Hii Imakaaje? Maalimu Seif kaenda Uingereza!

Hii Imakaaje? Maalimu Seif kaenda Uingereza!

Madhara
Tujadili bei ya sukari hayo ya ziara huwezi kuyazungumzia maana hujui makusudio yake zaidi ya kutabiri tabiri. Magu kazuia sukari sasa watu vijijini wanaweka mananasi kwenye Maji kufanya chai, uswahilini maandazi na vitumbua bei juu. Lumumba jadilini hayo wananchi wanaumia
ya sukarim sijui unayajua?!?!? Safi sana anatuondolea maradhi!
 
Angalia Katiba, sheria na kanuni utaelewa. Hakuna kati ya vyote hivyo vinarushusu uchaguzi kurudiwa. Na hata kama ndivyo vipi zile chaguzi za wawakilishi waliopewa hata vyeti na hata bila mgombea wala chama chochote kulalamika napo walijitangazia? Kuhusu pendekezo la kukimbilia mahakamani kupinga uchaguzi wa marudio, "... Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar pamoja na Katiba haziruhusu kupingwa au kuchunguza ZEC kimahakama".
Hata Kama wangeenda Mahakama wasingepata haki mbele ya Mfalume Dr Shein, Zanzibar kwa sasa inatawaliwa kidikiteta ni Utawala wa mabavu.
 
HUWA SITUMII LUGHA YA MATUSI KAMWE NA SIO KAWAIDA YANGU LAKINI KWA HILI, KULA, KANYE KISHA ULALE HUJUI KITU. NYAMA WEE. NGOJA HATA KAMA NI MIAKA 10000+ IKO SIKU YATAWATOKEA PUANI.
Hahahaaa...PMM umenichekesha!
 
Aliyenikaririsha kwamba Lowasa ni fisadi ni Slaa, Tundu Lisu, Mbowe, Lema, Kubenea na wala siyo Membe wala Nape, kwa kifupi kama hawa watu yaani Lisu, Kubenea, Mbowe, Slaa, na Lema wasingekuwepo Duniani mimi leo hii nisingejua kama Lowasa ni fisadi achilia mbali hata kulitumia neno lenyewe fisadi kwangu nililisikia kwa mara ya kwanza ktk kwa hao niliowataja hapo juu yaani Lisu, Slaa, Kubenea, Mbowe na Lema!

Saa ngapi unaenda kuchukua pesa yako pale Lumumba? Naona una kiu sana mpaka povu linakutoka mdomoni
 
Kaenda kuwambia kuwa Serikali imeamua kupoteza pesa bure kisa wajanja wachache wameandaa bajeti ya kujipatia pesa kwa kisingizio cha kurudia uchaguzi,matokeo Zanzibar yanajulikana hakuna haja ya kurudia Uchaguzi ni bora wamtangaze Shein kuwa ni Rais wa milele na hao JWTZ wapo huko kuendeleza Udikteta, balozi wa Uingereza kaenda ikulu kumzuga Magufuli lakini chini kapeti hawakubaliani na kinachotendeka Zanzibar.
Ndoto hizi
Hehehe kweli MBOWE ana mtaji du!
 
Acheni MUNGU aitwe mungu, yaani kuna watu wengine kwa ujinga wao kama Riziki na uhai ungekuwa unamilikiwa na binadamu, bila shaka leo sijui kama wangekuwa hai!
 
Sultani alivotimuliwa alienda wapi jamaneeeeee.....!!!!

Au tuseme alitawala akitokea wapi.....!!!!

Uingerezaaaaaaaaa......!!!!
 
Sina katiba ila ukinijulisha inasemaje pindi uchaguzi ukiharibika nitashukuru!
Angalia Katiba, sheria na kanuni utaelewa. Hakuna kati ya vyote hivyo vinarushusu uchaguzi kurudiwa. Na hata kama ndivyo vipi zile chaguzi za wawakilishi waliopewa hata vyeti na hata bila mgombea wala chama chochote kulalamika napo walijitangazia? Kuhusu pendekezo la kukimbilia mahakamani kupinga uchaguzi wa marudio, "... Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar pamoja na Katiba haziruhusu kupingwa au kuchunguza ZEC kimahakama".
 
Taafira yako ni potofu mwandishi tena haina hata muelekeo.... Ni juzi tu wana diplomasia wa mataifa mengi ya nje, mabalozi wakiwepo wa kiingereza waliandika kwa pamoja kauli ya kukemea uchaguzi wa marudio, leo hii ati unasema balozi wa uingereza amekutana na pombe kumpongeza kwa kazi aifanyayo ikiwamo uamuzi wa marudio ya uchaguzi Zanzibar. B******T!!

Yaliyozungumzwa wala huyajulikani lakini nina hakika 100% hayakuwa pongezi za uamuzi wa uchaguzi wa marudio Zanzibar. Sababu unaona picha za watu wanapeana mikono usidhani kama ati hapo ndio penye kuonyesha ya kuwa mkutano ulikuwa wa mapongez! That's just sad!
 
Maalim Seif yuko Uingereza kushitaki kwa Wazungu kuhusu Unguja na Pemba hapo hapo Balozi wa Uingereza ambaye ndiye mwakilishi wa Serikali wa nchi hiyo leo katinga Ikulu kumsalimia Raisi Magufuli na kumletea salamu za pongezi ktk kwa Mkuu wa Serikali anayoiwakilisha hapa nchini, sasa Maalimu katumwa na fisadi Lowasa na wenzake huko Uingereza ni nani hata atawasikiliza?

Watu wanahangaika, mimi ningewashauri CUF wakubali tu kufanya Uchaguzi na wapige Kampeni kikweli kweli ili angalau labda wanaweza kufika mbali au nani anajua labda hata kuwemo kwenye Serikali ya Umoja na CCM lkn kususia ni kwamba CCM inachukuwa Uongozi kwa 100% na hakuna kitu CUF au fisadi Lowasa &Co. watafanya kwani kama ni Jeshi liko chini ya Raisi wa JMTZ na ameshasema uchaguzi urudiwe na atakayeleta fyoko basi atafyokolewa, na kama ni Wazungu ambao ndiyo walikuwa wanawategemea ndiyo hao tena wanakuja Ikulu kumpongeza Raisi Magufuli kwa kazi anayoifanya hii ni pamoja na uamuzi wa marudio uchaguzi wa Unguja na Pemba kesho pia mtamuona Mwakilishi wa EU anaenda Ikulu kwa Magufuli, balozi wa Ujapani, Marekani, Uchina n.k

Hivyo CUF na ukawa hakuna kitu mtafanya, kubalini tu yaishe aliyekuzidi kakuzidi tu, CCM wana Raisi hivyo wameshika mpini ndiyo hivyo tena, mkileta fyoko mtafyokolewa kama Besigye na hakuna kitu mtafanya!
Mawazo yako mazuri , Pamoja na pongezi balozi wa Uingereza kasema Nini?Hawataki kushiriki uchaguzi why msiwaache
 
Mawazo yako mazuri , Pamoja na pongezi balozi wa Uingereza kasema Nini?Hawataki kushiriki uchaguzi why msiwaache


Kwani ni nani kawalazimisha kushiriki uchaguzi? Mpaka leo hii hawajajitoa rasmi kikanuni na kiutaratibu kwenye Uchaguzi kulingana na taarifa ya Tume ya Unguja na Pemba!
 
Tujadili bei ya sukari hayo ya ziara huwezi kuyazungumzia maana hujui makusudio yake zaidi ya kutabiri tabiri. Magu kazuia sukari sasa watu vijijini wanaweka mananasi kwenye Maji kufanya chai, uswahilini maandazi na vitumbua bei juu. Lumumba jadilini hayo wananchi wanaumia

Wakijadili hayo ujira wao uko hatarini mkuu. Hawa jamaa wa Lumumba wanafanya kazi kwa maagizo hawawezi kujadili post yoyote wasiyoelekezwa!!!!!!!!!!!!
 
Kwani ni nani kawalazimisha kushiriki uchaguzi? Mpaka leo hii hawajajitoa rasmi kikanuni na kiutaratibu kwenye Uchaguzi kulingana na taarifa ya Tume ya Unguja na Pemba!
kulingana na taarifa ya tume ya unguja na Pemba? Ile tume iliyokosa sifa za kusimamia uchaguzi? Hamna hata moja watakalosema ZEC linaloaminika... Mfano mdogo tu ni kuwa hata wagombea wengine waliokurupuka na kukiuka msimamo wa vyama vyao mfano yule Ahmad Rashid, ashaachishwa uanachama wa chama anachokisimamia kugombea uraisi, lakini tume hiyo hiyo imeng'ang'ania ya kuwa eti huyu ana sifa za kugombea uchaguzi? Anagombea yeye kibinafsi akiwakilishwa na chama gani sasa???? CCM version II au?

Hiyo ZEC ni kitengo tu cha chama tawala. Washapoteza sifa. Kama kufuata sharia walishaivunja tangu hapo zamani na kuinyea.... Narudia, hoja yako ni kama ushuzi tu kwenye hurricane mwandishi
 
Wewe Magufuli ameisha kufyokoa mara ngapi? Maana inaonekana unajua sana anavyofyokoa..
 
Akutukanae hakuchagulii tusi. H ivi umekosa adamu ya kufafanisha demokrasia ya Tanzania kuwa sawa na ya Uganda na kwa hivyo alivyofanyiwa Bisigye na maendelezo yake pia wafanyiwe wapinzani hapa Tanzania.
Tatizo wewe hujui kinachoendelea hapa duniani unakurupuka tu. Kama hujui uliza, na kwa hili hata Kisonge wanalijua pia unaweza kuwauliza. Maalim Seif ameenda Uingereza kwa ajili ya matibabu
 
lumumba inaharibu afya ya akili ya nguvu kazi ya taifa.Hebu ona huyu anavyojitoa ufahamu na kuandika ujinga.Anasema angalau cuf wafanye kampeni walau wanaweza pata nafasi ya kuunda serikali ya umoja wa kitaifa,huu ni upumbavu.Kwann gharama itumike kurudia uchaguzi wakati mnajua fika hamuwezi kubali kushindwa?shame on u
 
Back
Top Bottom