Hii Imekaaje? Rais wa Bank ya Dunia Kudhuru Manzese.

Original Pastor

JF-Expert Member
Nov 14, 2007
1,274
50
Habari wa JF mimi namshukuru mungu kwa kufika mwaka 2010 ila tuwaombee wale ambao hawakufika au wapo Hospitali wana matatizo mbalimbali. Sasa hii habari nimeipokea si kwa Masikitiko bali Furaha na Uzuni vyote vimekuja Pamoja. Kwani nakumbuka Huyu Rais wa Bank ya Dunia alishawahi kuja Manzese na kutoa Msaada Nyumba zote zijengwe vyema na Mitaa iweke vizuri cha Kushangaza walikuja na pesa ziliingia kwenye Kampeni ya Uchaguzi sasa Sielewi na Mh. Keenja hili analijua sasa anakuja tena Tanzania Dar es salaam Kutembelea Manzese kuna nini hu
ko? na je anakuja kukagua au kutoa tena msaada?? Someni hii source Mtanzania Daima
WAKATI Rais wa Benki ya Dunia, Robert Zoellick anatarajia kuzuru Manzese jijini Dar es Salaam wiki ijayo, wajumbe wa mitaa ya Mwembeni na Midizini wamegoma kushiriki shindano la usafi kwa mitaa minane ya kata hiyo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwa sharti la kutotaja majina yao gazetini, wajumbe hao walisema hatua ya kufanya usafi ni ya zimamoto kwa sababu tukio hilo linatakiwa kufanyika mara kwa mara.
Walisema pamoja na kutolewa kwa shindano hilo, lakini mitaa hiyo haikidhi haja ya kuwa mitaa licha ya kuwekwa kwenye ratiba ya kutembelewa na Zoellick.
Mshindi wa kwanza wa shindano hilo anatarajiwa kuzawadiwa sh 150,000 wakati mshindi wa pili atajinyakulia vifaa vyenye thamani ya sh 100,000.
Mitaa iliyotajwa kushiriki shindano hilo ni Uzuri Chakula bora, Mnazi Mmoja, Mvuleni, Kilimani, Muungano, Manzese Uzuri, Midizini na Mwembeni. Hata hivyo mitaa ya Mwembeni na Midizini imegoma kushiriki.
Walisema kabla ya ujio huo, wameshauri Ofisi ya Waziri Mkuu itembelee mitaa ya Manzese na ijionee hali ilivyo kwa sasa.
Mradi huo umefadhiliwa na Benki ya Dunia ambayo ilitoa sh milioni 600, Halmashauri ya Kinondoni ilitoa sh milioni 334 na wananchi walitakiwa kuchangia sh milioni 334.
 
Rais wa Bank ya Dunia Kudhuru Manzese.
rekebisha heading yako....Umebadili mantiki ya thread broda!
I think you wanted to say kuzuru
 
how to editing eading? please nimejaribu nimeshindwa imenibidi nitume tena poleni kwa usumbufu
 
Hi!! Moderators Please rekebisha hiyo Heading ni Kuzuru(kutembelea) sio kudhuru

Asante nashukuru au Ifute maana nimetuma ingine sababu nilishindwa kurekebisha sawa mkubwa
 
Itabidi aandamane na Gavana wa BOT ili amwonyeshe wa-TZ wenzake wanakoishi! Asisahau kumpitisha uwanja wa fisi, halafu mapumziko yawe kwenye makao mapya ya Gavana!!
 
Kwanza wana haki ya kugoma.Kwa bahati mbaya sababu ya kugoma kwao sio ya msingi sana!Wangesema wanagoma kwa sababu sera za IMF ndizo zimewaletea umaskini waliokuwa nao kwa hiyo hawawezi kumshangilia na kumshabikia kiongozi huyo ningewaelewa.Kwanza anakwenda Manzese kufanya nini,si kwenda kuhakikisha kama kweli kazi ambayo wameikusudia inakwenda vizuri.Wajinga ndio waliwao!

Jamani nani mwenye akili timamu atamshabikia kiongozi wa IMF?NI WALE WAJINGA TU.

Habari wa JF mimi namshukuru mungu kwa kufika mwaka 2010 ila tuwaombee wale ambao hawakufika au wapo Hospitali wana matatizo mbalimbali. Sasa hii habari nimeipokea si kwa Masikitiko bali Furaha na Uzuni vyote vimekuja Pamoja. Kwani nakumbuka Huyu Rais wa Bank ya Dunia alishawahi kuja Manzese na kutoa Msaada Nyumba zote zijengwe vyema na Mitaa iweke vizuri cha Kushangaza walikuja na pesa ziliingia kwenye Kampeni ya Uchaguzi sasa Sielewi na Mh. Keenja hili analijua sasa anakuja tena Tanzania Dar es salaam Kutembelea Manzese kuna nini hu
ko? na je anakuja kukagua au kutoa tena msaada?? Someni hii source Mtanzania Daima
WAKATI Rais wa Benki ya Dunia, Robert Zoellick anatarajia kuzuru Manzese jijini Dar es Salaam wiki ijayo, wajumbe wa mitaa ya Mwembeni na Midizini wamegoma kushiriki shindano la usafi kwa mitaa minane ya kata hiyo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwa sharti la kutotaja majina yao gazetini, wajumbe hao walisema hatua ya kufanya usafi ni ya zimamoto kwa sababu tukio hilo linatakiwa kufanyika mara kwa mara.
Walisema pamoja na kutolewa kwa shindano hilo, lakini mitaa hiyo haikidhi haja ya kuwa mitaa licha ya kuwekwa kwenye ratiba ya kutembelewa na Zoellick.
Mshindi wa kwanza wa shindano hilo anatarajiwa kuzawadiwa sh 150,000 wakati mshindi wa pili atajinyakulia vifaa vyenye thamani ya sh 100,000.
Mitaa iliyotajwa kushiriki shindano hilo ni Uzuri Chakula bora, Mnazi Mmoja, Mvuleni, Kilimani, Muungano, Manzese Uzuri, Midizini na Mwembeni. Hata hivyo mitaa ya Mwembeni na Midizini imegoma kushiriki.
Walisema kabla ya ujio huo, wameshauri Ofisi ya Waziri Mkuu itembelee mitaa ya Manzese na ijionee hali ilivyo kwa sasa.
Mradi huo umefadhiliwa na Benki ya Dunia ambayo ilitoa sh milioni 600, Halmashauri ya Kinondoni ilitoa sh milioni 334 na wananchi walitakiwa kuchangia sh milioni 334.
 
Katika kumbukumbu zangu Maraisi wote wa Benki ya Dunia hupanga kutembelea sehemu zile za wakazi wa kawaida kabisa kuona ni jinsi gani wananchi hao wanafaidika na kuumizwa na sera zao. Kama sikosei ziara ya Manzese kwa Rais wa Benki ya Dunia si ya kwanza. Pia Rais wa Benki hiyo aliwahi kutembelea Kigamboni kwenye mitaa na shughuli za kawaida za wananchi.
Hata hivyo kwa wale wenye kumbukumbu, Waziri Mkuu wa Uingereza aliwahi kutembelea soko la Buguruni wakati huo akiwa waziri wa fedha http://news.bbc.co.uk/2/hi/uk_news/politics/4177281.stm
 
Back
Top Bottom