Hili jambo limeniumiza sana

Hili jambo limeniumiza sana

Wapo baadhi ya wazazi wasiojitambua huelekeza mapenzi yao kwa mtoto mmoja kati ya wengi aliozaa bila kificho, na wakati mwingine huonyesha chuki kwa mtoto mmoja kati ya wengi aliozaa bila kificho.
Cha ajabu, mtoto anaependwa na mzazi kisha akajua yeye anapendwa sana huwa hawanaga mwisho wa kupendeza. Na pale inapotokea mtoto asiyependwa kuja kupata mafanikio, hujikuta hakumbuki nyumbani kwao kwa lolote. Jamii inayomzunguka humuona wa ajabu sana kwa kutokumbuka kwao. Jamii inachopaswa kuelewa ni kuwa mapenzi ya mzazi na mtoto hujengwa katika kile kipindi ambacho mtoto ni tegemezi, akivuka hapo bila kuwa na mapenzi nawe, imekula kwako, uwe mzazi au mlezi.
Kinachobaki ni huruma ya mtoto ya kuzaliwa.
 
huwezi kujua kwa nini Mungu kakuacha wewe uishi mbele ya macho yake asiyekupenda. Hakika nakuambia kuna jambo umeandaliwa mbele yake ili ajifunze. Nakuomba cha kwanza amini kuwa Mungu ni mkubwa kuliko mama, pili muheshimu mzazi wako kwani anajua wewe ulivyo kuanzia a to z, (vitabu vya dini vinasema) ndio aliyekuzaa na wengi wanakuambia ndo mungu wa pili kwa sababu anakujua kuliko hata mpenzi wako. Tatu unapotoa msamaha kamili toka moyoni, ndipo Mungu atatimiza anachotaka kukupa/kukufanyia
BELIEVE ME, DO THAT
 
watu wengine sijui mkoje! ulichoandika ni upumbavu mtupu! na unakeraa, kama ni kweli alikuomba msamaha halafu wewe ukajifanya eti umeumia sana kwa yaliopita, jua mama sio kama mwalimu" mtafute muombe msamaha mama yako! ningekuwa ndo mjomba wako ningekupiga marufuku kufika kwangu mpaka mamaako akuridhie. eti HILI JAMBO LIMENIUMIZA SANA! mangapi we uliomuumiza mamaako!? kama una akili weka mabaya ya mamaako aliokufanyia na mazuri aliokufanyia kwenye mizani sahihi, yapi yanazidi! kitendo cha mamaako kukuomba msamaha haitakiwi uendelee kumsikiliza bali ni kumzuia na badala yake wewe ndo umuombe msamaha yeye! baraka zinkufuata ulipo unazipiga teke!?
Heeee amuombe msamaha kwa kuacha kufa badala ya mdogo wake




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona jambo dogo dada, hii inamaanisha tangu uwe na mpenzi ambaye mama yako hakumpenda inamaanisha huenda alikushauri ukakata kimsikiliza si unajua mapenzi! Kutoka hapa akawa na kinyongo, ukichanganya na physchological disturbance ya kuondokewa na ndugu yako ambaye ameondoka wakati mama yako ana kinyongo na wewe= bora ungekufa wewe! Lakini kwa kuwa mlikuwa wawili Lea mama yako hadi mwisho wako au wake! Nafsi INA tabia ya kubadilika hivyo wewe kuwa kawaida tu wala usimnunie mama yako sio mke mwenza huyo, atarudisha mapenzi mema kwako usijali! Ila na wewe una makosa makubwa kuliko mama yako kitendo cha kukaa kimya wakati mama yako anakuomba msamaha! Wakati huo wewe ulikuwa na akili timamu wakati wa kutenda kosa lakini yeye hakuwa na akili timamu wakati anatenda kosa lake! Ulikuwa ni wakati mzuri wa kujenga mapenzi ya kweli katika familia yenu! Muenyeshe mungu wako wa duniani kuwa huna kinyongo nae, mama ata akisema wewe ufe haina tabu wewe na Mali yako ni Mali yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Samehe wahenga wanasema wazazi hawakosei
Yamenitokea kama hayo najua unayopitia samehe ili Uishi kwa Amani
 
Habari zenu jamani


Katika familia yangu tumezaliwa wawili Mimi nikiwa ndiye mtoto wa kwanza alafu akafwata midogo wangu ambaye tayari ni marehemu mwezi sasa umepita.....nimebaki Mimi na mama yangu baba alishafariki miaka imepita.

Kabla ya mdogo wangu kufariki alikuwa ni kipenzi cha mama sana hilo halikuwa linanisumbua niliona kawaida sana pia hiyo ilitokana na mahusiano ya mpenzi niliekuwa nae mama hakumpenda sana jambo hilo lilifanya Mimi na mama yangu tusiwe na maelewano.
Kitu kilichokuja kuniumiza na nimuone mama tofauti ni siku mdogo wangu alipofariki mama alikuwa akilia wa nguvu na huku akilitaja jina la mdogo wangu na Mimi.......nanukuu( BORA USINGEONDOKA WW KIPENZI CHANGU ANGEONDOKA DADA YAKO (yani mimi)INGEKUWA AFADHARI.
Maneno hayo halikuwa akiyarudia kuanzia mwanzo wa msiba mpaka anazikwa jambo hili liliwashangaza wengi na liliniumiza sana mpaka Leo nikikumbuka Yale roho inaniuma sana nashindwa hata kumuangalia mama yangu naishia kulia.
Pengine nimemkosea mama yangu sana lkn sikutegemea kama anaweza kuombea Mimi kufa imeniumiza sana.
Amekuja leo na baadh ya ndugu akiomba msamaha sijasema chochote nimeishia kulia.nataman niende mbali kwasababu nimejua Mimi si chochote kwake.





Mwenye ushauri au mawazo yoyote kisaikolojia siko sawa.
Pole sana.....kama kaja kuomba msamaha inawezekana katambua wapi kakosea.....kaa uongee naye vizuri mjue wapi mlitofautiana na jinsi gani mtarudisha mahusiano ya mama na mtoto.

Sent from my Compaq desktop-1997 Using Jamiiforums desktop app
 
Mama ni Mungu wa Pili katika dunia hii. Hakuna kitu kibaya kama kumchukia Mama. Unachopaswa kufahamu kuwa hakuna mwanadanu aliyekamilika. Hivyo uambie moyo wako kuwa huyu ni mama yangu na vyovyote itakavyokuwa atabaki kuwa mama yangu. The rest mwachie Mungu. Hata kama utaamua kumchukia haitasaidia. Nakusihi mlipe kwa wema hadi ajue kama wewe unampenda hata kama yeye hakupendi. Ukifanya hivyo Mungu ipo siku atakufanyia wepesi katika mambo yako na familia yako kwa ujumla.

Wahenga walisema: mpe mchawi akulelee mwanao...
Ahsante sana ubarikiwe
 
Mama yako amekukosea sana..Hata kama mlikua hamuelewani sio sababu ya kuongea maneno hayo wakati wa kipindi kigumu kama hicho. Wewe msamehe tu na Mungu atakusahaulisha yote
Shukran nitajitahidi kufanya hivo japo imekuwa ngumu kwangu sana
 
Pole sana mkuu..jitahidi kuifuta hiyo kumbukumbu kichwani (japo ni ngumu; angalau kidogokidogo) na umsamehe Mama yako...

Pia jaribu kutafuta mtaalam wa Saikolojia akusaidie
Kweli nitafanya hivo kisikolojia siko sawa kabisa
 
Back
Top Bottom