Amavubi
JF-Expert Member
- Dec 9, 2010
- 30,146
- 13,216
Hii imetokea nchini Cambodia.Baba amfunga mtoto wake kwenye mti mtaani kwa mnyororo na kufuli .Kisa hakwenda shule badala yake alikuwa mtaani kwenye internet cafe anacheza video game.Mtoto huyo mwenye umri wa miaka 13 alifungwa hapo mtini ili watu wamuone wamcheke na akome tabia ya kutokwenda shule.Majirani walipiga simu polisi na baba yake kukamatwa kwa kosa la child abuse.
Hii haina tofauti na mzazi mwenye mtoto anaeshindwa kujizuia kutoa haja ndogo kitandani.Wapo wazazi wanaomdhalilisha mtoto kwa kumwanika hadharani watoto wenzake wamwimbie ''kikojozi,kakojoa na nguo kazitia moto''Wazazi wenye tabia hii mkome kabisa kwani hujui kwa kiasi gani unamdhalilisha mtoto wako na kumnyanyasa kisaikolojia.