Hii nyumba inaweza kufikia gharama za ujenzi kiasi gani?

Hii nyumba inaweza kufikia gharama za ujenzi kiasi gani?

MrsPablo1

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2013
Posts
1,221
Reaction score
2,235
Naomba kuuliza wataalamu wa ujenzi hizi nyumba za hivi (kama zinavyoonekana sio kubwa) zinaweza kufikia gharama za ujenzi na finishing kali kiasi gani? nataka nikiwa na pesa kamili au inayokaribia kumaliza nyumba ndo nijenge, vyumba viwili au vitatu vidogo na bati llitolee maji nyuma hiyo hidden roof iwe mbele tuu. Msaada wenu tafadhali 😊
IMG_6149.jpeg
IMG_6152.jpeg

 
Kwa Mshahara wa ualimu hiyo nyumba labda ukope mkopo wa miaka nane mara mbili yan miaka 16

Tena sio huo ualimu wako wa diploma msingi namaanisha degree
 
Anza na ramani kwanza, tafuta mtaalamu akuandalie then peleka kwa Qs akupe estimate
 
Fundi wa kupaua awe fundi kweli kinyume na hapo utaichukia nyumba masika!!
 
Hiyo nyumba ni ya kisasa. Na finishing yake Inaitwa primier finishing. Inawez ika gharimu Zaid ya million 100 na kuendelea. Na kama Hauna experience na ujenz kbs bs utataboka sana
 
Fundi wa kupaua awe fundi kweli kinyume na hapo utaichukia nyumba masika!!
Watu wengi wanatoa lawama kwenda Kwa fundi kupaua.
Ila nyumba za hidden roof wa kulaumiwa si fundi bati pekee.

Tatizo la msingi linaanzia kwenye mchoro mzima wa nyumba kabla hata ya kujegwa.
Kuna sehemu niliitwa kwenda kurekebisha nikakuta PVC ya nchi 4 ndiyo imewekwa kama mfereji wa kupokea maji yote ya paa zote mbili 🤔
Matokeo yake mvua kidogo mferji unafurika maji
 
Mm naomba kujua nyumba ya room 3
Kimoja kiwe master, sitting room corridor, balcony mbili inakula matofali mangap mchanga kias gani
 
Back
Top Bottom