Kwa ujumla sioni ubaya wa juhudi za kulifufua shirika letu la ndege.
Ni jambo jema tu.
Ila hii ya kununua lidege likubwa kama hilo li Dreamliner, sioni tija yake kwa sasa.
Wangeanza ufufuzi wa hilo shirika kidogo kidogo na hizo ndege ndogo ndogo.
Halafu baadaye baada ya kutengeneza faida ndo wangehitimu kwenye hayo makubwa makubwa ya masafa marefu.
Kununua dege la masafa marefu na kulirusha kwenye safari fupi za ndani ni uwendawazimu!
Kuna kila dalili hilo li Dreamliner litakuwa grounded.
Hii serikali imechemka kabisa hapa!
No two ways about it.