Hii Mikoa Nani Kailoga?


Wacha uongo wewe..Mkoa ganiupo jirani na Pwani ambao Rais anatoka....?????

Mikoa jirani na Pwani ni Dar, Moro na Tanga....

Au unamaanisha Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani..
 
Usiulize mikoa hiyo imelogwa na nani, jiulize wewe mwenyewe na hata Tanzania imerogwa na nani! Hiyo mikoa unayoiona wewe kuwa bora, wenzako wa majuu wanaona kama ni vijiji tu! Jiulize, kwanini baadhi ya watumishi wa makampuni ya kimataifa wanafanya kazi Tanzania lakini wanalala Nairobi au J'Burg?
 
Wacha uongo wewe..Mkoa ganiupo jirani na Pwani ambao Rais anatoka....?????

Mikoa jirani na Pwani ni Dar, Moro na Tanga....

Au unamaanisha Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani..
tedo,
Usikurupuke kujibu post ya mwenzako bila kusoma kwa makini kilichoandikwa. Muktadha wa nilichoandika na ulichonukuu ni tofauti kabisa.
Hakuna mahali ambapo nimeandika mkoa jirani NA Pwani, ila nimeandika mkoa jirani WA Pwani. Kuna tofauti kubwa ya 'NA' na 'WA'. Soma vizuri post yangu hapo juu.
 
Last edited by a moderator:
Tabora Kigoma Rukwa Katavi Singida Lindi Mtwara Ruvuma na bado inaikumbatia ccm.Ama kweli umasikini ni mtaji wa ccm

duuh kumbe maendeleo ya mbeya yamepatikana kwa ajili ya upinzan au yale ya dar.Namuunga mkono aliyesema kuna haja ya watu kujuzwa historia ( history is a good teacher by st Augustine)
 

kweli mkuu m natoka ruvuma na nimeish mbeya, iringa , morogoro na dodoma nakufaham kidogo co anachokizungumza nazani amesikia tu ila hawez kuthibitisha infact ruvuma tunapiga hatua coz kwa sasa nimekaa na wengi wanaotoka uko anakosema kumeendelea na wengi wao naona wANa njaa kama mimi xo kugeneralize mambo wakati hali ni kama zinalingana cio kitu cha kukiamini.
 
Kwa ujumla maeneo mengi yenye umwinyi mwinyi hayana maendeleo pamoja na watu wake
 
Jiulize kwanini Bandari ya mtwara haiendelezwi wakati ni Bandari yenyekina kirefu kuliko DSM? Jiulize kwanini reli ya mtwara iliondolewa. Halafu uje Na Uzi huu. Hakuna alio iroga bali ni chuki Na husuda za baadhi ya viongozi wa nchi hii. Nitasema kweli daima fitina majungu Na unafiki kwangu mwiko. Ahadi ya mwanaTANU hiyo
 
Nashangaa wazanzibar wanavyolalamika muungano unawanyonya au unapendelea bara,wakati hata mikoa hii mi 3 bado nayo iko nyuma kutokana na kero za muungano lakin haijawah kudai tanganyika yao.

Zanzibar ni nchi na hiyo ni mikoa tu ya Tanganyika. Hata kilimo kwanza kimedunda, endelea kusubiri big result now.
 

Hakuna mji wenye sida ya maji kama Arusha,...Khaaa!!!
 
usikimbie ukweli mkuu, usisifie kitu kwa kuangalia upenzi, Mtwara bado iko nyuma na wala usitishwe na hyo gas iliyopatika huko, embu cheki mfano wa dhahabu na mkoa wa shinyanga

We endelea kujitoa ufahamu tu...!!
 
Hakuna mji wenye sida ya maji kama Arusha,...Khaaa!!!

Thats true huko Dodoma hapo mjini utasema umeendelea ukienda mitaa kadhaa tu yapale mjini raia ni maskini wa kutupwa na maji ndo shida usipime.
 

usiongopee watu mikoa yote ina maskin na hali mbaya sana,kariakoo nyumba za udongo ni juz tu zmeondoka, hyo kagera yako haina lolote mm naishi huko kagera biharamulo nyabusozi,muleba ndo ucseme khaaa misifa ya bure na roho mbaya mbaya tu. naconclude kuwa; MJINI NI NYuMbani KWako si kwa jirani,inawezekana ukawa unishi Dar na mm singida au lindi na kiuchumi usifue dafu.
 
Chunguza dini iliyotamalaki huko ndo utajua..

RUKWA, MARA, RUVUMA, na SINGIDA humo mwote imetamalaki dini gani?? au wewe ni lukuv mzee wa makanisa.....??
 
TZ yote majanga hamna afadhali wala ahueni...tuulizeni sisi ambao tunafanya vibiashara vyetu hapo NAIROBI.........
 
mkuu umenichekesha ivi unafikiri mtu mmoja ndo anaweza kuleta maendeleo au unataka kuniambia kule mbeya sugu ndo amepafanya pawe vile au huijui vizuri historia ya nchi hii? toa mikakati ya kweli ci kutuletea porojo kama za wanaojiita ukawa.

Sugu katajwa wapi? Au mcharuko tu?
 
Una maslahi binafsi Sizinga (Signature yako nimeiona...declare please!)....ni kweli Mtwara na Lindi zitakuwa mbali sana kiuchumi miaka ijayo kwa hii gesi asilia

Huko ni kujidanganya!! Tulitegemea shinyanga ingekuwa tajiri mno kutokana na almas lakini waapi!! Iko wapi tanzanite ya arusha? Hivi uranium ina mchango gani kwa taifa? Hebu tulia kwanza, usije ukaongeza mke kwa ajili eti gas imegundulika mtwara!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…