lanez
Member
- Apr 18, 2019
- 78
- 163
Kwa tafsiri inayofahamika, taasisi ni chombo kinachofanya kazi kwa kushirikisha watu wengi, ili mambo yaende. Kutokana na kufanya kazi kitaasisi basi hupelekea ufanisi zaidi. kwenye somo la Principle management tunafundishwa umuhimu wa kufanya kazi kitaasisi ili kuongeza ufanisi.
Vyama vya siasa kama CCM ni taasisi , hivyo huitaji kuendeshwa kitaasisi na kutokumtegemea mtu ili taasisi isimame. Wote tunafahamu CCM ni taasisi kubwa, na yenye kila aina ya rasilimali watu na vitu toka kuanzishwa kwake. Lakini kwa miaka mitano ya utawala wa Mh Magufuli kama mwenyekiti wa CCM, CCM imekuwa hijiendeshi kitaasisi tena, bali hutegemea mtu mmoja tu, ambaye ni mwenyekiti wake Magufuli. Hili ni moja la kosa kubwa, alilolifanya Mh. Magufuli, kuigeuza taasisi kubwa kama CCM kumtegemea mtu mmoja.
Huu ni ushahidi, wa Mh Magufuli kuigeuza CCM kumtegemea mtu mmoja.
Toka aingie kwenye uongozi wake, mara nying Mh Magufuli amekuwa akijitaja "yeye" Na sio "Sisi " mfano
nitakuteua
Unaweza ukapita huku, lakini kule nikakukata
Nimemkata mtoto wa Dada yangu, nimemteua Gwajima.
Nimeamua kutengeneza vitambulisho mimi mwenyew
Sifanyi hiki nafanya hiki, sipangiwi n.k
Kwa wanaofatilia hotuba za Mh Magufuli, hizo kauili ni kawaida kuzisikia, kitu ambacho kimeleta madhara makubwa, ndani ya CCM. Unaweza ukajiuliza ni matatizo gani hayo, lakini kwa kawaida binadamu usipo wa "acknowledge " kwenye jambo ambalo mmefanya pamoja, huwa wanakuwa "disappointed "sana. Inawezekana wasiseme lakini moyoni wanaumia, hivyo kuendesha mgomo kisiri siri ili waone kama unaweza fika peke yako.
Madhara ya Mh Magufuli, kujijenga kama Taasisi ndani ya Taasisi, yalikuwa na madhara ya muda mrefu, pengine ilikuwa ngumu kuyakugundua kipindi kile, lakini kipindi hiki cha uchaguzi yameonekana wazi, yameonekanaje, basi fuatilia hapa chini.
kipindi hiki cha uchaguzi, ambacho Mh. Magufuli, amekili kuna maeneo hatofika pamoja na kupumzika sana kwa kampeni zake, tulitegemea basi katibu uenezi na katibu mkuu, kuendesha mikutano mikubwa mikoani chini ya mwamvuli wa wagombea ubunge. Kipindi cha Kikiwete ilikuwa kawaida kumuona nape na kinana wakifanya mkutano mkubwa mikoani bila hata uwepo wa Mh kikwete, hii ilitokana na CCM kuendeshwa kitaasisi.
Wagombea ubunge wengi wa CCM, mikutano yao imekuwa ya kinyonge mno huko mikoani na ndio maana hata hatuoni picha za wagombea ubunge CCM wakiwa wamejaza watu wengi. Hili pia limesababishwa na kumtegemea Mh Magufuli pekee.
mikutano ya mgombea Makam Rais na Waziri mkuu, bado haina hadhi ile ya CCM ya kipindi cha nyuma. Zaman ilikuwa inatosha kabisa mkutano wa mgombea urais, kinana, Nape na January makamba kutikisa mkoa mzima, lakini leo kinyonge mpaka Mh Magufuli awepo.
Mwisho, watu wamshauri Mh Magufuli airudishe CCM kujiendesha kitaasisi, aachane na maneno "CCM ya Magufuli" mara "serikali ya Magufuli " kwani akishinda Leo, ataisababishia ugumu CCM mwaka 2025. Hata Marehem Benjamin mkapa, aliwai kuonesha kuchukizwa, na kujimilikisha CCM na serikali kama anavyofanya Mh.
"Maendeleo hayana vyama "
Vyama vya siasa kama CCM ni taasisi , hivyo huitaji kuendeshwa kitaasisi na kutokumtegemea mtu ili taasisi isimame. Wote tunafahamu CCM ni taasisi kubwa, na yenye kila aina ya rasilimali watu na vitu toka kuanzishwa kwake. Lakini kwa miaka mitano ya utawala wa Mh Magufuli kama mwenyekiti wa CCM, CCM imekuwa hijiendeshi kitaasisi tena, bali hutegemea mtu mmoja tu, ambaye ni mwenyekiti wake Magufuli. Hili ni moja la kosa kubwa, alilolifanya Mh. Magufuli, kuigeuza taasisi kubwa kama CCM kumtegemea mtu mmoja.
Huu ni ushahidi, wa Mh Magufuli kuigeuza CCM kumtegemea mtu mmoja.
Toka aingie kwenye uongozi wake, mara nying Mh Magufuli amekuwa akijitaja "yeye" Na sio "Sisi " mfano
nitakuteua
Unaweza ukapita huku, lakini kule nikakukata
Nimemkata mtoto wa Dada yangu, nimemteua Gwajima.
Nimeamua kutengeneza vitambulisho mimi mwenyew
Sifanyi hiki nafanya hiki, sipangiwi n.k
Kwa wanaofatilia hotuba za Mh Magufuli, hizo kauili ni kawaida kuzisikia, kitu ambacho kimeleta madhara makubwa, ndani ya CCM. Unaweza ukajiuliza ni matatizo gani hayo, lakini kwa kawaida binadamu usipo wa "acknowledge " kwenye jambo ambalo mmefanya pamoja, huwa wanakuwa "disappointed "sana. Inawezekana wasiseme lakini moyoni wanaumia, hivyo kuendesha mgomo kisiri siri ili waone kama unaweza fika peke yako.
Madhara ya Mh Magufuli, kujijenga kama Taasisi ndani ya Taasisi, yalikuwa na madhara ya muda mrefu, pengine ilikuwa ngumu kuyakugundua kipindi kile, lakini kipindi hiki cha uchaguzi yameonekana wazi, yameonekanaje, basi fuatilia hapa chini.
kipindi hiki cha uchaguzi, ambacho Mh. Magufuli, amekili kuna maeneo hatofika pamoja na kupumzika sana kwa kampeni zake, tulitegemea basi katibu uenezi na katibu mkuu, kuendesha mikutano mikubwa mikoani chini ya mwamvuli wa wagombea ubunge. Kipindi cha Kikiwete ilikuwa kawaida kumuona nape na kinana wakifanya mkutano mkubwa mikoani bila hata uwepo wa Mh kikwete, hii ilitokana na CCM kuendeshwa kitaasisi.
Wagombea ubunge wengi wa CCM, mikutano yao imekuwa ya kinyonge mno huko mikoani na ndio maana hata hatuoni picha za wagombea ubunge CCM wakiwa wamejaza watu wengi. Hili pia limesababishwa na kumtegemea Mh Magufuli pekee.
mikutano ya mgombea Makam Rais na Waziri mkuu, bado haina hadhi ile ya CCM ya kipindi cha nyuma. Zaman ilikuwa inatosha kabisa mkutano wa mgombea urais, kinana, Nape na January makamba kutikisa mkoa mzima, lakini leo kinyonge mpaka Mh Magufuli awepo.
Mwisho, watu wamshauri Mh Magufuli airudishe CCM kujiendesha kitaasisi, aachane na maneno "CCM ya Magufuli" mara "serikali ya Magufuli " kwani akishinda Leo, ataisababishia ugumu CCM mwaka 2025. Hata Marehem Benjamin mkapa, aliwai kuonesha kuchukizwa, na kujimilikisha CCM na serikali kama anavyofanya Mh.
"Maendeleo hayana vyama "