Hii ni aibu kwa serikali ya JK

Hii ni aibu kwa serikali ya JK

Mkondakaiye

JF-Expert Member
Joined
Dec 5, 2011
Posts
838
Reaction score
174
Serikali ya JK imekuwa ikijinadi kwa kujenga madarasa mengi ya shule za msingi na sekondari, majengo ambayo hayana vifaa vya kufundishia, vitabu na walimu. Mwaka huu aibu imewakuta, wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la saba wamefeli sana kiasi cha kufanya ufaulu kitaifa kuwa chini ya 30%. Maafisa elimu wa mkoa wameagizwa kufanya uchaguzi wa wanafunzi hadi kufikia alama 70 kutoka alama ya mwisho kufaulu 100 kati ya 250. lengo ni kujaza madarasa ya sekondari yaliyojengwa ambayo hayana vitabu, walimu na vifaa vya kufundishia. Kazi hiyo inaanza jumatatu tarehe 17/12/2012 ili waziri wa elimu atangaze matokeo tarehe 21/12/2012

Najiuliza kama hapo mwanzo mwanafunzi aliyekuwa anapata alama ya mwisho kuchaguliwa alama 100 hakuwa na uwezo sekondari, leo mwanafunzi anaengia sekondari kwa alama 70 atamudu masomo hayo? yaani kwa wastani ana alama 14 kwa kila somo.

Serikali imeamua kutafuta wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika kuwapeleka sekondari. Hii ni aibu ya serikali ya JK.ambayo inaangalia uwingi (quantity) badala ya ubora (quality)

SERIKALI YA JK IMEVUNA ILICHOPANDA. IMEKALIA KUFANYA UFISADI NA KUSAHAU ELIMU.
 
Serikali ya ccm kwisha kazi yaani wanataka kuua na elimu, hospitalini hakuna dawa watu wanakufa kila kukicha. Wakina mama wanajifungulia njiani/majumbani wanafariki na vichanga vyao kwa kukosa ambulance ya kuwawahisha mahospitalini alafu hapa JF kuna wendawazimu wanasema ssm iendelea pambafu zao. Tunahitaji mabadiliko na raisi wetu tuliopewa na Mungu Dr Slaa tena alichaguliwa na alishinda 2010 kwa asilimia 80% ccm wakachakachua haya yote tunayajua
 
Tanzania nchi ya siasa. Katika elimu siasa, katika afya siasa, katika maliasili siasa, katika serikali za mitaa siasa, katika kilimo (uti wa mgongo ambao sasa nadhani umevunjika) nako ni siasa, hata biashara ni siasa n.k kwa hiyo usishangae kuwa na madarasa mengi yasiyo na walimu, vitabu, maabara nk au kuwa na zahanati nyingi zisizo na matabibu, madawa, laboratory, n.k maana katika siasa maendeleo yanapimwa kwa wingi wa vitu, ubora baadae; hata bidhaa zinazoingia si mnaona ni wingi tu si ubora ndio maana counterfeits kibao wakati ziko mamlaka kama TBS, TFDA, nk lakini hata huko pia siasa! Je, tutafika? msisahau pia tuko kipindi cha mibaka uchumi!
 
Kinachotakiwa ni kupinga huu ujin**** wa magamba kwa nguvu zote kwani wanako tupeleka siko huko, tutawezaje kupambana katika jumuiya ya A M kwa alama 70 za watoto kuingia sekondari?
 
Hili si jambo la kuongelea uvunguni. Kama kuna ushahidi wa nyaraka uwekwe wazi na hatua zichukuliwe. Huu ni uuaji wa Taifa kuliko hata ule wa kuuwa binadamu. Wanaharakati, HakiElimu, n.k. livalieni njuga hili.
 
Hali hiyo inaumiza sana, tukihoji, watoto wa vigogo wanasema hatuna hadhi ya kuhoji. hatujalelewa malezi ya watoto wa vigogo CCM. Tanzania imekuwa ni ya watua wachache wanaokula mishahara ya waalimu, wanaouza magogo nje tushindwe hadi kutengeneza madawati ya wadogo zetu. Elimuk wa sasa Tanzania sio haki ya msingi ni kama suala la Anasa. Inauma. Tunaua Taifa hivi hivi kwa kushabikia siasa za CCM. Nape alisema wao ndio watakaouliuzwa, namwomba aitishe mkutano wa waalimu awaulize kwanini matokeo ni mabaya, na je waliofeli wataenda sekondari kama tulivyozoea kudanganya kutengeneza taifa la watu wa vyeti badala ya uwezo wa kuhoji mambo na kujitegemea?
 
serikali ya jk imekuwa ikijinadi kwa kujenga madarasa mengi ya shule za msingi na sekondari, majengo ambayo hayana vifaa vya kufundishia, vitabu na walimu. Mwaka huu aibu imewakuta, wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la saba wamefeli sana kiasi cha kufanya ufaulu kitaifa kuwa chini ya 30%. Maafisa elimu wa mkoa wameagizwa kufanya uchaguzi wa wanafunzi hadi kufikia alama 70 kutoka alama ya mwisho kufaulu 100 kati ya 250. Lengo ni kujaza madarasa ya sekondari yaliyojengwa ambayo hayana vitabu, walimu na vifaa vya kufundishia. Kazi hiyo inaanza jumatatu tarehe 17/12/2012 ili waziri wa elimu atangaze matokeo tarehe 21/12/2012

najiuliza kama hapo mwanzo mwanafunzi aliyekuwa anapata alama ya mwisho kuchaguliwa alama 100 hakuwa na uwezo sekondari, leo mwanafunzi anaengia sekondari kwa alama 70 atamudu masomo hayo? Yaani kwa wastani ana alama 14 kwa kila somo.

Serikali imeamua kutafuta wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika kuwapeleka sekondari. Hii ni aibu ya serikali ya jk.ambayo inaangalia uwingi (quantity) badala ya ubora (quality)

serikali ya jk imevuna ilichopanda. Imekalia kufanya ufisadi na kusahau elimu.

hakika wahenga walisema ukubwa wa pua si wingi wa kamasi

 
Kwani wana haja ya kujua wanaoingia humo wana akili au walifaulu
Kwani watoto wao wamo katika hilo kundi
Watoto wao wako katika zile shule zinaoanza na Saint fulani na International School na hawako huku kwa akina sie ambako walimu badala ya kufunsisha wanauza maandazi na wengine wamejiajiri kupaka rangi viatu
Sasa shuhudia janga hilo la watakaofaulu kidato cha pili na cha nne kama sio na ha wataambiwa wenye Div four waruhusiwe kuingia vyuo vikuu maana Div one na Two zitakuwa nadra sana

Hii ni Tanzania zaidi ya uijuavyo
 
Serikali ya JK imekuwa ikijinadi kwa kujenga madarasa mengi ya shule za msingi na sekondari, majengo ambayo hayana vifaa vya kufundishia, vitabu na walimu. Mwaka huu aibu imewakuta, wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la saba wamefeli sana kiasi cha kufanya ufaulu kitaifa kuwa chini ya 30%. Maafisa elimu wa mkoa wameagizwa kufanya uchaguzi wa wanafunzi hadi kufikia alama 70 kutoka alama ya mwisho kufaulu 100 kati ya 250. lengo ni kujaza madarasa ya sekondari yaliyojengwa ambayo hayana vitabu, walimu na vifaa vya kufundishia. Kazi hiyo inaanza jumatatu tarehe 17/12/2012 ili waziri wa elimu atangaze matokeo tarehe 21/12/2012

Najiuliza kama hapo mwanzo mwanafunzi aliyekuwa anapata alama ya mwisho kuchaguliwa alama 100 hakuwa na uwezo sekondari, leo mwanafunzi anaengia sekondari kwa alama 70 atamudu masomo hayo? yaani kwa wastani ana alama 14 kwa kila somo.

Serikali imeamua kutafuta wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika kuwapeleka sekondari. Hii ni aibu ya serikali ya JK.ambayo inaangalia uwingi (quantity) badala ya ubora (quality)

SERIKALI YA JK IMEVUNA ILICHOPANDA. IMEKALIA KUFANYA UFISADI NA KUSAHAU ELIMU.

MKUU MKONDAKAIYE!!

Heshima kwako MKUU!

Kwa taarifa yako, huu ni mpango maalimu wa kuwapa elimu duni watoto wa kiTanzania, huku watoto wa viongozi wakisoma kwenye shule zilizo bora na hasa nje ya nchi ili tuendelee kuwawajinga. Na mwisho wa siku watoto wao ndio waje waendeleze tawala zao za kifalme na ki- ukoo hapa nchini. si uliona dada Mwanaasha pamoja na kupata division 0, sasa hivi yupo USA anasoma!!

Wala usishangae kwa hilo, miaka hii michache kabla ya 2015 utashuhudia mengi. Na utaiona nchi yetu Tanganyika ikiingia kwenye maajabu ya dunia ya taifa lililo jaa wajinga wasio juwa kusoma wala kuandika. Si hayo tu, subiri maajabu mengine yanakuja soon.

2015 weka alama ya ndiyo kwa CHADEMA. halafu utauona moto wake.
 
Kila mchuma majanga atalia na wakwao.Natamani nione siku chadema inaapishwa sijui wanachama na viongozi wa ccm watajitetea vipi mbele ya serikali ya chadema
 
Kuna posti ukisoma unaweza lia machozi! Wale watu wanaoitetea CCM hivi wamerogwa?? Unaanzaje anzaje kuwatetea magamba!?
Jinsi ninavyoamini katika elimu., naamini kwa elimu bora gape la waliokuwa nacho na wasiokuwa nacho litafutika.
 
wasomi wakiongezeka ni kero kwao watakuwa usumbufu kwa jamii. ndio maana wanafanya mambo kama haya.
 
Kuna posti ukisoma unaweza lia machozi! Wale watu wanaoitetea CCM hivi wamerogwa?? Unaanzaje anzaje kuwatetea magamba!?
Jinsi ninavyoamini katika elimu., naamini kwa elimu bora gape la waliokuwa nacho na wasiokuwa nacho litafutika.

hata dr.slaa alishawahi kusema hv watanzania tumerogwa yani kuna watu hata uwape fact gani yani wanatetea ccm utasema nini sijui.
 
am speaking from the heart,..2005 sikumpigia kura jk pamoja na ushabiki mkubwa wa simba na yanga wa watu,eti mtetezi wa wanyonge,jamaa nilijua mpigaji tokea yuko wizara ya nishati na madini
 
Hili si jambo la kuongelea uvunguni. Kama kuna ushahidi wa nyaraka uwekwe wazi na hatua zichukuliwe. Huu ni uuaji wa Taifa kuliko hata ule wa kuuwa binadamu. Wanaharakati, HakiElimu, n.k. livalieni njuga hili.

Mkuu Ruge unataka waraka wa nini wakati maafisa elimu wa mikoa na wilaya wako kazini kuwatafuta hao wanafunzi waliofeli ili waende sekondari. hapo ulipo nenda ofisi za elimu uliza afisa elimu wa wilaya yako au mkoa wako yuko wapi. na tarehe 21/12/2012 fuatilia wanafunzi waliochaguliwa alama zao mwisho ni ngapi.
 
Serikali ya JK imekuwa ikijinadi kwa kujenga madarasa mengi ya shule za msingi na sekondari, majengo ambayo hayana vifaa vya kufundishia, vitabu na walimu. Mwaka huu aibu imewakuta, wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la saba wamefeli sana kiasi cha kufanya ufaulu kitaifa kuwa chini ya 30%. Maafisa elimu wa mkoa wameagizwa kufanya uchaguzi wa wanafunzi hadi kufikia alama 70 kutoka alama ya mwisho kufaulu 100 kati ya 250. lengo ni kujaza madarasa ya sekondari yaliyojengwa ambayo hayana vitabu, walimu na vifaa vya kufundishia. Kazi hiyo inaanza jumatatu tarehe 17/12/2012 ili waziri wa elimu atangaze matokeo tarehe 21/12/2012

Najiuliza kama hapo mwanzo mwanafunzi aliyekuwa anapata alama ya mwisho kuchaguliwa alama 100 hakuwa na uwezo sekondari, leo mwanafunzi anaengia sekondari kwa alama 70 atamudu masomo hayo? yaani kwa wastani ana alama 14 kwa kila somo.

Serikali imeamua kutafuta wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika kuwapeleka sekondari. Hii ni aibu ya serikali ya JK.ambayo inaangalia uwingi (quantity) badala ya ubora (quality)

SERIKALI YA JK IMEVUNA ILICHOPANDA. IMEKALIA KUFANYA UFISADI NA KUSAHAU ELIMU.

Kilichosababisha kufeli pia inatakiwa tukumbuke wanafunzi hawa wamefanya mtihani tofauti na miaka ya nyuma kwani ndo walianzisha mfumo wa KUSHED kwa maswali ya multiple choice tu kitu ambacho ndo kinaendelea kudidimiza elimu yetu sijawahi kuona mwanafunzi anajibu mtihani wa Hesabu kwa multiple choice hawa akina Mulugo wanakotupeleka sio kwenyewe.
 
Walimu wakiomba madai yao magamba wanawapeleka mahakamani wakidhani wanawakomoa
 
Serikali ya JK imekuwa ikijinadi kwa kujenga madarasa mengi ya shule za msingi na sekondari, majengo ambayo hayana vifaa vya kufundishia, vitabu na walimu. Mwaka huu aibu imewakuta, wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la saba wamefeli sana kiasi cha kufanya ufaulu kitaifa kuwa chini ya 30%. Maafisa elimu wa mkoa wameagizwa kufanya uchaguzi wa wanafunzi hadi kufikia alama 70 kutoka alama ya mwisho kufaulu 100 kati ya 250. lengo ni kujaza madarasa ya sekondari yaliyojengwa ambayo hayana vitabu, walimu na vifaa vya kufundishia. Kazi hiyo inaanza jumatatu tarehe 17/12/2012 ili waziri wa elimu atangaze matokeo tarehe 21/12/2012

Najiuliza kama hapo mwanzo mwanafunzi aliyekuwa anapata alama ya mwisho kuchaguliwa alama 100 hakuwa na uwezo sekondari, leo mwanafunzi anaengia sekondari kwa alama 70 atamudu masomo hayo? yaani kwa wastani ana alama 14 kwa kila somo.

Serikali imeamua kutafuta wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika kuwapeleka sekondari. Hii ni aibu ya serikali ya JK.ambayo inaangalia uwingi (quantity) badala ya ubora (quality)

SERIKALI YA JK IMEVUNA ILICHOPANDA. IMEKALIA KUFANYA UFISADI NA KUSAHAU ELIMU.
Wasije wakasema Ni Blandina kasababisha.......
 
Kuna jamaa yangu, amenionyesha TSM 9 mwanafunzi kidato cha kwanza 2013 kwa jumla ya Alama 69. Amechanguliwa. Hili ni janga la kitaifa.
 
Back
Top Bottom