FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 36,066
- 40,725
Familia ya Rockerfeller ndio familia ya kitajiri zaidi huko Marekani inayoshikilia sekta za Kibenki, Kiviwanda, Mafuta na Siasa. Inatajwa kwamba matajiri wote duniani wanaongozwa na kuendeshwa na familia hii, hasa hasa Billgates na wenzake.
Mwaka 2010 walitotoa maelekezo kwa matajiri na wanasiasa vibaraka waliochini yao kuandaa mpango kabambe wa ‘Lock up’ ya dunia, yaani jinsi ya kuifungia dunia nzima iwe inakaa ndani tu kama wafungwa , tena kwa hiari yao. Mpango uliweka hatua zifuatazo.
1.) Kiandaliwe kirusi kinachosambaa kwa kasi sana ila kinachoua kwa asilimia ndogo sana ili kiweze kuendana na mpango ulioandaliwa.
2.) Kirusi kiboreshwe na kiweze kutumika kama silaha endapo kitahitajika.
3.) Kirusi kisafirishwe hadi kwenye maabara ya daraja la 4 huko Winnipeg Canada, halafu kiibiwe na WaChina na kisafirishwe hadi China ( ShinZhengli).
4.) Viongozi wa taasisi zote kubwa na za magongwa duniani na Marekani za CDC, WHO, UN ambao wangehusika moja kwa moja na kutoa taarifa ugonjwa wafadhiliwe kwa pesa nono ili waweze kutoa yale maelezo na maelekezo (lockdown) ambayo tunataka wayatoe kwa dunia, watu hao wa kufadhiliwa ni pamoja na Faucci wa CDC, Tedros wa WHO nk.
5.) Tumtumie Billgates kufadhili na kusimamia mpango wa kufanya utafiti wa Chanjo na kusimamia mpango wa kuisambaza dunia nzima na kuhakikisha kila binadamu duniani anachoma chanjo hiyo.
Sasa baada ya kuvuja kwa nyaraka hizi , walitumia vyombo mbalimbali vya habari vya kihuni kutoa ufafanuzi na utetezi, mfano ni hii propaganda video iliyojaribu kusema kwamba hiyo document iliandikwa kwa nia njema tu ya kuiandaa dunia kwa hatari mbalimbali za kiafya, na haukuwa mpango., video ipo chini.