Hii ajali jana nusura itutoe roho

Hii ajali jana nusura itutoe roho

Jana Asubuhi na mapema nilipanda gari la Isamilo linalotokea Iringa kwenda Mwanza. Mvua ilikuwa inanyesha kubwa sana.

Tulipofika mlima Nyang'oro Dereva wa Gari alikuwa anakata zile kona za Nyang'oro kama vile ni wakati wa kiangazi na kama anapanda mlima wakati alikuwa anashuka. Kufika kona ya mwisho gari likamshinda likapaa juu na kuanguka.

Bahati nzuri hakuna aliyeumia sana isipokuwa mama na kijana mmoja ambapo yule mama alipelekwa Hospitali ya Dodoma kwa Gari la TANAPA na kijana anajitafutia matibabu mwenyewe.

Mungu yu mwema leo nipo hai kuandika habari hii.

View attachment 1344937
Muda mfupi baada ya Gari hilo kuanguka.


Hv huyo Dereva mmemuacha kweli walau
Mngemtengua miguu abaki na kumbukumbu... maana hana tofaut na mtu anaekufyatulia risas ikakukosa maana alikuwa ana nia ya kuwauwa ilitakiwa achezee kichapo kitakachompa ukilema walau wa vidole abaki na kumbukumbu hajui familia ngapi angeziacha yatima hajui maisha ya wangap angeyaharibu watoto kubaki bila wazaz

.. ajali nyingi zinasababishwa na uzembe ingawa siri ya kifo anayo Muumba ila kuna wakat nahs tunamsingizia mzee wa watu.. maana alitupa maarifa ya kutawala dunia na vilivyopo ingawa hatuna uwezo wa kuumba kiumbe hai ila
Tunajua jinsi ya kukitoa uhai.

Na hata jinsi ya kutibu maradhi ndo msingi wa maarifa aliotupa so vifo vya kizembe ni kujitakia. Kumbuka alisema WATU WANGU WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
  • Thanks
Reactions: 7ve
Kufika 2025 dar itakuwa Kama lamu
Unataka kuniambia hata hizi ndito zinazo tingisha mikia kama ya sungura zitakua zinavaa maburka? Hizi bar tam tam za Kinondoni nazo zitakua magofu?
 
Pole sana mwambie huyo mdada mwenye tshert ya orange Nampa hi
 
ili swala la abiria kujihudumia wenyewe wakati wakati magari yamekatiwa bima ikiwamo za kuwalinda abiria si sahihi kwani abiria wengi hawajui wakipata ajali wanapaswa kulipwa fidia ya matibabu
 
asee pole mkuu, pole kwa majeruhi pia

Sent from my SM-J700H using Tapatalk
 
Ni jambo la kushukuru mkuu




Hajaacha kuniwekea mafuta ya taa kwenye ubwabwa
 
Kama kawaida yetu wabongo kutochukua hatua mpk tupatwe na janga.Mkuu ulishindwa nn kumpa onyo dereva mpk anaenda kuwabwaga?kuna siku natoka morogoro nimepanda new force nikawa nasikia mtu anaongea na cm kwa sauti huku anacheka nikamuuliza abiria mwenzangu nani huyu anapiga kelele hivi akasema dereva huyo aisee nilisimama kama upepo nikamfata pale nikamwambia naomba wakati umetupakia sisi abiria usithubutu tena kuongea na hiyo simu yako.Mbona alitii mpk tunafika dar hakuongea na cm tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
Point hii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili la madereva wa vyombo vya usafiri kwenda mwendo mdogo sana wanapokuwa wanaenda mwendo kasi bila kuzingatia sheria, na abiria wanapolalamika limeshanikuta mara nyingi sana, lakini sikuwa najua kama kwenda mwendo mdogo bila sababu ni kosa pia.
Changamoto inabaki katika kutoa taarifa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom