Hii tabia tuache jamani, 'ni kabila gani'?

Hii tabia tuache jamani, 'ni kabila gani'?

Quinton Canosa

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2012
Posts
1,228
Reaction score
1,264
Habari za mchana wanajamvi,

Kuna hiki kitu binafsi mimi sikipendi japo bado kimekuwa kigumu kutoka kwenye baadhi ya vichwa vya watu.Wiki moja iliyopita jamaa yangu ambaye ni mwenyeji wa mkoa wa Mbeya alitembelewa na binti nyumbani kwao,jamaa akaona isiwe shida ikabidi amtambulishe kwa wanafamilia kama mchumba wake mtarajiwa,cha ajabu baadhi ya ndugu wa mwanaume wakauliza huyo msichana ni kabila gani, jamaa akawajibu ni mchaga wa machame, basi wote wakakaa kimya.

Yule binti alipoondoka tu maneno yakaanza mara oooh ndugu yetu sisi hatutaki uoe mwanamke kutoka uchagani aidha machame,au mpare na makabila yote ya mkoa wa Kilimanjaro,ukawa mjadala mrefu jamaa akaanza kubishana kwamba anaoa anayejisikia yeye ukawa ugomvi mkubwa sana na ndugu wa mwanaume wakaanza wakamwambia likimpata la kumpata asiwashirikishe kwani wao wanajua tabia za makabila haya.

Jamani hii tabia itaisha lini kwani makabila haya yana nini kibaya mpaka kunakuwa na ubaguzi wa aina hii.

Maoni yenu wakuu
 
hata mm nishawah kusikia kutoka kwa jamaa yang moja mpare. Kuwa hawa watu wapo after money sana hawana true love hata kidogo. Kwamba ukiwa na mafanikio anaweza kukua ili arithi hiyo mali. Ngoja aje miss chaga atakupa ins and outs of this issue
 
Sijui kwanini watu wengine wanakua hivi,ingekua issue ya dini ningeelewa lakini kabila sio issue manake kila mtu na Tabia yake na malezi yake,wengine Sio wachaga lakini wanatabia chafu kuliko ...........
 
Bahati mbaya jamii zetu na hata waoaji au waolewaji bado wana uelewa finyu kuhusu ndoa.....

Ndoa ni muunganiko wa watu wawili waliopendana na wakaamua kuishi pamoja....kama mwili mmoja....hapo haisemwi kama ni makabila gani na wala ni watu wa asili gani bali kinachoongelewa ni watu wawili waliopendana kwa kuwa mapenzi hayana mipaka.....
Na vile vile suala la mtu kuoa au kuolewa ni suala binafsi...nikiwa na maana linamhusisha mtu mmoja yeye kama yeye....kitendo cha kumuingilia mtu kwenye maamuzi yake yanayohusu ndoa ni sawa na kitendo cha kuyaingilia maisha ya mtu ingawaje kushauriana na mambo ya kawaida hakuna mkamilifu...lakini ushauri wako usiwe kwa shunikizo la yeye achukue maamuzi......

Kumbuka mtu anayeolewa au kuowa ni wewe na kama ni karaha na raha za ndoa utazipata wewe....changamoto zote za maisha ya ndoa utakumbana nazo wewe.....kwa hiyo kama wewe ndiye muhusika mkuu wa hili swala kwanini watu wengine wakufanyie maamuzi ya wewe kuingia kwenye ndoa....!!!???

Vile vile suala la watu kujadili makabila ni moja kati ya masuala yanayoonyesha ni jinsi gani jamii zetu zilivyo mbali na ustaarabu....
Kwa kawaida ubaya...umalaya, wizi na uchafu mwingine wowote hauna sehemu husika bali ni tabia tu mtu aliyoichukua kutoka kwenye jamii iliyomzunguka.....ni kama vile wadada wa kihaya walivyoamua kuuza miili yao ilihali kuna wadada wengi wa kihaya wenye tabia nzuri na wametulia kwenye ndoa zao....tusimuhukumu mtu kwa kabila lake wala kwa mahali alipotoka wala kwa historia yake bali mtu ahukumiwe kwa matendo kama ambavyo mwingine angeyafanya matendo hayo......

MAISHA NI YAKO , CHAGUO NI LAKO......
 
jamaa yako ni kabila gani kwanza??? hao waliojaji ukabila ndo jibu tosha usituumize vichwa kutafakari makabila mengine yenye ukabila wakati lipo hapo unalo.
 
Bahati mbaya jamii zetu na hata waoaji au waolewaji bado wana uelewa finyu kuhusu ndoa.....

Ndoa ni muunganiko wa watu wawili waliopendana na wakaamua kuishi pamoja....kama mwili mmoja....hapo haisemwi kama ni makabila gani na wala ni watu wa asili gani bali kinachoongelewa ni watu wawili waliopendana kwa kuwa mapenzi hayana mipaka.....
Na vile vile suala la mtu kuoa au kuolewa ni suala binafsi...nikiwa na maana linamhusisha mtu mmoja yeye kama yeye....kitendo cha kumuingilia mtu kwenye maamuzi yake yanayohusu ndoa ni sawa na kitendo cha kuyaingilia maisha ya mtu ingawaje kushauriana na mambo ya kawaida hakuna mkamilifu...lakini ushauri wako usiwe kwa shunikizo la yeye achukue maamuzi......

Mchuma janga hula na wa kwao. Ndugu hususan wazazi wana haki ya kuingilia ndoa za watoto wao. Wao walishi, kuna mambo mengi wameyaona sasa unapotaka kufanya jambo ambalo wanaona dhahiri athari yake hawawezi kukaa kimya lazima walisema au kupinga. Wewe una maamuzi ya kukubaliana nao ua kutowasilikiliza.

Si kweli kuwa kila wawili wanapooana basi wameunganishwa na upendo. Ndoa inaweza kuwa ajira, ndoa inaweza kuwa mkakati wa kujipatia mali hata kwa kufanya mauaji au kwa talaka iliyokusudiwa tangu awali kabla ndoa haijafungwa. Ingekuwa kila ndoa ni upendo tusingeshuhudia dhahama kibao kila siku mmoja wa wanandoa akilalamika. michepuko n.k.

Ukiingiza siasa katika suala la ndoa lazima iko siku utajuta hata kimya kimya.
 
Labda Makabila hayo yanaidadi kubwa ya wajane. ndiyo maana hawataki huyo mke mtarajiwa aje kuwa mjane hapo baadaye.
 
nasikia wanawake wakichaga huwa wanakamchezo ka kuua mume especialy mkiwa mmechuma hela to the maxmum and na watoto wa kurithi tayar wapo ndani, nliskia tu wakuu msije anza kuninyea
 
Kuna hizo stori za mauaji wa waume zao baada ya kuchuma Mali na watoto kuwa wakubwa ili wafaidi wao na watu wa kwao. Wengi huamini katika kuchuma Mali kwa mwanaume na kupeleka utajiri kwao. Wanaume wa kusini wengi wanachanganyikiwa na wadada wa kichaga, simshangai rafiki wa mtoa mada. Ila huwezi jua moyo wa mtu
 
Sichagui Sibagui atakaenizika simjui (Kwa hisani ya Ankal)
 
Habari za mchana wanajamvi,

Kuna hiki kitu binafsi mimi sikipendi japo bado kimekuwa kigumu kutoka kwenye baadhi ya vichwa vya watu.Wiki moja iliyopita jamaa yangu ambaye ni mwenyeji wa mkoa wa Mbeya alitembelewa na binti nyumbani kwao,jamaa akaona isiwe shida ikabidi amtambulishe kwa wanafamilia kama mchumba wake mtarajiwa,cha ajabu baadhi ya ndugu wa mwanaume wakauliza huyo msichana ni kabila gani, jamaa akawajibu ni mchaga wa machame, basi wote wakakaa kimya.

Yule binti alipoondoka tu maneno yakaanza mara oooh ndugu yetu sisi hatutaki uoe mwanamke kutoka uchagani aidha machame,au mpare na makabila yote ya mkoa wa Kilimanjaro,ukawa mjadala mrefu jamaa akaanza kubishana kwamba anaoa anayejisikia yeye ukawa ugomvi mkubwa sana na ndugu wa mwanaume wakaanza wakamwambia likimpata la kumpata asiwashirikishe kwani wao wanajua tabia za makabila haya.

Jamani hii tabia itaisha lini kwani makabila haya yana nini kibaya mpaka kunakuwa na ubaguzi wa aina hii.

Maoni yenu wakuu
Hiyo ni muhimu mkuu usichukue. Mimi hapa nikivutiwa na demu machoni na kumuita,baada tu ya salam naulizia mkoa wake wa asili ili nitabiri kabila lake, then namuuliza kabila nikisikia "nshomile" au jamii zao napiga chini na kuanza kuulizia ndizi badala ya gemu.
 
Ukabila tz tunakoenda tutakuwa km wakenya
 
Habari za mchana wanajamvi,

Kuna hiki kitu binafsi mimi sikipendi japo bado kimekuwa kigumu kutoka kwenye baadhi ya vichwa vya watu.Wiki moja iliyopita jamaa yangu ambaye ni mwenyeji wa mkoa wa Mbeya alitembelewa na binti nyumbani kwao,jamaa akaona isiwe shida ikabidi amtambulishe kwa wanafamilia kama mchumba wake mtarajiwa,cha ajabu baadhi ya ndugu wa mwanaume wakauliza huyo msichana ni kabila gani, jamaa akawajibu ni mchaga wa machame, basi wote wakakaa kimya.

Yule binti alipoondoka tu maneno yakaanza mara oooh ndugu yetu sisi hatutaki uoe mwanamke kutoka uchagani aidha machame,au mpare na makabila yote ya mkoa wa Kilimanjaro,ukawa mjadala mrefu jamaa akaanza kubishana kwamba anaoa anayejisikia yeye ukawa ugomvi mkubwa sana na ndugu wa mwanaume wakaanza wakamwambia likimpata la kumpata asiwashirikishe kwani wao wanajua tabia za makabila haya.

Jamani hii tabia itaisha lini kwani makabila haya yana nini kibaya mpaka kunakuwa na ubaguzi wa aina hii.

Maoni yenu wakuu
Wewe binafsi unawaelewaje wachagga wa machame? Tuanzie hapo.
 
Mti wenye matunda ndiyo unaopigwa mawe.
 
Katika hili wachaga mtanuna mtacheka lakini lazima mkubali kwamba dhambi hii inawaandama
Hata mimi sijui ni kwanini?
Dhihilisheni kwa jamii kwamba mnaonewa na wanawake wenu hawana hizo tabia
vinginevyo mtaendelea kuibeba dhambi hiyo
 
Back
Top Bottom