Hii ajali jana nusura itutoe roho

Hii ajali jana nusura itutoe roho

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,176
Reaction score
48,460
Jana Asubuhi na mapema nilipanda gari la Isamilo linalotokea Iringa kwenda Mwanza. Mvua ilikuwa inanyesha kubwa sana.

Tulipofika mlima Nyang'oro Dereva wa Gari alikuwa anakata zile kona za Nyang'oro kama vile ni wakati wa kiangazi na kama anapanda mlima wakati alikuwa anashuka. Kufika kona ya mwisho gari likamshinda likapaa juu na kuanguka.

Bahati nzuri hakuna aliyeumia sana isipokuwa mama na kijana mmoja ambapo yule mama alipelekwa Hospitali ya Dodoma kwa Gari la TANAPA na kijana anajitafutia matibabu mwenyewe.

Mungu yu mwema leo nipo hai kuandika habari hii.

1581093738732.png



1581093831994.png
 
Kama kawaida yetu wabongo kutochukua hatua mpk tupatwe na janga.Mkuu ulishindwa nn kumpa onyo dereva mpk anaenda kuwabwaga?kuna siku natoka morogoro nimepanda new force nikawa nasikia mtu anaongea na cm kwa sauti huku anacheka nikamuuliza abiria mwenzangu nani huyu anapiga kelele hivi akasema dereva huyo aisee nilisimama kama upepo nikamfata pale nikamwambia naomba wakati umetupakia sisi abiria usithubutu tena kuongea na hiyo simu yako.Mbona alitii mpk tunafika dar hakuongea na cm tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom