Kumekuwepo na taarifa kuhusiana na mabadiliko ya uongozi ndani ya CCM hasa katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara na Katibu Mkuu.kuna fununu kuwa Mzee Kinana ameshaandika barua ya kuomba kupumzika na kwa upande wa Katibu Mkuu inasemekana Mama haridhishwi na utendaji wa katibu mkuu wa sasa Ndg Daniel Chongolo.
Sina uhakika kama taarifa hii ni ya kweli lakini kama mwana CCM nimeandaa uchambuzi huu ili kuangazia ni makada gani wa CCM wanaweza kuwa msaada mkubwa hasa wakati huu tunapoelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na vitongoji wa 2024 na uchaguzi mkuu wa 2025.
Ni ukweli usiopingika kuwa upinzani umekua hapa nchini na vilevile kuna changamoto nyingi za wananchi hazijashughulikiwa ipasavyo hivyo ni muhimu CCM ikawapata viongozi makini zaidi,wenye uwezo mkubwa zaidi waadilifu na wenye uwezo wa kuunda mfumo imara unaoweza kuisimamia serikali.
MAKAMU MWENYEKITI
WANAOTAJWA NI
Mizengo Pinda
Abdalllah Bulembo
Steven Wassira na
Dr Bashiru Ally Kakurwa.
Anayefaa ni Dr Bashiru Ally Kakurwa
Huyu amewahi kuwa katibu mkuu wa CCM,na alihudumu kwa muda mfupi katika nafasi ya Katibu mkuu kiongozi baada ya kifo cha Kijazi.Huyu ni msomi wa ngazi ya Daktari wa falsafa na kwakuwa ni mtaalamu mbobezi wa sayansi ya siasa anajua vilivyo namna ya kwenda na upepo wa siasa.
Alifanya kazi nzurikama Mwenyekiti wa kamati maalumu iliyopewa kazi na JPM ya kukagua,kubaini na kuchunguza mali za CCM nchi nzima.
Kamati hii ndiyo iliyowaondoa mchwa wote waliokuwa wameatamia mali za Chama na mapato ya CCM yaliongezeka zaidi kutokana na kazi nzuri iliyofanywa na kamati hiyo.
Huyu ndiye mtu sahihi zaidi katika nafasi ya makamu Mwenyekiti wa CCM Bara kwa wakati huu.
Bado umri unamruhusu na ni mtu mwenye ushawishi mkubwa wa kisiasa hapa nchini kutokana na imani ya walio wengi kuwa hana harufu ya ufisadi na track record yake inaonyesha kuwa siyo kiongozi anayetumia nafasi yake kujinufaisha.
Isitoshe ni muumini mzuri wa siasa ya ujamaa na kujitegemea ambayo ndiyo itikadi ya CCM.
Wana CCM wengi wanamkubali na kama atateuliwa katika nafasi hiyo CCM watakuwa wamelamba dume
NAFASI YA KATIBU MKUU
Wanaotajwa ni
Nape Nnauye
Amos Makala
Dr Albert Chalamila na
Dr Emmanuel Nchimbi
Anayefaa ni Dr Emmanuel Nchimbi
Huyu ni miongoni mwa viongozi seniors ndani ya CCM hasa kutokana na kushika nafasi nyeti ndani ya CCM ikiwemo Mwenyekiti wa UVCCM taifa.
UVCCM ya Dr Emmanuel Nchimbi ilikuwa ni UVCCM kwelikweli
Siyo hii ya sasa na sisi wana CCM kindakindaki tuna kamsemo ketu kuwa "Nchimbi aliondoka na UVCCM yake.
Kwhiyo Dr Emmanuel Nchimbi anaijua vyema CCM na hata katika secretariat ya sasa hakuna mtu zaidi yake.
Huyu atakiimarisha Chama zaidi.
Matukio mbalimbali yanayoendelea chini ya kapeti ndani ya Chama yanaonyesha "Chama kimevamiwa"
Baada ya uteuzi wa Mwenezi Paul Christian Makonda ni vyema CCM ikawaleta on board "Viongozi halisi" ili iweze kurudi kwenye njia.
Kwasasa hakuna mtu mwingine anayefaa zaidi ya Dr Emmanuel Nchimbi na kinyume chake ni kuendeleza mzaa.
CCM ya sasa imekuwa dhaifu sana kutokana udhaifu wa baadhi ya wajumbe wa secretariat ya sasa na mtu atakayenyoonya mambo ni Dr Emmanuel Nchimbi.
Sina uhakika kama taarifa hii ni ya kweli lakini kama mwana CCM nimeandaa uchambuzi huu ili kuangazia ni makada gani wa CCM wanaweza kuwa msaada mkubwa hasa wakati huu tunapoelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na vitongoji wa 2024 na uchaguzi mkuu wa 2025.
Ni ukweli usiopingika kuwa upinzani umekua hapa nchini na vilevile kuna changamoto nyingi za wananchi hazijashughulikiwa ipasavyo hivyo ni muhimu CCM ikawapata viongozi makini zaidi,wenye uwezo mkubwa zaidi waadilifu na wenye uwezo wa kuunda mfumo imara unaoweza kuisimamia serikali.
MAKAMU MWENYEKITI
WANAOTAJWA NI
Mizengo Pinda
Abdalllah Bulembo
Steven Wassira na
Dr Bashiru Ally Kakurwa.
Anayefaa ni Dr Bashiru Ally Kakurwa
Huyu amewahi kuwa katibu mkuu wa CCM,na alihudumu kwa muda mfupi katika nafasi ya Katibu mkuu kiongozi baada ya kifo cha Kijazi.Huyu ni msomi wa ngazi ya Daktari wa falsafa na kwakuwa ni mtaalamu mbobezi wa sayansi ya siasa anajua vilivyo namna ya kwenda na upepo wa siasa.
Alifanya kazi nzurikama Mwenyekiti wa kamati maalumu iliyopewa kazi na JPM ya kukagua,kubaini na kuchunguza mali za CCM nchi nzima.
Kamati hii ndiyo iliyowaondoa mchwa wote waliokuwa wameatamia mali za Chama na mapato ya CCM yaliongezeka zaidi kutokana na kazi nzuri iliyofanywa na kamati hiyo.
Huyu ndiye mtu sahihi zaidi katika nafasi ya makamu Mwenyekiti wa CCM Bara kwa wakati huu.
Bado umri unamruhusu na ni mtu mwenye ushawishi mkubwa wa kisiasa hapa nchini kutokana na imani ya walio wengi kuwa hana harufu ya ufisadi na track record yake inaonyesha kuwa siyo kiongozi anayetumia nafasi yake kujinufaisha.
Isitoshe ni muumini mzuri wa siasa ya ujamaa na kujitegemea ambayo ndiyo itikadi ya CCM.
Wana CCM wengi wanamkubali na kama atateuliwa katika nafasi hiyo CCM watakuwa wamelamba dume
NAFASI YA KATIBU MKUU
Wanaotajwa ni
Nape Nnauye
Amos Makala
Dr Albert Chalamila na
Dr Emmanuel Nchimbi
Anayefaa ni Dr Emmanuel Nchimbi
Huyu ni miongoni mwa viongozi seniors ndani ya CCM hasa kutokana na kushika nafasi nyeti ndani ya CCM ikiwemo Mwenyekiti wa UVCCM taifa.
UVCCM ya Dr Emmanuel Nchimbi ilikuwa ni UVCCM kwelikweli
Siyo hii ya sasa na sisi wana CCM kindakindaki tuna kamsemo ketu kuwa "Nchimbi aliondoka na UVCCM yake.
Kwhiyo Dr Emmanuel Nchimbi anaijua vyema CCM na hata katika secretariat ya sasa hakuna mtu zaidi yake.
Huyu atakiimarisha Chama zaidi.
Matukio mbalimbali yanayoendelea chini ya kapeti ndani ya Chama yanaonyesha "Chama kimevamiwa"
Baada ya uteuzi wa Mwenezi Paul Christian Makonda ni vyema CCM ikawaleta on board "Viongozi halisi" ili iweze kurudi kwenye njia.
Kwasasa hakuna mtu mwingine anayefaa zaidi ya Dr Emmanuel Nchimbi na kinyume chake ni kuendeleza mzaa.
CCM ya sasa imekuwa dhaifu sana kutokana udhaifu wa baadhi ya wajumbe wa secretariat ya sasa na mtu atakayenyoonya mambo ni Dr Emmanuel Nchimbi.