encyclopaedia Tanzaree
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 513
- 397
Bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu (HESLB) yapiga ramli, hicho ndicho unaweza kusema baada ya kutoa awamu ya kwanza ya majina ya waliopangiwa mikopo 2017/18 ambapo kati ya maombi 32,495, waliopangiwa mikopo ni wanafunzi 10,196.
Mkurugenzi mtendaji wa HESL amesema orodha hiyo ya wanafunzi 10,196 imepatikana baada ya kupokea na kuchambua awamu ya kwanza ya majina ya wanafunzi 32,495 waliopata udahili katika chuo kimoja.
Pia amesema kwa jumla Sh108.8 bilioni zitatolewa kwa wanafunzi 30,000 wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2017/2018.
Sasa swali ni je, wamejuaje kama wanafunzi 30,000 ndo watakaokuwa na uhitaji hadi mwisho wa zoezi kama bado hawajamalizia kupitia maombi yote?
Je, watakaokata rufaa watakuwa kundi lipi?
MY TAKE.
Bodi ya mikopo haitendi haki ktk utoaji wa mikopo, na hili limedhihirishwa kwa wao kutabiri idadi ya watu wenye uhitaji kabla hata hawajapitia maombi yote.
Mkurugenzi mtendaji wa HESL amesema orodha hiyo ya wanafunzi 10,196 imepatikana baada ya kupokea na kuchambua awamu ya kwanza ya majina ya wanafunzi 32,495 waliopata udahili katika chuo kimoja.
Pia amesema kwa jumla Sh108.8 bilioni zitatolewa kwa wanafunzi 30,000 wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2017/2018.
Sasa swali ni je, wamejuaje kama wanafunzi 30,000 ndo watakaokuwa na uhitaji hadi mwisho wa zoezi kama bado hawajamalizia kupitia maombi yote?
Je, watakaokata rufaa watakuwa kundi lipi?
MY TAKE.
Bodi ya mikopo haitendi haki ktk utoaji wa mikopo, na hili limedhihirishwa kwa wao kutabiri idadi ya watu wenye uhitaji kabla hata hawajapitia maombi yote.