Afisa Tabibu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2021
- 484
- 799
Masela wameacha sofa nyumbani, wapo hospital kumfariji mchizi wao.
Hakuna shada la maua, hakuna chocolate zilizoletwa kama zawadi, wahuni wapo wao na mioyo yao tu.
Hapo zishapigwa story za mademu, ushazungumzwa utani wa mpira, na michongo kibao wanayoisikilizia.
Hapo yamezungumzwa matumaini yasiyo na dalili ya kutimia.
Hapo zipo ndoto za kutoboa maisha, hata zisizo fikirika.
Kila kinywa kina neno la ushindi, hakuna wa kutangaza majanga ya mwenzake hapo, cha siri kitabaki sirini, matusi ndio rejesta pendwa zaidi hapo.
Story kuhusu ugonjwa unaomsumbua mchizi, zimepigwa kwa kiwango kidogo sana..
Washikaji wanaumia mwenzao kulazwa lakini kuna pole chache sana, wahuni wanajali kwa vitendo.
Kuna mwana hana nauli hapo, lakini atachangiwa na kesho atafika kwao.
Kuna mchizi hajui atakula nini, lakini baadae atashiba.
Hapo wameenda kumliwaza mgonjwa, lakini kuna mtu atafarijiwa kuhusu msoto wake kuliko hata huyo aliyelazwa.
Hii picha iwekeni kwenye maktaba zenu, zisizofikiwa na Panya yeyote yule.
Mkikutana na wana ma snitch waonesheni kuwa wanaume tuna kawaida ya kulindana
Hakuna shada la maua, hakuna chocolate zilizoletwa kama zawadi, wahuni wapo wao na mioyo yao tu.
Hapo zishapigwa story za mademu, ushazungumzwa utani wa mpira, na michongo kibao wanayoisikilizia.
Hapo yamezungumzwa matumaini yasiyo na dalili ya kutimia.
Hapo zipo ndoto za kutoboa maisha, hata zisizo fikirika.
Kila kinywa kina neno la ushindi, hakuna wa kutangaza majanga ya mwenzake hapo, cha siri kitabaki sirini, matusi ndio rejesta pendwa zaidi hapo.
Story kuhusu ugonjwa unaomsumbua mchizi, zimepigwa kwa kiwango kidogo sana..
Washikaji wanaumia mwenzao kulazwa lakini kuna pole chache sana, wahuni wanajali kwa vitendo.
Kuna mwana hana nauli hapo, lakini atachangiwa na kesho atafika kwao.
Kuna mchizi hajui atakula nini, lakini baadae atashiba.
Hapo wameenda kumliwaza mgonjwa, lakini kuna mtu atafarijiwa kuhusu msoto wake kuliko hata huyo aliyelazwa.
Hii picha iwekeni kwenye maktaba zenu, zisizofikiwa na Panya yeyote yule.
Mkikutana na wana ma snitch waonesheni kuwa wanaume tuna kawaida ya kulindana