HESLB bado hawajatoa VRF kwenye salary slip

Huo utofauti ukoje?unajua Sisi wengine tupo mikoani kufika makao makuu ni mbali kidogo

Kumbuka sasa hivi VRF na penalty zimefutwa.

Hivyo, automatically kiwango cha pesa unachodaiwa kitabadilika. Hapo ndio inconsistency inapotokea. Kuna watu madeni yao ni makubwa lakini si kwa sababu ya riba au penalty bali uingizaji mbaya wa taarifa za madeni.

Verified loan statement inaonesha mchanganuo uliokamilika kama ifuatavyo

i) Ulikopeshwa shilingi ngapi.

Hapa utapewa taarifa kwa mchanganuo. Kwa mfano kiasi cha tuition fee, meals and accommodation, research fund, practical training n.k ulichokopeshwa.

ii) Umerejesha kiasi gani hadi sasa.

Hapa utaoneshwa marejesho yako ya kila mwezi. Kuna watu wanadaiwa pesa nyingi kumbe kosa ni la muajiri kuna miezi hakuwa anapeleka pesa.

Na hii inatokea hata kwa waajiriwa wa serikali pia. Kwa hiyo usijipe moyo wewe ni mwajiriwa wa serikali.

Wewe nenda tu kapate statement yako ujue hali ya mkopo wako.
 
Umemjibu vyema uyu jamaa atakua bodi ndo maana anatetea uzembe wanaoufanya
 
Sasa hili ni kosa la nani? Mtumishi au loan board?

Mkuu kwani wewe unahitaji kumjua mwenye kosa ni nani au unataka deni lako liishe?

Collective justice ni ngumu sana, hasa kwenye kesi kama hizi. Wewe nenda bodi kaweke mambo sawa, otherwise watakukata deni litaisha na wataendelea tu kukukata.

Kitakachofata ni wewe kuanza kudai pesa waliyozidisha kukukata kimakosa.

Hapo sasa ndio utajua kuwa viatu huwa kweli vinaisha ukivitembelea sana.

Ila ni kama alivyosema mkuu hapo juu. Kupanga ni Kuchagua. The ball is in your court.
 

Na nilisikia kwamba kuna value retention fee before 1 May 2021 kwamba nayo imeesabiwa je hili ni kweli?
 
Swali linajibiwaje na swali, ndugu? Katika wote waliochangia hapa, yaani umeona mimi ndio naweza kuwa na taarifa hiyo! Uliona na mimi niliuliza swali - maanake sina taarifa.
Je vrf wameifuta yote au wamebakiza kiasi?
 
Hii bodi ina mauzauza sana. Kuna cases zinatafarisha kwelikweli!
1. Mdau 1 alikuwa na deni la 5m (alikopeshwa 11m, na kuanza kulipa 2016), ghafla kwenye system inasoma laki 6. Sijui kama kuna formula yenye kuweza kufafanua hilo.
2. Mdau 2 alikopeshwa 8 m, akaanza kulipa 2014, mpaka sasa bodi inatambua kuwa HAJAWAHI KULIPA HATA SENTI, slip inasomeka 1.5m Kama deni.
NB. Niishie hapo kwa sasa
 
Umefanya udadavuzi mzuri mno na ndivyo ilivyo!
 
body wanatakiwa wataarifu utumishi warekebishe madeni kwenye salary slip sababu hizi slip tunazitumia bank na maeneo mengine kama kupata mikopo ya maendeleo nk., pia unaweza wauzia bank huo mkopo mf mimi slip inaonyesha nadaiwa 16.7m , board statement baada ya kuondoa tozo zao nadaiwa 8.5m, hii 8.5m ikitokea kwenye salary slip ni ahueni kubwa kwan itarahisisha kukopa zaid ie pesa kubwa zaid kwa ajir ya maendeleo na bank kuchukua huo mkopo wa heslb
 
Hivi mtu ukishindwa kuafikiana na bodi kuna chombo cha juu unaweza kwenda au ndio mahakamani tu?
 
Hivi waweza angalia deni lako kupitia web Yao...?
Mana nimejaribu ila nimeshindwa ona linakaa sehemu gani..!
Kama hutojali naomba unielekeze mana nilishafwatilia hata control number kwa simu huko mwanza ila maelezo walinipa sijaona matokeo yake...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…