Mkuu wewe ndo umetaja wasukuma na wavivu, bila kujali kabila yoyote akiwa mvivu hajitumi na akili mgando hawezi kufanikiwa, maana maendeleo ni udhubutu.
Mkuu swala lakuwa na dhahabu nakubaliana nalo na ingetakiwa kanda ya ziwa ipige maendeleo makubwa kwa sababu ya hayo madini, but unfortunately hali huko ndo mbaya kuliko inavotakiwa, rasilimali za madini hazijaweza kuisadia Africa, hususani Tanzania kujikwamua maana inaendeshwa na mabepari ka Acacia kwa hyo return kwa community ni mdogo, hayo madini hayawwzi kuondoa umaskini kusikochukuliwa hatua madhubuti maana madini hayagusi wananchi moja kwa moja ka shughuli nyingine za uchumi.
Hyo ya wachaga kukimbia kwao ni akili ya kwenda kutafta fursa sehemu nyingine ili kujipanua hata mataifa makubwa yanaleta makampuni yao kuwataftia wananchi wao fursa kuondoa u maskini, ndo mana nchi hii miradi mingi inafanywa na wageni hyo yote ni fursa hata wewe usikae sehemu moja eti kisa kwenu usiangalie fursa nyingine huo ni uzembe, watu wana search green pasture.
Mkuu shule za kata zimekataje mzizi wa fitina wakati ndo zimesaidia kuondoa ujinga kwa Watanzania wengi. Kumrudisha nyuma aliyetangulia sio solution dawa ni wewe kujikwamua ili upige hatua, mi tangia nimeanza shule darasni waliokuwa wengi walikuwa wachaga, wahaya wanyakyusa sana sana mkuu kwa wingi.
Miaka kumi waweza kutawala lakini itategemea umeijengea vipi jamii yako kuhusu kuwa na mwamko wa elimu na Ku grab different opportunities.
Sawa ndugu ila uache habari za kujisifu, sabab wachaga ni watanzania, waafrika na Waafrka bado ni watu duni katika dunia.Hkuna mchaga anatambulika katika matajiri wa Afrika na dunia.Hivyo tupambane tu kuondokana na umaskini kama wenzetu wa bara Asia wanatoka taratibu katika poverty circle, tusifurahie umasikini wa mtu yeyote mweusi kwani ni aibu ya wote.