Hili la kuchinja lisitugawe, Linazungumzika

Hili la kuchinja lisitugawe, Linazungumzika

scramble

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2012
Posts
1,593
Reaction score
257
Mwanzoni mwa wiki hii waziri wassira alikutana na viongozi wa dini za Kikiristu na Kiislamu mkoani mwanza. Lengo la kukutana kwao lilikua kujadili suala la kuchinja wanyama wanaouzwa katika bucha mkoani mwanza.

Kumekuwepo na tofauti kati ya Wakristu na Waislamu kuhusu suala la kuchinja. Kuna mchungaji alichinja mnyama katika shughuli ya nyumbani kwake huku akijua kuwa waislamu nao watahudhuria. Kutokana na imani ya dini ya kiislamu, muislamu haruhusiwi kula mnyama ambao haukuchinjwa na muislamu kwa dua na taratibu maalumu. Waislamu baada ya kula pale shughulini walibaini kuwa nyama ile ni ya mnyama ambao hakuchinjwa kwa mujibu wa mafunzo ya kiislamu. jambo hili liliwaudhi sana wakaja juu na kuliripoti serikalini.

Kwa upande wa viongozi wa kikristu waliona kama wananyimwa haki ya kuchinja. kwa nini walaumiwe kwa kuchinja mnyama? mbona wanadhalilishwa!? Wakajibu mapigo kuwa serikali imewabeba waislamu katika suala la kuchinja kwa miaka mingi licha ya katiba kusema kuwa serikali haina dini. Wakatamka kuwa kuanzia sasa wakristu nao wapewe fursa ya kuchinja machinjioni na kama inawezekana wawe na bucha zao. Wakakumbusha kuwa waislamu wamekua wakipata tozo (ushuru) kwenye kila ng'ombe au mbuzi anaechinjwa.

Baada ya mkuu wa mkoa kupelekewa suala hili, alitamka kuwa tumekua na utamaduni wa kuwatanguliza waislamu wachinje kwenye machinjiyo ya miji mbalimbali na hata kwenye shughuli mbalimbali. Aliomba huu utamaduni uendelee. Kauli hii ilizidisha petroli kwenye moto. Viongozi wa kikristu walipinga kauli ya mkuu wa mkoa. Hali ilizidi kuwa tata. Serikali ya mkoa ililazimika kuliwasilisha tatizo hili ikulu, dsm.

Serikali iliamua kumtuma waziri Wassira kwa lengo la kusuluhisha suala hili. aliomba utamaduni wa waislamu kuchinja uachwe uendelee. viongozi wa kikristu hawakuafiki sawia maneno ya wassira. Kikao kikamalizika bila ya muafaka wa pamoja!


Maoni yangu juu ya kadhia hii
Mimi siyo msemaji wa wakristu au waislamu. Vilevile siyo msomi bobezi wa biblia au qurani. Naona kuwa suala hili likitapakaa katika mikoa mingine litaibua mambo mengi sana. Nahofia tanzania inaweza kuwa kama Nigeria! Kwa waislamu kuchinja ni suala la ibada. Kwa wakristu ningeomba itolewe mistari inayoelezea zoezi la kuchinja na yachunguzwe yafuatayo;

1- Je, kuchinja kumewekea masharti katika biblia? Kama yapo ni yepi?
2- Je, mkristu amezuiwa kula mnyama aliechinjwa na mtu asiye wa imani yake? Kama mistari ipo iwekwe wazi.

Kama itabainika kuwa kuna zuio la mkristu kula mnyama aliechinjwa na asie mkristu, basi moja kwa moja machinjioni awepo mkristu atakae chinja wanyama kwa ajili ya wakristu. ibada ya mtu isipuuzwe. Kama kwenye biblia hakuna msisitizo kuhusu kula nyama ya mnyama ambae hakuchinja na mkristu, basi nashauri tuendelee na utamaduni tulio nao kwa sasa wa waislamu kuwa wachinjaji.


Nini hatari ya jambo hili?
Kwanza nitamke kuwa kama biblia inaelekeza wakristu wasile nyama ya mnyama ambae alichinjwa na asie mkristu, bila shaka agizo la biblia liheshimiwe. Lazima iwe hivyo. Kama jambo hili halijawekewa msisitizo katika biblia, basi tuliache liendelee kama lilivyo. Sizuii kugawana maeneo ya kuchinjia lkn lina athari zifuatazo;

1- Kutakua na bucha za waislamu na za wakristu.
2- Mgawanyiko huu unaweza kutupeleka kwenye kuwa na maduka, daladala nk..... maalumu kwa waislamu na wakristu.

Tukifika huko hali itakua tete sana!

Nchi yetu inanyemelewa na udini kwa sasa. ni bomu ambalo likipasuka litatupeleka pabaya sana. Sisi vijana tumekua na ubaguzi wa kidini tofauti na wazee wetu ambao waliishi kama ndugu licha ya tofauti zao za kiimani. Tuheshimu na kuthamini umoja tulionao na tusithubutu kuuvuruga!

Naomba watakaojadili uzi huu watangulize imani ya dini (siyo udini. udini ni kuficha ukweli, kubagua, kushabikia, kukandamiza haki, ........ kwa lengo la kuunga mkono dini husika). Walio na mistari ya vitabu vyetu vya dini wanaweza kutuelimisha pia.


nimeandika kwa nia njema. pale nilipo teleza ni udhaifu wa kibinadamu

nawasilisha!
 
Mkuu mie naona utaratibu wa kuchinja waachiwe waislam kama ilivyokuwa, sio vbaya wao wakawa wachinji wa nchi hii!
 
wakakumbusha kuwa waislamu wamekua wakipata tozo (ushuru) kwenye kila ng'ombe au mbuzi anaechinjwa.


Kutokana na ukosefu wa ajira, wakristo nao wanataka nao wajiajiri kwenye uchinjaji. Kama kusingekuwa na posho anayopewa mchinjaji isingekuwa tabu. Pia Mbona wanakataa kuchinja kitimoto?
 
Mimi sio msomaji wa bible lakini nakuhakikishia kitabu kikubwa kama kile kitakuwa na vifungu vinavyoweza kutafsiriwa kuwa vinakataza kula nyama iliyochinjwa kwa kutamkiwa maneno ambayo kwa wakristo hayaeleweki. Sheria za kwenye vitabu vya Mungu haziko black and white nyingi ziko katikati ni kazi ya waumini kutafsiri. Wasabato wakitumia the same bible hawali kitimoto wakati wenzao wanatandika kama kawaida.
 
Nakubaliana na mtoa mada, uelewa wangu kuhusu uchinjaji kwenye bible nimewahi kukutana na mistari inayozuia kula nyamafu na damu, na eneo lingine inakataza kula nyama iliyotolewa kwa ibada za sanamu.

Binafsi, waislam wangeendelea kuchinja (Lakini isiwe kisheria) tufanye hivi kwa ajili yetu wanajamii na sio serikali wala chama.

Kutenga mabucha ya kikristo na kiislam kutaufanya ubaguzi huu uende mbali zaidi ya hapa. Familia zetu wengine tumejaliwa kuishi watu wa dini mbili tofauti, tutakua tunanunua nyama kwenye mabucha mawili?

Tunapokuwa na sherehe/misiba tuamue ni watu gani waje na wale chakula kilichoandaliwa? Hii haiendelezi chuku na undugu tulioudumisha kwa muda mrefu licha ya tofauti zetu za kidini?
 
Haya ni matunda ya chokochoko tulizozilea 2010. Nashindwa kuwaelewa viongozi wazima na akili zao wanakaa na kujadili upuuzi kama huu. Hebu tutafakari yafuatayo; Je ni ustaarabu kuchinja kitimoto au kibudu au mnyama aliyenyongwa au hata mbwa nyumbani kwako huku ukijua kuwa miongoni mwa watakaokula, wapo ambao kwa imani au utamaduni wao huwa hawali hicho chakula.
 
Kutokana na ukosefu wa ajira, wakristo nao wanataka nao wajiajiri kwenye uchinjaji. Kama kusingekuwa na posho anayopewa mchinjaji isingekuwa tabu. Pia Mbona wanakataa kuchinja kitimoto?

Tukiuendekeza umaskini wetu, tutadai kila aina ya upuuzi.
 
Naomba nitamke wazi kwamba mimi ni mkristu. Ni kweli kwamba inatakiwa kuheshimiana kwa kuangalia ni nani anaathirika vipi kuhusu nini? Naunga mkono kwamba utamaduni huu tuliouzoea wa huyu Muislam kuchinja kwa ajili ya jumuia ukaendelea kwa kuwa yeye kuchinja ni ibada. Lakini swali linalokuja hapo je, kuna maana ya ibada ambayo inajulikana kwa wananchi wote? na kama ipo je kufanya kazi ya kuajiriwa ni ibada kiasi cha kupanga mpaka tozo kwa kazi hiyo? Kama kuhiji ni sehjemu ya ibada wanapata kiasi gani kila mmoja anapoenda Mecca? Kwa mtazamo wangu binadamu ameumbwa na MUNGU ili aitawale dunia imeletwa dini ili imsaidie kuitawala dunia kwa matakwa ya MUNGU, hivyo binadamu ni bora zaidi kuliko dini. Kuishi kwa amani na upendo ni bora kuliko kuwa na dini tulizoletewa na Waarabu na Wazungu bila kuchunguza.
 
Mwanzoni mwa wiki hii waziri wassira alikutana na viongozi wa dini za Kikiristu na Kiislamu mkoani mwanza. Lengo la kukutana kwao lilikua kujadili suala la kuchinja wanyama wanaouzwa katika bucha mkoani mwanza. kumekuepo na tofauti kati ya Wakristu na Waislamu kuhusu suala la kuchinja. Kuna mchungaji alichinja mnyama katika shughuli ya nyumbani kwake huku akijua kuwa waislamu nao watahudhuria. kutokana na imani ya dini ya kiislamu, muislamu haruhusiwi kula mnyama ambao haukuchinjwa na muislamu kwa dua na taratibu maalumu. waislamu baada ya kula pale shughulini walibaini kuwa nyama ile ni ya mnyama ambao hakuchinjwa kwa mujibu wa mafunzo ya kiislamu. jambo hili liliwaudhi sana wakaja juu na kuliripoti serikalini.

kwa upande wa viongozi wa kikristu waliona kama wananyimwa haki ya kuchinja. kwa nini walaumiwe kwa kuchinja mnyama? mbona wanadhalilishwa!? wakajibu mapigo kuwa serikali imewabeba waislamu katika suala la kuchinja kwa miaka mingi licha ya katiba kusema kuwa serikali haina dini. wakatamka kuwa kuanzia sasa wakristu nao wapewe fursa ya kuchinja machinjioni na kama inawezekana wawe na bucha zao. wakakumbusha kuwa waislamu wamekua wakipata tozo (ushuru) kwenye kila ng'ombe au mbuzi anaechinjwa.

baada ya mkuu wa mkoa kupelekewa suala hili, alitamka kuwa tumekua na utamaduni wa kuwatanguliza waislamu wachinje kwenye machinjiyo ya miji mbalimbali na hata kwenye shughuli mbalimbali. aliomba huu utamaduni uendelee. kauli hii ilizidisha petroli kwenye moto. viongozi wa kikristu walipinga kauli ya mkuu wa mkoa. hali ilizidi kuwa tata. serikali ya mkoa ililazimika kuliwasilisha tatizo hili ikulu, dsm.

serikali iliamua kumtuma waziri wassira kwa lengo la kusuluhisha suala hili. aliomba utamaduni wa waislamu kuchinja uachwe uendelee. viongozi wa kikristu hawakuafiki sawia maneno ya wassira. kikao kikamalizika bila ya muafaka wa pamoja!


Maoni yangu juu ya kadhia hii
mimi siyo msemaji wa wakristu au waislamu. vilevile siyo msomi bobezi wa biblia au qurani. naona kuwa suala hili likitapakaa katika mikoa mingine litaibua mambo mengi sana. nahofia tanzania inaweza kuwa kama nigeria! kwa waislamu kuchinja ni suala la ibada. kwa wakristu ningeomba itolewe mistari inayo elezea zoezi la kuchinja na yachunguzwe yafuatayo;

1- Je kuchinja kumewekea masharti katika biblia? kama yapo ni yepi?
2- Je mkristu amezuiwa kula mnyama aliechinjwa na mtu asiye wa imani yake? kama mistari ipo iwekwe wazi.

kama itabainika kuwa kuna zuio la mkristu kula mnyama aliechinjwa na asie mkristu, basi moja kwa moja machinjioni awepo mkristu atakae chinja wanyama kwa ajili ya wakristu. ibada ya mtu isipuuzwe. kama kwenye biblia hakuna msisitizo kuhusu kula nyama ya mnyama ambae hakuchinja na mkristu, basi nashauri tuendelee na utamaduni tulio nao kwa sasa wa waislamu kuwa wachinjaji.


Nini hatari ya jambo hili?
kwanza nitamke kuwa kama biblia inaelekeza wakristu wasile nyama ya mnyama ambae alichinjwa na asie mkristu, bila shaka agizo la biblia liheshimiwe. lazima iwe hivyo. kama jambo hili halijawekewa msisitizo katika biblia, basi tuliache liendelee kama lilivyo. sizuii kugawana maeneo ya kuchinjia lkn lina athari zifuatazo;

1- kutakua na bucha za waislamu na za wakristu.
2- mgawanyiko huu unaweza kutupeleka kwenye kuwa na maduka, daladala nk..... maalumu kwa waislamu na wakristu.

tukifika huko hali itakua tete sana!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!


nchi yetu inanyemelewa na udini kwa sasa. ni bomu ambalo likipasuka litatupeleka pabaya sana. sisi vijana tumekua na ubaguzi wa kidini tofauti na wazee wetu ambao waliishi kama ndugu licha ya tofauti zao za kiimani. tuheshimu na kuthamini umoja tulionao na tusithubutu kuuvuruga!


naomba watakao jadili uzi huu watangulize imani ya dini (siyo udini. udini ni kuficha ukweli, kubagua, kushabikia, kukandamiza haki, ........ kwa lengo la kuunga mkono dini husika). walio na mistari ya vitabu vyetu vya dini wanaweza kutuelimisha pia.


nimeandika kwa nia njema. pale nilipo teleza ni udhaifu wa kibinadamu

nawasilisha!


Wakristo ni wastaarabu, hatutaki vita, hatutaki kunyang'anyana na waislamu haki ya kuchinja. Tuwaachie wachinje kila siku kila mahali, na Nguruwe wachinje, sio kuchagua wanyama baadhi, kama wanaona suala la nguruwe lipo kinyume kiitikadi waache kuingilia masuala ya itikadi zingine. Suala linalofanya nyama iwe halali ni kisu, au imani au nia ya mchinjaji, au mahitaji ya kuchinja. Watanzania hata hili tunajadili kweli jamani!
 
Mabucha ya waislamu kila slku nyama zitakuwa zinalala kwani wao mara nyingi husubiri siku za sikukuu ndo wale nyama.
 
Hoja ya kuchinja haina mshiko. Haikuhitaji hata Diwani,seuse Waziri kuimaliza. Nchi yetu si ya kidini. Kila mtu anaabudu kivyake,anachinja wanyama wake na kula vyake. Hatuingiliani. Tusilazimishane kusoma Biblia au Msahafu kutafuta wapi nani ameruhusiwa au kukatazwa kuchinja. Tusifike huko. Chinja upendavyo kwa imani yako..
 
Nadhani hoja sio kuchinja kwa ajili ya matumizi binafsi bali ni kwa ajili ya public
 
Matumizi yoyote Mkuu asilazimishwe mtu. Hutaki unaacha. Mbona karibu nyama ya mabucha yote Kibaha huchinjwa na wamasai ambao karibu wote ni wakristo?
Halafu kitu kidogo kama hiki kinashikiliwa bango na serikali pamoja na matumizi makubwa ya kodi yetu kukifuatilia as if hakuna vitu vingine vya maana kushughulikia
 
Back
Top Bottom