Hii ndio Bei ya unga wa sembe na dona nilipo

Hii ndio Bei ya unga wa sembe na dona nilipo

ukweli hili limeshakua janga na sasa ndio tutajua ukweli wa tani milioni moja
 
Serikali inatakiwa ichukue hatua kudhibiti huu mfumuko. Huyo anayeomba exemption, tumpe ila tumpangie bei ya kuuza. Wananchi wengi shs 100 bado ni pesa kubwa.
 
NAWAAMBIA WANANCHI WA TANZANIA HAKUNA NJAA, NIMEPITA PALE NIMEKUTA MU KALIMA NYANYA ZIKIWA ZA KIJANI KABISA AJABU JIRANI YAK KALIMA MAHINDI YAMEKAUKA. MBONA YULE WA NYANYA NI ZA KIJANI?????

KWA KWELI HAKUNA UKAME, MVUA ZINANYESHA NENDENI MKALIME.

HAPA KAZI TU!!!!!
 
Kazi ipo kwa ambao hamjawahi kushuhudia njaa live mwaka huu mtapata exprience japo tumuombe Mungu mtukufu atuepushie mbaali baa la njaaa ni hatari mno kwa wanaolikumbuka duh!
 
Kg 50 ya unga sawa elfu 74000 duh... Mfuko wa cement kg 50,elfu14500 bora kujenga...
 
Ugali,uji,ni mainly food kwa jamii nyingi za kiafrica hasa mahindi ambayo hutumiwa sana na karibu makabila mengi ya kitanzania,sisi huku kwetu,tunalima mahindi,ngano ndio main food yetu,tens tunalima kwa jembe la mkono,sababu ya milima trector na maksai hawawezi tumika, so tukikosa mvua hatuvuni kabisa ,sasa habari ya kupanda bei ya sembe na dona nakumbwa na wasiwasi na mvua hazijanyesha kwa hiyo njaa naiona ileee inakuja kwetu,
 
Mitaa ninayokaa mabachela huwa inawalazimu kutembea umbali wa kutembea kwa dakika 20 au nusu saa ili angalau kupata mlo wa ugali wenye bei nafuu manake bei ya mtaani haikamatiki.
 
Habari wakuu, hali ya maisha imezidi kuwa mbaya kiuchumia kwa baadhi ya raia wengi wa nchi hii. Pesa ikiwa haipatikani na ikipatikana hamna cha maana unachoweza kuifanyia...

Nimekuwa nasikia kupanda kwa unga tu, jana nimepita mashine kununua unga kilo 25 kwa bei ya jumla na kukuta unga umepanda bei kwa asilimia kubwa mwanzo unga kilo 25 tulikuwa tunanunua kwa sh.32.000 ila kwa sasa umefika sh 37000...

Bei ya reja reja kwa eneo nililopo kilo moja ni 1700.. Itakuwa vyema uzi huu ukatumika kupeana bei ya chakula hiki muhimu kwa watanzania wengi.
adfba84f3f18c8ee03dc844ec17d2a4c.jpg
e8ab08f50309bbc0f9692d43229857a5.jpg
019a2a868b6d355f5f05284cbc510966.jpg
Kimahesabu nunua huo wa kilo 50 kwa shilingi 74,000/= utaokoa fedha nyingi sana. Kilo moja ni shilingi 1480/=
 
Tatizo ni kuto amua kuwa wakweli ,maisha yana mutual niche, ukiona wanyama wanakufa kwa ukame ,that's means herbivores wanakosa chakula wanakufa, pia carnivores watakosa lishe hii ni hatari kwa viumbe wote yaani had I wadudu wata athirika ,man hasa mtanzania.anayetegemea mshara na kilimo kwa price hii ya mahindi ,after couple of days njaa itamkumba tu,
 
Back
Top Bottom