Original Pastor
JF-Expert Member
- Nov 14, 2007
- 1,274
- 50
Habari wa JF mimi namshukuru mungu kwa kufika mwaka 2010 ila tuwaombee wale ambao hawakufika au wapo Hospitali wana matatizo mbalimbali. Sasa hii habari nimeipokea si kwa Masikitiko bali Furaha na Uzuni vyote vimekuja Pamoja. Kwani nakumbuka Huyu Rais wa Bank ya Dunia alishawahi kuja Manzese na kutoa Msaada Nyumba zote zijengwe vyema na Mitaa iweke vizuri cha Kushangaza walikuja na pesa ziliingia kwenye Kampeni ya Uchaguzi sasa Sielewi na Mh. Keenja hili analijua sasa anakuja tena Tanzania Dar es salaam Kutembelea Manzese kuna nini hu
ko? na je anakuja kukagua au kutoa tena msaada?? Someni hii source Mtanzania Daima
WAKATI Rais wa Benki ya Dunia, Robert Zoellick anatarajia kuzuru Manzese jijini Dar es Salaam wiki ijayo, wajumbe wa mitaa ya Mwembeni na Midizini wamegoma kushiriki shindano la usafi kwa mitaa minane ya kata hiyo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwa sharti la kutotaja majina yao gazetini, wajumbe hao walisema hatua ya kufanya usafi ni ya zimamoto kwa sababu tukio hilo linatakiwa kufanyika mara kwa mara.
Walisema pamoja na kutolewa kwa shindano hilo, lakini mitaa hiyo haikidhi haja ya kuwa mitaa licha ya kuwekwa kwenye ratiba ya kutembelewa na Zoellick.
Mshindi wa kwanza wa shindano hilo anatarajiwa kuzawadiwa sh 150,000 wakati mshindi wa pili atajinyakulia vifaa vyenye thamani ya sh 100,000.
Mitaa iliyotajwa kushiriki shindano hilo ni Uzuri Chakula bora, Mnazi Mmoja, Mvuleni, Kilimani, Muungano, Manzese Uzuri, Midizini na Mwembeni. Hata hivyo mitaa ya Mwembeni na Midizini imegoma kushiriki.
Walisema kabla ya ujio huo, wameshauri Ofisi ya Waziri Mkuu itembelee mitaa ya Manzese na ijionee hali ilivyo kwa sasa.
Mradi huo umefadhiliwa na Benki ya Dunia ambayo ilitoa sh milioni 600, Halmashauri ya Kinondoni ilitoa sh milioni 334 na wananchi walitakiwa kuchangia sh milioni 334.
ko? na je anakuja kukagua au kutoa tena msaada?? Someni hii source Mtanzania Daima
WAKATI Rais wa Benki ya Dunia, Robert Zoellick anatarajia kuzuru Manzese jijini Dar es Salaam wiki ijayo, wajumbe wa mitaa ya Mwembeni na Midizini wamegoma kushiriki shindano la usafi kwa mitaa minane ya kata hiyo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwa sharti la kutotaja majina yao gazetini, wajumbe hao walisema hatua ya kufanya usafi ni ya zimamoto kwa sababu tukio hilo linatakiwa kufanyika mara kwa mara.
Walisema pamoja na kutolewa kwa shindano hilo, lakini mitaa hiyo haikidhi haja ya kuwa mitaa licha ya kuwekwa kwenye ratiba ya kutembelewa na Zoellick.
Mshindi wa kwanza wa shindano hilo anatarajiwa kuzawadiwa sh 150,000 wakati mshindi wa pili atajinyakulia vifaa vyenye thamani ya sh 100,000.
Mitaa iliyotajwa kushiriki shindano hilo ni Uzuri Chakula bora, Mnazi Mmoja, Mvuleni, Kilimani, Muungano, Manzese Uzuri, Midizini na Mwembeni. Hata hivyo mitaa ya Mwembeni na Midizini imegoma kushiriki.
Walisema kabla ya ujio huo, wameshauri Ofisi ya Waziri Mkuu itembelee mitaa ya Manzese na ijionee hali ilivyo kwa sasa.
Mradi huo umefadhiliwa na Benki ya Dunia ambayo ilitoa sh milioni 600, Halmashauri ya Kinondoni ilitoa sh milioni 334 na wananchi walitakiwa kuchangia sh milioni 334.