Bahati mbaya jamii zetu na hata waoaji au waolewaji bado wana uelewa finyu kuhusu ndoa.....
Ndoa ni muunganiko wa watu wawili waliopendana na wakaamua kuishi pamoja....kama mwili mmoja....hapo haisemwi kama ni makabila gani na wala ni watu wa asili gani bali kinachoongelewa ni watu wawili waliopendana kwa kuwa mapenzi hayana mipaka.....
Na vile vile suala la mtu kuoa au kuolewa ni suala binafsi...nikiwa na maana linamhusisha mtu mmoja yeye kama yeye....kitendo cha kumuingilia mtu kwenye maamuzi yake yanayohusu ndoa ni sawa na kitendo cha kuyaingilia maisha ya mtu ingawaje kushauriana na mambo ya kawaida hakuna mkamilifu...lakini ushauri wako usiwe kwa shunikizo la yeye achukue maamuzi......
Kumbuka mtu anayeolewa au kuowa ni wewe na kama ni karaha na raha za ndoa utazipata wewe....changamoto zote za maisha ya ndoa utakumbana nazo wewe.....kwa hiyo kama wewe ndiye muhusika mkuu wa hili swala kwanini watu wengine wakufanyie maamuzi ya wewe kuingia kwenye ndoa....!!!???
Vile vile suala la watu kujadili makabila ni moja kati ya masuala yanayoonyesha ni jinsi gani jamii zetu zilivyo mbali na ustaarabu....
Kwa kawaida ubaya...umalaya, wizi na uchafu mwingine wowote hauna sehemu husika bali ni tabia tu mtu aliyoichukua kutoka kwenye jamii iliyomzunguka.....ni kama vile wadada wa kihaya walivyoamua kuuza miili yao ilihali kuna wadada wengi wa kihaya wenye tabia nzuri na wametulia kwenye ndoa zao....tusimuhukumu mtu kwa kabila lake wala kwa mahali alipotoka wala kwa historia yake bali mtu ahukumiwe kwa matendo kama ambavyo mwingine angeyafanya matendo hayo......
MAISHA NI YAKO , CHAGUO NI LAKO......