Pelekaroho
JF-Expert Member
- Sep 15, 2010
- 1,599
- 368
Zamani tulikuwa na jeshi letu la kujenga Taifa ambalo lilisifika saana kwa kulima mahindi kwa wingi, sikuhizi jeshi letu linasifika kwa kupiga raia wasokuwa hatia.Ni sahihi sana, Jeshi la Ujerumani linamiliki night clubs, Jeshi la Croatia linasifika kwa kutengeneza juice ya passion, Jeshi la Canada limepata umaarufu mkubwa sana kwa kutengeneza vitafunio na tambi za paketi. Sioni tatizo kwa jeshi letu kufanya ujasiriamali, muhimu ni kuangalia kusiwe na mgongano wa kimaslahi na usalama wa wananchi.