuu wa nchi yeyote ile duniani anapotembelewa na viongozi wenzie hao wageni wake ndo huwa wanatoa mkono wa salamu kwanza na sio mwenyeji.

Wale wenye ujuvi kwenye masuala haya ya kidiplomasia na protokali mje mtusaidie hapa au huenda Mh. JPM ameathirika na adabu
a mafunzo ya heshima aliyoyapata kwenye makuzi yake ya utotoni usukumani?

Anyway nampa big up kwenye kutumbua majipu na kupanga serikali yake asisahau wakurugenzi wa halmashauri hawa ndo wanakula hela za miradi ya maendeleo ya wananchi bila shaka utumbuaji utawahusu tu.

Neno ujuvi limetumika sivyo badala yake tumia neno Ujuzi.
 
Ni swali zuri na muhimu.

Kwenye diplomasia kuna mambo mengi, usalimiaji, uvaaji, ulaji, utembeaji, uongeaji n.k.

Nadhani wahusika watashughulikia
 
Ni swali zuri na muhimu.

Kwenye diplomasia kuna mambo mengi, usalimiaji, uvaaji, ulaji, utembeaji, uongeaji n.k.

Nadhani wahusika watashughulikia

Haya hebu mcheki Mfalme mSwati hapo akishuka kwenye ndege nchi za watu kiprotocol ya uvaaji wewe mtaalamu koko unasemaje hapo

images
 
umeuliza swali zuri sana na unaonyesha umesomea diplomasia. sasa analia majibu ya watu wasio na uelewa watakavyokuja. wataliweka kisiasa, matusi na mengin. protokali zinatakiwa kufuatwa wakati wote na zimewekwa kwa malengo maalum. hii ndio sababu huwa tunasema ni vyema viongozi wa siasi wakapitia vyuo vya diplomasia

nampongeza nape na wengine wengi waliosomea kozi za diplomasia. zinasaidia sana kuwatengeneza wanasiasa. unajua kuwa na ujuzi tu haitoshi, lazima ujifunze kutumia huo ujuazi au kipaji. mtu anaweza kuwa mwanasiasa mzuri lakini akipata maarifa ya diplomasia na akasoma kozi ya protokali inamfanya awe bora.

sijui njia sahihi ya kusalimiana kwa marais maana sijafikia kozi ya protokali ingawa najua kwenye kozi ya diplomasia, protokali ni sehemu yake



Haya msomi wa Diplomasia koko angalia mfalme Mswati akiwa India mcheki alivyovaa hivyo vi notisi vyako koko vya darasani vinasemaje kuhusu hili?

images
 
Zina nn mkuu...???unakumbuka jinsi wamarekani walivoreact kwa kitendo cha raisi wao kuonyesha ishara ya kumsujudu mfalme wa saudia...huyo ni rais wa nchi mkuu...sio CEO wa kampuni anapokea wawekezaji...ifike wakati rais awe rais kweli na sio rahisi hata kama ni rais wa taifa maskini...sasa kama kwa hao mabalozi tu anafanya hvo je akija rais wa Marekani hapa itakuweje...

In shortest and clearest its obvious kwamba akija mtu kama Obama hivi lazima mkuu wa walomweka pale atainama kama vile kumsujudu vile. Huu ni umasikini mkubwa wa roho na mmbaya sana kulinganisha na wakuu wa nchu nyingine, anapaswa kusafiri japo kidogo japo si mapenzi yake ili akawe upto dated kidogo.
 
Watu hupenda kuchukulia mambo kimzaha mzaha...china na japani kipindi flani walisimamisha mazungumzo kwasababu japani alitaka kutoa mkono kwanza baada ya kusaini makubaliano na baada ya china kukubali ombi la japan ndipo saini za makubaliano kuhusu kisiwa yalisainiawa...

Kila ishara, kitendo kinatoa meneno millioni kidogo kwa watu na taifa.... msichukulie mzaha tu... jiulizeni ni kwann raisi anavaa TAI NYEKUNDU NA SUTI NYEUSI katika baadhi ya shughuli zake?!?!
 
In shortest and clearest its obvious kwamba akija mtu kama Obama hivi lazima mkuu wa walomweka pale atainama kama vile kumsujudu vile. Huu ni umasikini mkubwa wa roho na mmbaya sana kulinganisha na wakuu wa nchu nyingine, anapaswa kusafiri japo kidogo japo si mapenzi yake ili akawe upto dated kidogo.


Mkuu tatizo letu watz ni kuchukulia mambo kirahisi rahisi tu...eti kwani inampunguzia nn...ndo maana hata maccm yamekuwa yanatutawala kirahisi rahisi tu...wametubemenda miaka nenda miaka rudi bado tunazidi kuyang'ang'ania tu...shame on us...
 
Zina nn mkuu...???unakumbuka jinsi wamarekani walivoreact kwa kitendo cha raisi wao kuonyesha ishara ya kumsujudu mfalme wa saudia...huyo ni rais wa nchi mkuu...sio CEO wa kampuni anapokea wawekezaji...ifike wakati rais awe rais kweli na sio rahisi hata kama ni rais wa taifa maskini...sasa kama kwa hao mabalozi tu anafanya hvo je akija rais wa Marekani hapa itakuweje...
Unafikiri atasalimia kwa magoti labda!..............hapna
 
S
Mkuu tatizo letu watz ni kuchukulia mambo kirahisi rahisi tu...eti kwani inampunguzia nn...ndo maana hata maccm yamekuwa yanatutawala kirahisi rahisi tu...wametubemenda miaka nenda miaka rudi bado tunazidi kuyang'ang'ania tu...shame on us...

Shame on them and NOT on all of us mkuu. baadhi tunajitambua sana kamanda
 
Ni hivi katika diplomasia salamu hutumika kulingana na mazingira nchi nyingi za afrika salamu zao ni kushikana mikono na protokali haikatazi rais kushikana mikono na mgeni no matter awe mdogo au mkubwa!hvyo basi hakuna protokali inayosema nan aanze kumpa mkono mwenzie ila kiafrika mwenyeji ndio anayetakiwa kuanza na kama umeona hata jinsi ya kukaa rais atamuelekeza mwenyeji sehemu ya kukaa then atakaa alafu atakaa na yeye rais!!
 
Nimejaribi ku observe video za Mh. Rais Magufuli anapokutana na watu mbali mbali kama vile mabalozi huwa anatangulia yeye kunyoosha mkono na kusalimia.

Kwa ujuvi wangu mdogo naelewa kwamba kiprotokali mkuu wa nchi yeyote ile duniani anapotembelewa na viongozi wenzie hao wageni wake ndo huwa wanatoa mkono wa salamu kwanza na sio mwenyeji.

Wale wenye ujuvi kwenye masuala haya ya kidiplomasia na protokali mje mtusaidie hapa au huenda Mh. JPM ameathirika na adabu
a mafunzo ya heshima aliyoyapata kwenye makuzi yake ya utotoni usukumani?

Anyway nampa big up kwenye kutumbua majipu na kupanga serikali yake asisahau wakurugenzi wa halmashauri hawa ndo wanakula hela za miradi ya maendeleo ya wananchi bila shaka utumbuaji utawahusu tu.
naona majaliwa ameanza kuwatumbua.
 
Unafikiri atasalimia kwa magoti labda!..............hapna

Ni vema angesalimia kwa kupiga magoti ili msaada izidi kumiminika mkuu wangu...si unajua tena bila msaada mambo hayaendi kabisa yaani..
 
Ni vema angesalimia kwa kupiga magoti ili msaada izidi kumiminika mkuu wangu...si unajua tena bila msaada mambo hayaendi kabisa yaani..
Bila kujali procol kuanza kumsalimia au kumpa mgeni mkono ni isharA ya ukarimu mengine nawaachia
 
Back
Top Bottom