Hii boat iliishia wapi?

Hii boat iliishia wapi?

Tiba

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2008
Posts
4,607
Reaction score
3,187
Wadau,

Miaka michache iliyo pita, kuna boat ilinunuliwa na tajiri mmoja kufanya safari zake kati ya Mwanza na Bukoba. Boat hii ilileta gumzo kubwa kwani Magufuli kama waziri wa ujenzi alikataa hiyo boat isisafirishwe kupitia barabara zetu kutoka Dar kwenda Mwanza kwa madai ya kulinda barabara. Hatimae boat hii ilisafirishwa kupitia Mombasa na mwisho ilifika Mwanza na kuanza safari zake kati ya Mwanza na Bukoba.

Nani anayejua hii boat ilipatwa na nini na kwa sasa iko wapi?

Tiba

Kwa ninachokijua, baada ya kuletwa Mwanza zilianza safari kama kawaida, ratiba ilikuwa kutoka Mwanza saa 3 asubuhi mpaka Bukoba saa 9 mchana, nyingine ilikuwa inatoka kwa muda ule Bukoba, baadae ikawa saa 1, then saa 6 mza, thn saa 7, saa1 bkb, i mean go and return

Ajali ya kwanza ilipigwa na dhoruba kali kiasi cha kushindwa kufika kwa wakati, baada ya saa 6 za ratiba ikafka baada ya saa 10, (kumbuka kuletwa kwake kulitawaliwa na figisufigisu nyingi ivo iyo ikawa sababu ya kusimamishwa rasmi), boti ya pili ambayo iliendlea kufanya kazi ilipata tatzo la kuzimika injin ikiwa katikati ya ziwa siku moja mm nimetoka bukoba, ilibaki huko muda mwingi kuanzia asubuh saa 4, ilipata msaada saa 11, jion na abiria walifka mwanza saa 4, usiku, baada ya kuvutwa na mv ukerewe,

Baada ya pale boti zile zikasimamishwa rasmi tatizo jingine lilikuwa ni viwango vya nauli mfano kipindi icho nauli to Bukoba victoria ilikuwa
Daraja la tatu 8600
daraja la pil kukaa 10600
Daraja la pili kulala 12600
daraja la kwanza 23500
cabin ilikuwa 35000

Mabasi kipindi icho hayakuwa meng, mohamed trans na bunda ilkuwa arround 12000~15000, Wakati izo boti naul ilkuwa 23000~35000 kwa madaraja ya kwanza. Kwa hiyo kwa namna fulan kuahirbka kwa boti izo ambazo tuliambiwa zitapunguza muda mwngi wa safari ilikuwa kama kujichimbia kaburi kwa wamiliki.

Kifupi kulikuwa na comftability ya hatari, zilisafiri mchana watu kupata raha na kuangalia mandhari ya ziwa victoria, tofaut na meri ambayo ufanya safari usiku, haikuwa tofauti na kupanda fastjet ukiachilia mbali suala la muda. Boti hizi pia zilipunguza muda wa safari kutoka saa 13 majini ( mv victoria) na saa 14-15 (mv serengeti) mpaka saa 6.
 
Ilisitisha safari maana kwenye injini yake iliunguza kifaa kwa kitaalamu kinaitwa ropgifiboreingene
 
Zilikuwa boti 2, ziliruhusiwa kupita kenya na zikafika mwanza kupitia bandari ya kisumu baada ya kuruhusiwa na raila odinga
 
Hiko kifaa kiliungua baada ya kugonga mwamba unaoitwa frooktotostabolization mofatti

Jamani JF kwa vituko hamna mfano, yaani nimecheka mpaka basi. Kwa hiyo hiyo boat iko wapi kwa sasa na inatumikaje?

Tiba
 
Zilikuwa boti 2, ziliruhusiwa kupita kenya na zikafika mwanza kupitia bandari ya kisumu baada ya kuruhusiwa na raila odinga

Ni kweli zilipita Kenya na hatimae kufika Mwanza, sasa ziko wapi na zinatumikaje?

Tiba
 
Ilisitisha safari maana kwenye injini yake iliunguza kifaa kwa kitaalamu kinaitwa ropgifiboreingene

Kwa hiyo hicho kifaa hakijapatikana spare yake mpaka leo au?

Tiba
 
Ilisitisha safari maana kwenye injini yake iliunguza kifaa kwa kitaalamu kinaitwa ropgifiboreingene

Hiko kifaa kiliungua baada ya kugonga mwamba unaoitwa frooktotostabolization mofatti

Mwanamke mwenye mimba changa anaweza kupata complications kama akiyasoma hayo majina mpaka mwisho Tiba hivi vingine hivi tuviache tu kama vilivyo
 
Last edited by a moderator:
Nakumbuka hii ishu ya boti ilileta uhasama sana hadi mijahidina ikawa inatokwa povu et magufuli akuziruhusu zisipite kwenye barabara zetu kwa sababu mwenye boti Muislamu. Naye Magufuli akajitokeza bila kumung'unya mdomo na kusema ni yeye kasema hapana kama vp mniombee albadili
 
Mwanamke mwenye mimba changa anaweza kupata complications kama akiyasoma hayo majina mpaka mwisho Tiba hivi vingine hivi tuviache tu kama vilivyo

Afadhali na wewe umeona hiyo ndugu yangu. Hayo majina ni hatari. But seriously hii boat iliishia wapi?

Tiba
 
Last edited by a moderator:
Nakumbuka hii ishu ya boti ilileta uhasama sana hadi mijahidina ikawa inatokwa povu et magufuli akuziruhusu zisipite kwenye barabara zetu kwa sababu mwenye boti Muislamu. Naye Magufuli akajitokeza bila kumung'unya mdomo na kusema ni yeye kasema hapana kama vp mniombee albadili

Ni kweli ilikuwa ni issue iliyopamba vichwa vya habari za magazeti na hata hapa JF. Sasa mwisho wa hii boat ulikuwaje maana sijaisikia siku nyingi sana.

Tiba
 
Hiko kifaa kiliungua baada ya kugonga mwamba unaoitwa frooktotostabolization mofatti
hiki kifaa nacho kilikuwepo kwenye titanic nazan kwa kitaalam wakat hule kilijulikana kama MAFIZIKOLO-AMPHIBIAN DECLOFENAC
 
Ni kweli ilikuwa ni issue iliyopamba vichwa vya habari za magazeti na hata hapa JF. Sasa mwisho wa hii boat ulikuwaje maana sijaisikia siku nyingi sana.

Tiba
hii nchi tiba achana nayo tu jins ilivyo uhenda labda hata boti zenyewe hazikuwepo
 
Zipo mwanza sielewi fukwe gani lakini nikiwa naenda ukerewe naziona zimepaki,
 
Back
Top Bottom