Elusive
JF-Expert Member
- Nov 26, 2008
- 223
- 4
Kwa wanaofuatilia vipindi vya CNN International kwa hizi siku za karibuni wataona kuwa kila baada ya nusu saa sauti ya mtangazaji inasema 'from here and every where this is CNN' kwa lugha tofauti pamoja na jina la nchi ambayo hiyo lugha inaongewa na maandishi yakimaanisha ni CNN pamoja na lugha zinazotajwa na kiswahili nacho pia kinatumika katika tangazo hilo ambalo huanza na jina la Tanzania na taswira ya milima na nyika na maneno ya HII NI CNN ikifuatiwa na sauti ya mwandishi Isha Sesei inaongea Hii ni CNN. Tangazo hili ni la sekunde au nusu sekunde lakini nionavyo mimi ni kuwa linadhihirisha kuwa Lugha ya kiswahili ni kubwa na inaongewa na watu wengi hata wakafiria kuingiza katika hayo matangazo yao inafaa tuwapongeze kwa hilo nasi pia tujipongeze kwa kuitukuza Lugha yetu.