Hii ni aibu kwa Wizara ya Utalii kwa kinachoendelea Hifadhi ya Taifa ya Nyerere

SHILLINGS

Senior Member
Oct 24, 2013
160
648
Kwako Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohamed Mchengerwa (Mb),

Hatua za haraka zinahitajika Hifadhi ya Taifa ya Nyerere/Selous. Mgogoro mkubwa unaanza kuibuka kati ya waendesha utalii (tour operator) na watalii wanaoenda kwenye hifadhi hii. Kitendo cha Maaskari wa Mbuga kuwatoa kwa nguvu watalii kwenye ndege hakikubaliki, ni ukosefu wa maadili, akili (commonsense), na nidhamu ya kazi. Tusisubiri hadi watalii wakapigwa, tutaua utalii kwa kukosa maarifa.

Jana Kaimu Mhifadhi Mkuu wa Mbuga za Taifa wa kanda ya kusini alifanya kikao na wadau wa utalii katika hifadhi ya Taifa ya Nyerere kilichofanyika kijiji cha Mloka na kutoa maagizo ya ghafla kwa kila muendesha utalii (tour operator) kulipa tozo ya dola za kimarekani 82.6 kwa kila mgeni (non-residents) na tozo muhsusi kwa wageni wengine ambao atatumia kiwanja kidogo cha ndege cha Mtemere (Selous Mtemere Airstrip).

Tozo hii haijalishi kwamba mgeni alipatikana kabla au baada ya utekelezaji wa amri hii, hivyo kumlazimisha muendesha utalii kulipa hata bila kujali kwamba malipo haya hayakujumuishwa kwenye malipo ya mgeni. Kwa mfano kwa muendesha utalii mwenye wageni 10 atapaswa kuwalipia dola za kimarekani 826. Pamoja na waendesha utalii (tour operators) kuomba muda (grace period) kumekuwa kukitumika nguvu, lugha chafu ambazo zinahatarisha utoaji wa hudua kwenye mbuga hii.

Pamoja na kwamba mbuga hii bado ni changa na kukosa miundombinu ya kutosha kwa watalii, pamoja na kutopata matangazo ya kutosha hivyo kuwa na wageni wachache, katika hali isiyo ya kawaida maaskari wa hifadhi (Rangers) wameanza kutekeleza agizo hili ndani ya masaa 24 kwa kuwatoa kwa nguvu kwenye ndege watalii waliotoka kwenye kiwanja hiki kwenda Zanzibar/Dar es Salaam.

Hali hii imesababisha mgogoro mkubwa kati ya waendesha utalii (tour operators), wenye mahoteli na wageni hivyo kuhatarisha uhai wa kampuni zao, ustawi wa mbuga hii, ajira za watu, na fursa mbalimbali za kiuchumi.

Hatua za haraka zinahitajika. Pascal Mayalla
 
Tozo hii haijalishi kwamba mgeni alipatikana kabla au baada ya utekelezaji wa amri hii

Hatari sana serikali kufanya maamuzi kwa mihemuko.

Maana safari nyingi za watalii wameshalipia kila kitu miezi kibao kabla ya kutua Tanzania.

Hii ya kustukiza mtalii na tour operator wakiwa mwituni wakati tayari maandalizi yote yalishalipwa siku kibao na kwa uwazi ktk dunia ya habari zote kiganjani na ktk intaneti ni la kuhuzunisha ktk karne hii ya 21 .

TOKA MAKTABA :

Mkutano wa mawakala wa usafiri Africa ya Mashariki na Kusini mwa Africa mjini Zanzibar.

video: courtesy of Millard Ayo

ESATA yataka Matumizi zaidi ya TEHAMA katika miamala, kuweka booking ya mahoteli, makaazi ya wageni (Bnb vacation homes ) na usafiri yanahitaji kuongezeka ili kuendana na mazingira ya sasa ya dunia ya utalii na wasafiri n.k

Waziri wa Utalii Zanzibar ataka mkutano huo uje na maazimio ya namna gani eneo hili la Afrika liwe rafiki ki gharama na visa ya kusafiria ili wageni zaidi waweze kumiminika ukanda huu wa Afrika.

AESATA TRAVEL AGENCIES CONFERENCE

Building Sustainable and Resilient Travel Agencies in Africa

22-23 May 2023

The Association of Eastern Africa Travel Agents (AESATA) is a regional membership organization of travel agents from 11 countries in Eastern and Southern Africa. The organization is composed of national travel agent associations from Kenya, Uganda, Tanzania, Somalia, Ethiopia, and Malawi. Others are Rwanda, Zambia, Zimbabwe, Mauritius, and Angola.

The main objective of the Association is to provide a unified platform to address cross-border issues in the travel industry, advocate for an enabling business environment; and act as a single voice to articulate members’ concerns of mutual interest at international forums

Conference Background
Whilst the Covid-19 pandemic devastated the global travel and tourism industry, causing untold economic and social loss, the reality is that the industry was already facing a tumultuous business environment. Faced with a myriad of challenges, such as technological disruptions, changing travel patterns and clients preferences, stringent regulatory environments, shrinking profit margins, and effects of climate change, among others, many travel agencies across the world were already thinking about redefining their business models to confront these realities and survive.

As the post-pandemic recovery journey continues, it should never be business as usual. Travel agents must deeply think about the most effective business approach that will ensure mistakes of the past are avoided, and a much stronger and more resilient industry capable of withstanding global shocks is built. Africa, in particular, needs to rethink its agency business model, embrace adaptive technologies, expand into new markets, and strongly advocate for government support toward growing the industry.

AESATA is organizing this conference under the theme “Rebuilding Sustainable and Resilient Travel Agencies in Africa.” Specifically, the Conference will offer participants an opportunity to:
  • Share knowledge, experiences, and lessons learned post the COVID pandemic
  • Rethink and review the travel agency business model in the aftermath of a changing business environment.
  • Interact and network with industry colleagues and stakeholders
  • Sample and experience the travel and tourism offerings of Zanzibar
Source : AESATA CONFERENCE 2023
 
Kwako Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohamed Mchengerwa (Mb),

Hatua za haraka zinahitajika Hifadhi ya Taifa ya Nyerere/Selous. Mgogoro mkubwa unaanza kuibuka kati ya waendesha utalii (tour operator) na watalii wanaoenda kwenye hifadhi hii. Kitendo cha Maaskari wa Mbuga kuwatoa kwa nguvu watalii kwenye ndege hakikubaliki, ni ukosefu wa maadili, akili (commonsense), na nidhamu ya kazi. Tusisubiri hadi watalii wakapigwa, tutaua utalii kwa kukosa maarifa.

Jana Kaimu Mhifadhi Mkuu wa Mbuga za Taifa wa kanda ya kusini alifanya kikao na wadau wa utalii katika hifadhi ya Taifa ya Nyerere kilichofanyika kijiji cha Mloka na kutoa maagizo ya ghafla kwa kila muendesha utalii (tour operator) kulipa tozo ya dola za kimarekani 82.6 kwa kila mgeni (non-residents) na tozo muhsusi kwa wageni wengine ambao atatumia kiwanja kidogo cha ndege cha Mtemere (Selous Mtemere Airstrip).

Tozo hii haijalishi kwamba mgeni alipatikana kabla au baada ya utekelezaji wa amri hii, hivyo kumlazimisha muendesha utalii kulipa hata bila kujali kwamba malipo haya hayakujumuishwa kwenye malipo ya mgeni. Kwa mfano kwa muendesha utalii mwenye wageni 10 atapaswa kuwalipia dola za kimarekani 826. Pamoja na waendesha utalii (tour operators) kuomba muda (grace period) kumekuwa kukitumika nguvu, lugha chafu ambazo zinahatarisha utoaji wa hudua kwenye mbuga hii.

Pamoja na kwamba mbuga hii bado ni changa na kukosa miundombinu ya kutosha kwa watalii, pamoja na kutopata matangazo ya kutosha hivyo kuwa na wageni wachache, katika hali isiyo ya kawaida maaskari wa hifadhi (Rangers) wameanza kutekeleza agizo hili ndani ya masaa 24 kwa kuwatoa kwa nguvu kwenye ndege watalii waliotoka kwenye kiwanja hiki kwenda Zanzibar/Dar es Salaam.

Hali hii imesababisha mgogoro mkubwa kati ya waendesha utalii (tour operators), wenye mahoteli na wageni hivyo kuhatarisha uhai wa kampuni zao, ustawi wa mbuga hii, ajira za watu, na fursa mbalimbali za kiuchumi.

Hatua za haraka zinahitajika. Pascal Mayalla
Hakuna jambo watanzania wanaweza Rais Samia binafsisha hii mbuga

USSR

Sent from my TECNO B1c using JamiiForums mobile app
 
Hali Mbuga ya Taifa ya Nyerere inazidi kuwa mbaya, ndege zimeanza mpango wa kusitisha safari za mbuga hii na kupemeleka wageni Mikumi, busara inahitajika kulinda uaminifu wa Tour Operators kwa wageni, kuzilinda hoteli, ajira na mitaji kwa waendesha shughuli za utalii. Sekta hii ni very delicate, hatua za haraka zinahitajika.
 
Huu ni ujumbe kutoka kwa Tour Operator:

"Nimepata tarifa ndege tunazo tumia kuleta wageni Nyerere zinaweza cancel kutokana kutokana na hii changamoto ilio jitokeza week hii hapa nimefanya booking wagen wangu waje kesho naambiwa kesho hamna uwakika wa ndege mbaka sasa sababu abiria wengi kutoka Zanzibar ambao walitakiwa waje kesho wamecancel ivyo mm sijui wagen nn niwambie na pesa washalipa mm naomba viongozi wakubwa mtusaidie sana hii nguvu tunatumia kupambana na maisha sisi tumetoka familia duni sana tunafanya kazi ili tunyenge taifa wagen wangu kesho mm ata cha kujibu sina ivyo Naomba mtusaidie sisi wafanya biashara wadogo tunaumia sana na tutafilisika 😭😭😭"

Hali ni mbaya
 
Huu ni ujumbe kutoka kwa Tour Operator:

"Nimepata tarifa ndege tunazo tumia kuleta wageni Nyerere zinaweza cancel kutokana kutokana na hii changamoto ilio jitokeza week hii hapa nimefanya booking wagen wangu waje kesho naambiwa kesho hamna uwakika wa ndege mbaka sasa sababu abiria wengi kutoka Zanzibar ambao walitakiwa waje kesho wamecancel ivyo mm sijui wagen nn niwambie na pesa washalipa mm naomba viongozi wakubwa mtusaidie sana hii nguvu tunatumia kupambana na maisha sisi tumetoka familia duni sana tunafanya kazi ili tunyenge taifa wagen wangu kesho mm ata cha kujibu sina ivyo Naomba mtusaidie sisi wafanya biashara wadogo tunaumia sana na tutafilisika 😭😭😭"

Hali ni mbaya
Hata kwa hili tusimkumbuke magufuli baba?
 
Slava to Nyerere NP
04ADBE5D-9CED-4A5C-86D7-63386E044089.jpeg
 
Kwako Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohamed Mchengerwa (Mb),

Hatua za haraka zinahitajika Hifadhi ya Taifa ya Nyerere/Selous. Mgogoro mkubwa unaanza kuibuka kati ya waendesha utalii (tour operator) na watalii wanaoenda kwenye hifadhi hii. Kitendo cha Maaskari wa Mbuga kuwatoa kwa nguvu watalii kwenye ndege hakikubaliki, ni ukosefu wa maadili, akili (commonsense), na nidhamu ya kazi. Tusisubiri hadi watalii wakapigwa, tutaua utalii kwa kukosa maarifa.

Jana Kaimu Mhifadhi Mkuu wa Mbuga za Taifa wa kanda ya kusini alifanya kikao na wadau wa utalii katika hifadhi ya Taifa ya Nyerere kilichofanyika kijiji cha Mloka na kutoa maagizo ya ghafla kwa kila muendesha utalii (tour operator) kulipa tozo ya dola za kimarekani 82.6 kwa kila mgeni (non-residents) na tozo muhsusi kwa wageni wengine ambao atatumia kiwanja kidogo cha ndege cha Mtemere (Selous Mtemere Airstrip).

Tozo hii haijalishi kwamba mgeni alipatikana kabla au baada ya utekelezaji wa amri hii, hivyo kumlazimisha muendesha utalii kulipa hata bila kujali kwamba malipo haya hayakujumuishwa kwenye malipo ya mgeni. Kwa mfano kwa muendesha utalii mwenye wageni 10 atapaswa kuwalipia dola za kimarekani 826. Pamoja na waendesha utalii (tour operators) kuomba muda (grace period) kumekuwa kukitumika nguvu, lugha chafu ambazo zinahatarisha utoaji wa hudua kwenye mbuga hii.

Pamoja na kwamba mbuga hii bado ni changa na kukosa miundombinu ya kutosha kwa watalii, pamoja na kutopata matangazo ya kutosha hivyo kuwa na wageni wachache, katika hali isiyo ya kawaida maaskari wa hifadhi (Rangers) wameanza kutekeleza agizo hili ndani ya masaa 24 kwa kuwatoa kwa nguvu kwenye ndege watalii waliotoka kwenye kiwanja hiki kwenda Zanzibar/Dar es Salaam.

Hali hii imesababisha mgogoro mkubwa kati ya waendesha utalii (tour operators), wenye mahoteli na wageni hivyo kuhatarisha uhai wa kampuni zao, ustawi wa mbuga hii, ajira za watu, na fursa mbalimbali za kiuchumi.

Hatua za haraka zinahitajika. Pascal Mayalla
Hebu tuwe wazalendo kwa nchi yetu. Tuache kulalamika kila mara tunapoambiwa tulipe ama kodi au tozo. Hilo tukio uliloleta hapa chanzo ni uhuni tu wa hizo kampuni. Mfano hao African Safari na wengine hawataki kulipa park fees y ndege wala hawakutaka kuzungumzia kwa utaratibu kuhusu vibali vya wageni wao waliowabeba. Jamani hatuna wajomba Ulaya, nchi hii tutaijenga wenyewe kwa kodi zetu.

Tusichafue taasisi za serikali. Mwambie mr Sarungi wa African safari afuate taratibu na wenzake wa kampuni nyingine. 🙏🙏🙏
 
Hebu tuwe wazalendo kwa nchi yetu. Tuache kulalamika kila mara tunapoambiwa tulipe ama kodi au tozo. Hilo tukio uliloleta hapa chanzo ni uhuni tu wa hizo kampuni. Mfano hao African Safari na wengine hawataki kulipa park fees y ndege wala hawakutaka kuzungumzia kwa utaratibu kuhusu vibali vya wageni wao waliowabeba. Jamani hatuna wajomba Ulaya, nchi hii tutaijenga wenyewe kwa kodi zetu.

Tusichafue taasisi za serikali. Mwambie mr Sarungi wa African safari afuate taratibu na wenzake wa kampuni nyingine. 🙏🙏🙏
Nidhamu na busara kwa wasimamizi na watedaji wa mbuga ya Taifa ya Nyerere pamoja na waendesha huduma za utalii (Tour Operators) inahitajika kwenye suala hili, malaka husika zinapaswa kufikia makubaliano juu na waendesha shughuli za utalii kweye mkanganyiko huu.

Utalii hauhitaji ubabe, utalii hauhitaji lugha chafu, utalii unahitaji watu wenye weledi na watu wa masuluhisho, amri haziwezi kusaidia. Wadau wa utalii wanapaswa kuandaliwa kabla ya kutoa maamuzi ambayo yatathiri bishara zao, ajira za waendesha wageni (guides), wafanyakazi wa mahoteli/kambi, n.k.

Kwa muda mrefu waendesha huduma za utalii (Tour Operators) wamekuwa wakiuza hifadhi ya Taifa ya Nyerere kwa wageni bila tozo ya $82.6 kwa kila mgeni anayetumia uwanja mdogo wa Mtemere, tozo hii imekuwa ikilipwa kwa wageni wanaoingia kwenye mbuga hii au wanaotumia viwanja vingine vidogo vya kambi zilizopo ndani ya hifadhi. Waendesha huduma za utalii (Tour Operators) hawa hawakuandaliwa kwa mabadiliko haya ya ghafla (ubruptly changes)yaliyojitokeza sasa.

Waendesha huduma za utalii (Tour Operators) ambao tayari wana wageni ambao walifanya-bookings wiki chache nyuma, miezi au miaka michache nyuma bila ya kujumuisha tozo hii (ambayo haikuwepo kabla) wanalazimishwa kuwalipia wageni wao tozo hii.

kwa mfano Muendesha huduma za utalii (Tour Operators) ana wageni ishirini (20) waliofanya booking miezi sita (6) iliyopita wanaotoka Zanzibar kwenda Jimbiza Camp (kwa mfano) iliyopo nje ya mbuga atalazimika kuwalipia wageni wale dola za imarekani 1652 (sawa na Shilingi 3, 882, 200) ambazo kimsingi mgeni hakulipishwa. Kwa muendesha huduma huyu mdogo wa Utalii(Tour Operator) akiwa na makundi 10 kwa mfano ni dhahiri anakwenda kufilisiska na kuua ajira.

Ni wakati sasa wa mamlaka husika kumfikiria huyu mtoa huduma za utalii na kumuandaa kabla ya utekelezaji wa sheria.
 
Nidhamu na busara kwa wasimamizi na watedaji wa mbuga ya Taifa ya Nyerere pamoja na waendesha huduma za utalii (Tour Operators) inahitajika kwenye suala hili, malaka husika zinapaswa kufikia makubaliano juu na waendesha shughuli za utalii kweye mkanganyiko huu.

Utalii hauhitaji ubabe, utalii hauhitaji lugha chafu, utalii unahitaji watu wenye weledi na watu wa masuluhisho, amri haziwezi kusaidia. Wadau wa utalii wanapaswa kuandaliwa kabla ya kutoa maamuzi ambayo yatathiri bishara zao, ajira za waendesha wageni (guides), wafanyakazi wa mahoteli/kambi, n.k.

Kwa muda mrefu waendesha huduma za utalii (Tour Operators) wamekuwa wakiuza hifadhi ya Taifa ya Nyerere kwa wageni bila tozo ya $82.6 kwa kila mgeni anayetumia uwanja mdogo wa Mtemere, tozo hii imekuwa ikilipwa kwa wageni wanaoingia kwenye mbuga hii au wanaotumia viwanja vingine vidogo vya kambi zilizopo ndani ya hifadhi. Waendesha huduma za utalii (Tour Operators) hawa hawakuandaliwa kwa mabadiliko haya ya ghafla (ubruptly changes)yaliyojitokeza sasa.

Waendesha huduma za utalii (Tour Operators) ambao tayari wana wageni ambao walifanya-bookings wiki chache nyuma, miezi au miaka michache nyuma bila ya kujumuisha tozo hii (ambayo haikuwepo kabla) wanalazimishwa kuwalipia wageni wao tozo hii.

kwa mfano Muendesha huduma za utalii (Tour Operators) ana wageni ishirini (20) waliofanya booking miezi sita (6) iliyopita wanaotoka Zanzibar kwenda Jimbiza Camp (kwa mfano) iliyopo nje ya mbuga atalazimika kuwalipia wageni wale dola za imarekani 1652 (sawa na Shilingi 3, 882, 200) ambazo kimsingi mgeni hakulipishwa. Kwa muendesha huduma huyu mdogo wa Utalii(Tour Operator) akiwa na makundi 10 kwa mfano ni dhahiri anakwenda kufilisiska na kuua ajira.

Ni wakati sasa wa mamlaka husika kumfikiria huyu mtoa huduma za utalii na kumuandaa kabla ya utekelezaji wa sheria.
Nimekuelewa vizuri. Muhimu ni uelewa wa pamoja. Wafanyabiashara na viongozi wa hifadhi kila mmoja anamtegemea mwenzake kunufaika. Watoa huduma watii sheria na hifadhi iwe rafiki kwa watoa huduma.

Muhimu ni kuendelea kuzungumza. Ila kwa case iliyoletwa hapa ni kama vile hifadhi ina makosa wakati hao jamaa pia ni source ya tatizo. Ndege ya kwanza waliondoa kiujanja wakataka kuondoa ndege ya pili; kuzuiliwa ndiyo zikaja taarifa nyingi humu. Tushirikiane kujenga taifa. SISI NI TAIFA.🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom