Hii Mbeya umeme vipi?

Hii Mbeya umeme vipi?

Da Vinci XV

JF-Expert Member
Joined
Dec 7, 2019
Posts
3,871
Reaction score
6,468
HII MBEYA UMEME VIPI?

Ndagafijo

Nimetoka zangu huko visiwani nyumbani kwa mama wa nchi nikasema walau nijivinjari huku bara, ili kusaka tonge ili yule bidada mrembo asiye na doa, nimmilikiye asije nikimbia licha ya subra na uvumilivu alojaliwa na manaan.

Sio hilo tu je huyu binti yake ambaye , ambaye akitoka kwa uzuri mama yangu mzazi yeye ndio anafuatia katika dunia hii je angelikula wapi bila ya mimi baba yake kuvuja jasho?

Nikajichimbia dar nimebamizwa na joto la mwendokasi hapo mpaka ubongo ukachemka ipasavyo ,nikashuka songea hapo kuna vijimambo nilikuwa nachimba na project kadhaa wa kadhaa kuhusu vita vya maji maji na masapta sapta mengine kedekede.

Nikakwea Bus mpaka kwa wanyakyusa, Ndagafijo, kule Green City, hivi sijui huu ubize nlio nao wa kufatilia kuhusu tafiti zangu ndio ili tonge liende mdomoni, nasahau kufatilia kuhusu nchi kiujumla na sekeseke tofauti, nimeskia mambo ya kina January Makamba, lakini sikubase kiundani kutokana na haka kamradi kafupi nikafanyako huku kanavyonilawiti, pesa mwanaharamu sana.

Hivi ni Mbeya tu au?
Maana kila nikienda sehemu ambayo nipo nafanyia project zangu mtaa mmoja huku ambao jamaa yangu ninayefanya nae hizo project yupo huku kunaitwa, mbalizi siku ya tatu leo kila nikija mchana hamna umeme mpaka saa 12 ya jioni.

Muda mwingine nakuwaga ilomba nako mambo ni hivyo hivyo.

Walau sio mbaya nikitoka eneo ambalo nimefikia (Isyesye) nikikwea bajaji mpaka kabwe naona warembo wa kinyakyusa na shepu zao ni balaa, hapo nitakwea, daladala kila mpaka huko mbalizi hapo warembo hawa hunipooza machungu kwa jinsi walivyofungasha sema Mwenyezimungu fundi sana.

MUNGU awape nini huu mkoa kwa ukarimu🙌

Ndaga
 
Watu wanaonyoa nywele zote kichwani sio wa kuwaamini. Tunatiana hasara tu na kutukosesha hela.
 
Kama utafanikiwa kupata sehemu karibu na nyumba za watu waliochukulia umeme line moja na hospitali ya Meta (Meta Referral Hospital) hutojutia kabisa.

Katika line zote za umeme ni hii pekee inayoheshimiwa almost 100%
 
Kama utafanikiwa kupata sehemu karibu na nyumba za watu waliochukulia umeme line moja na hospitali ya Meta (Meta Referral Hospital) hutojutia kabisa.

Katika line zote za umeme ni hii pekee inayoheshimiwa almost 100%
Daaah hawo wana bata sana
 
Si Mbeya peke yake ni karibia kila mji unahujumiwa
 
Back
Top Bottom